Nilikuwa na mpango wa kufungua biashara Tanzania kwenye mambo ya afya lakini mitambo yangu yote inahitaji umeme wa uhakika. Wataalamu wa vifaa wameniambia umeme ukizimazima unaweza kuaribu vifaa vyangu. Imekuwa vigumu sama kufanya maamuzi ya biashara Tanzania kwa sasa kwani pamoja na mikimbizano yote ya kufungua biashara vitu muimu kama umeme wa uhakika hatuna. Sisi vijana tulio nje tumekuwa watu wa kusemwa tu kuanzia kwa familia mpaka kwa wananchi kwamba turudi Tanzania mambo mazuri na eti sisi tunacheza tu huku nje kwani watu nyumbani wana maaendeleo sana. Sasa tunajaribukurudi na miradi ya kisasa ya kusaidia wananchi lakini serikali na mipango yake ya umeme haieleweki. Hii ndugu zangu inasikitisha sana kwasababu Tanzania inaonekana wazi kwamba kikwazo cha maendeleo si Wananchi, si mtaji, si biashara bali ni mipango ya serikali ambayo mtu binafsi huwezi kufanya.
Mimi nawaomba wale wadau ambao wanapigia kelele vijana warudi kufanya biashara kwenye mazingira haya waangalie kwani bongo palivyo utaishia kula mtaji na biashara haita simama kabisa. Je ni lini Tanzania itakuwa na umeme na maji ya uhakika? maana kama ni miaka mitano basi tufanye shughuli nyingine!. Kwa mawazo yangu kama ni mtu mwadilifu na unafanya shughuli zako kiwazi bila rushwa ni vigumu sana kufanikiwa Tanzania kwa mazingira yaliyopo sasa. Vilevile watu wengi ambao wanakuambia mambo ni mazuri inawezekana ni mtu kaanza kanyumba kake pale Tanzania na kwasababu wewe wa nje huna nyumba wanafikiria unabeba mabox siku nzima! na unacheza. 90% ya Watanzania niliokutana nao wanadanganya au kukuza mambo pasipo sababu ya uhakika!. Vijana wengi wanakutana kunywa bia na vibatari kwa wakati mwingine na kugigamba kwa idadi ya pesa walizonazo bank nyingi za kijanja janja na kujisifia idadi ya wanawake walionao!!. Kama una wazazi walio na umri wa juu kuwa makini kwani hata pale muhimbili ni pa kubabaisha tu na watu wenye uwezo wanaenda India kutibiwa vitu vidogo kama kisukari. Kwa ujumla Tanzania ni nchi ambayo haiko serious na viongozi wengi ni wabinafsi wa hali ya juu na huwezi kuishi bila kudanganya!. Mungu ibariki Tanzania
Mimi nawaomba wale wadau ambao wanapigia kelele vijana warudi kufanya biashara kwenye mazingira haya waangalie kwani bongo palivyo utaishia kula mtaji na biashara haita simama kabisa. Je ni lini Tanzania itakuwa na umeme na maji ya uhakika? maana kama ni miaka mitano basi tufanye shughuli nyingine!. Kwa mawazo yangu kama ni mtu mwadilifu na unafanya shughuli zako kiwazi bila rushwa ni vigumu sana kufanikiwa Tanzania kwa mazingira yaliyopo sasa. Vilevile watu wengi ambao wanakuambia mambo ni mazuri inawezekana ni mtu kaanza kanyumba kake pale Tanzania na kwasababu wewe wa nje huna nyumba wanafikiria unabeba mabox siku nzima! na unacheza. 90% ya Watanzania niliokutana nao wanadanganya au kukuza mambo pasipo sababu ya uhakika!. Vijana wengi wanakutana kunywa bia na vibatari kwa wakati mwingine na kugigamba kwa idadi ya pesa walizonazo bank nyingi za kijanja janja na kujisifia idadi ya wanawake walionao!!. Kama una wazazi walio na umri wa juu kuwa makini kwani hata pale muhimbili ni pa kubabaisha tu na watu wenye uwezo wanaenda India kutibiwa vitu vidogo kama kisukari. Kwa ujumla Tanzania ni nchi ambayo haiko serious na viongozi wengi ni wabinafsi wa hali ya juu na huwezi kuishi bila kudanganya!. Mungu ibariki Tanzania