Nashindwa kuchukuwa maamuzi sahihi ushauri wenu wadau

scientificall

JF-Expert Member
Jun 4, 2015
454
314
Hii ndo full story ya kinachonitatiza. Nilivyomaliza chuo kikuu nlikuwa na nia ya kutafuta mchumba na kuoa maana umri unazidi kusogea kwani mpaka sasa nina miaka 30.

Katika mazungumzo ya utani nilimdokeza dada angu kuwa mimi nataka kuoa hata kama ntakuwa sijapata ajira lakini ntajiajili mwenyewe na nahitaji kuwa na familia.

Dada alichukulia serious akasema ngoja nije nkuoneshe kabinti kana tabia nzuri na hakana skendo hio ilikuwa mwaka jana binti huyo akiwa form 1v.

Basi siku akanipgia simu dada angu huko kijijini kuwa yule binti keshamuomba namba ake ya simu.

Baada ya kuntumia namba mimi sikuanza kutaka kujua kama ni mzuri au vipi nkatupia kamaba kwa kumwambia nlipata kumuona sehemu nlivyokuwa huko kijijini kwetu.

Binti hakuwa na neno kwani alikuwa mdogo sana miaka 18 hivyo nlitumia mbinu kwa kuongea nae mara kwa mara mpaka akakubali kuwa katika mahusiano nami kwa lengo la kumuoa baadae.

Basi nkapanga safari kwenda kumuona kijijini. Tulikutania kwa dada angu tukazungumza mengi na mipango kabambe.
Ni mzuri wa wastani ila anatabia njema.
Hakutaka nimfanye chochote kwani alisema hataki sex mpaka ntakapo muoa.
Nami nkamuakikishia hilo.

Mpaka natoka kijijini sikuweza kumgegeda japo nlitamani lakini mazingira na makubaliano yaligongesha mwamba juhudi zangu.

Baada ya kurudi mjini basi nkawa nimepata ajira namshukuru Allah kipato nachokipata kwa mwezi mimi na familia tunaweza ishi na kufanya maendeleo mengine.

Huyo binti nmekuwa nawasiliana nae kama mke wa baadae na nimeshampima kiadabu na heshima kweli anayo japo sijui kama atabailika. Na ameshawambia baadhi ya ndugu zake kuwa mimi ndo mchumba wake hvyo hvi karibuni ntamuoa.

Ila kadri siku zinavyozidi kwenda nafsi angu inanambia bado hujapata ambacho nafsi yako inapenda. Kwani sema kweli mimi rangi ya mtume ndo kigezo cha kwanza kwa mke wangu ila yule mtoto ni maji ya kunde sio mweupe japo nmekufa na kuoza nae ameshasalimu amri.

Mawazo ya kuoa kwangu yameshatawala ubongo kila nkiona mtoto mweupe hapa mjini natamani kuoa.

Wiki jana kaja binti mmoja mzuri hapa kazini kumchukuwa mdogo wake anaumwa asee binti nlimpenda sana kwanza anavyoongea mpaka nlimtamani nafsi ikasema haya sasaaaaa

Sema kweli nlimchelewesha kumuudumia mpaka nikaomba na namba ya simu kwa kigezo cha kuwa namjulia hali mgojwa.
Binti mweupe mansharaha mzuri.

Nlijipanga ili nianze kutupia sumu na muelekeo unaonekana atakubali sababu ameshaanza hata kuntumia picha zake na tumepanga leo tuweke bayana mezani nimwambie la moyoni juu yake sababu uzuri wake umenipagawisha japo sijajua tabia yake ipoje japo anaonekana ana tabia njema.

Sasa je nimusaliti mpenzi wangu wa zamani ambae tayari nshamuaidi kumuoa? Na je huyu binti akinkubalia ntaweza kuvumilia nsioe na mpunga nshauandaa?

Sitaki nchukue maamuzi bila kushauriwa nawasilisha kwenu wadau

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Acha tamaaa, kaoe uliyemuahidi! Yaaani huwa hatuoi uzuri wa mtu maana uzuri huwa unaisha! Huyu mpya uliempata nna wasiwasi ni. Kama beki hazikabi asijekusumbua baadae. Bora awe mmbaya umgonge peke yako kuliko awe mzuri mgonge mtaaa mzima. Binti uliempata ukiwa huna pesa mara nyingi ni wife material.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mbona maamuzi ulishachukua hata kabla ya kupata ushauri?

Laana zingine tunajitakia tu, huyo rangi ya mtume mzuri wewe tu ndio umemuona na hana mtu mwingine? Mwenzio kakaa anajua anamchumba kumbe unapanga mengine.

Hata walio kwenye ndoa sio kwamba hawaoni wengine wazuri, wanajifunza kukinai tu kwamba tumeshakubaliana na mwenza wangu tuishi kama mme na mke. Sio kwamba wana wenza wazuri kuliko wote duniani. Na uzuri sio sifa pekee ya kuolewa.
 
Wavulana wavulana wavulana,ntakuwa nanyi hadi lini?Wallahi tukiondoka sisi wazee mtaolewa nyie vijana.Ndio maana ushoga umeongezeka!Kuoa hakukuzuii kupiga miti nje hao wanawake weupe!wapo tu wanapigwa miti na waume za watu.Oa mwanamke mzuri wa wastani mwenye nidhamu na upendo pamoja na hekima na kujali.Unaruhusiwa kuongeza wa pili watatu hadi wa4 mkuu.pia huyo mweupe angalia weupe upo madukani ndugu yangu utaenda kukuta tako kama black panther!
 
Sahihi kaanzia mapenzi ukubwani
Angekua tayari ameshagonyagonya sidhani kama hio rangi ingemsumbua ki hivyo
Jamaa anatakiwa amalizie stage ya kwanza akishaimaliza ndio aanze mambo ya ndoa. Yeye anataka kuoa kwa pressure kua umri wake umeshaenda wkt kina lemutuz mpaka leo bado hawajaumaliza ujana.

Maendeleo hayana chama
 
Mkuu scientificall nikupe siri moja, hakuna msichana mzuri utakaeoa kama yule aliependekezwa na ndugu niamini mimi, Wanawake kwa wanawake wanajuana sana kaka na sister wako naamini hatokuchagulia mali mbovu. Achana na rangi hizi zingine nizakutengeneza mkuu, rudi kijijini kaoe mtoto mbichi, maji ya Kunde yakipata viungwa na spices yanakuwa na rangi ya mtume pia, amin amin nakwambia.
 
Back
Top Bottom