denooJ
JF-Expert Member
- Mar 31, 2020
- 18,511
- 68,141
Hiyo quote hapo juu ya Kinana aliitoa kuonesha vile wanavyofanya wakati wa uchaguzi, wizi.'…Uchaguzi unaanza wakati wa kuhesabu kura na kukamilika wakati wa kutangaza matokeo…'-Colonel Abdulrahman Omar Kinana
Sasa tuambie Lowassa alishinda wakati wa kampeni, au wa kupiga kura au wakati wa kuhesabu?
Huo wizi hufanyika wakati wa kuhesabu kura ndio maana mara nyingi masanduku ya kura huibiwa kwenye magari na kwenda kufichwa maporoni kwa kutumia green guard, naye ndie akasema hapa ndipo uchaguzi huanza akijua fika hawana uungwaji mkono wa watanzania.
Na kwenye kutangaza mshindi akimaanisha kwasababu anayetakiwa kutangaza mshindi ni tume, na tume ndio wameiweka mfukoni, basi wanakuwa na uhakika wa kutangazwa washindi hata kama hawakushinda kihalali.