MINOCYCLINE
JF-Expert Member
- Apr 2, 2015
- 8,011
- 16,748
Tukatae tukubali kuna Sekta zingine katika Kipindi kirefu tu cha Maombolezo huwa zinaathirika mno (hasa Kiuchumi) iwe directly or indirectly pia.
Si tu katika Nyanja hiyo ya Kiuchumi pekee bali hata katika Nyanja ya Kijamii na ya Kihuduma pia huathirika kwa namna moja au nyingine katika Kipindi kirefu cha Maombolezo ambacho huwa ni Siku 21 Kikatiba hata kama Marehemu atazikwa Siku ya Nane (8) tu.
Kwa mfano moja ya Sekta ambayo najua ndiyo Huathirika zaidi ( japo hawataki Kukiri hili ama kwa Kuiogopa Mamlaka au kuendelea Kujipendekeza Kwao) ni ya Habari na Utangazaji.
Mapato ya Kiuchumi ya Sekta hii yanatokana na kurusha Hewani kwa Matangazo ya Biashara ambayo ni ya Kimkataba zaidi hivyo Taifa kuwa katika Kipindi kirefu cha Maombolezo ya Kiongozi wa Kitaifa na Media nyingi Kulazimishwa kuwa na Maudhui ya aina Moja ya Kuomboleza kwa Siku 21 huku Vipindi vingine kusimama ni kuwatesa ( kuvitesa ) tu Kiuchumi huku wakiwa pia wanatakiwa kulipa Kodi Serikalini (TRA) kwa wakati.
Si hivyo tu lakini hata Walaji wa Vipindi mbalimbali vya Redio na Runinga nao pia huathirika katika Kipindi kirefu cha Maombolezo cha Siku 21 za Kikatiba. Sikio la Mwanadamu linahitaji kusikia Mambo ( Masuala ) mbalimbali lakini Kulilazimisha ndani ya Siku 21 zote liwe linasikiliza tu Ngonjera, Mapambio, Hotuba na Simulizi hizo hizo tu ni Kulitesa na pia Kuuonea Ubongo wa Walaji hasa Kiafya. Wataalam wa Saikolojia ya Mawasiliano hapa najua mnanielewa vyema tu.
Ushauri wangu tu All - Rounder na silazimishi iwe kama nitakavyo ni kwamba ili Kutengeneza mlinganyo wa Haki kwa Mwanadamu basi Ukomo wa Maombolezo kwa Kiongozi wa Kitaifa uwe tu pale (ile Siku) anayozikwa na Kesho yake Ratiba zingine zenye Faida kubwa wale waliobaki duniani ziendelee.
Ingekuwa tunaomboleza Siku 21 na ya 22 anafufuka na kuendelea kuwa nasi ningeona ina tija na mantiki ila tunaomboleza Siku nyingi hizo 21 halafu Mpendwa wetu wala harudi na ndiyo Kwanza anaanza tu Kujishindilia vizuri huko Udongoni tayari kwa Kuoza na kuwa Mbolea ya Ardhi na Mimea iliyopo.
Naipenda sana Falsafa ya Wayahudi ambapo hata afe (afariki) nani wao Kwanza hawalii na hawachelewi Kuzika na Kuomboleza Kwao kunachukua kati ya Siku 1 hadi 3 tu kisha wanafunga Mjadala wa Mazishi na kuendelea na Mambo mengine ya Kujenga nchi yao.
Na ikumbuke hata Kiimani hili ndilo Taifa la Mungu lakini hawana Shobo katika Misiba kama Mataifa mengine duniani. Waisraeli wana Msemo wao Ukifa ndiyo imetoka hiyo hivyo kuna wengine watanyanyuka na Maisha lazima yaendelee kwa Ujenzi na Ustawi wa Kimaendeleo wa Taifa lao Teule la Israeli (Israel)
Tujifunzeni pia kwenda na kasi ya dunia.
Si tu katika Nyanja hiyo ya Kiuchumi pekee bali hata katika Nyanja ya Kijamii na ya Kihuduma pia huathirika kwa namna moja au nyingine katika Kipindi kirefu cha Maombolezo ambacho huwa ni Siku 21 Kikatiba hata kama Marehemu atazikwa Siku ya Nane (8) tu.
Kwa mfano moja ya Sekta ambayo najua ndiyo Huathirika zaidi ( japo hawataki Kukiri hili ama kwa Kuiogopa Mamlaka au kuendelea Kujipendekeza Kwao) ni ya Habari na Utangazaji.
Mapato ya Kiuchumi ya Sekta hii yanatokana na kurusha Hewani kwa Matangazo ya Biashara ambayo ni ya Kimkataba zaidi hivyo Taifa kuwa katika Kipindi kirefu cha Maombolezo ya Kiongozi wa Kitaifa na Media nyingi Kulazimishwa kuwa na Maudhui ya aina Moja ya Kuomboleza kwa Siku 21 huku Vipindi vingine kusimama ni kuwatesa ( kuvitesa ) tu Kiuchumi huku wakiwa pia wanatakiwa kulipa Kodi Serikalini (TRA) kwa wakati.
Si hivyo tu lakini hata Walaji wa Vipindi mbalimbali vya Redio na Runinga nao pia huathirika katika Kipindi kirefu cha Maombolezo cha Siku 21 za Kikatiba. Sikio la Mwanadamu linahitaji kusikia Mambo ( Masuala ) mbalimbali lakini Kulilazimisha ndani ya Siku 21 zote liwe linasikiliza tu Ngonjera, Mapambio, Hotuba na Simulizi hizo hizo tu ni Kulitesa na pia Kuuonea Ubongo wa Walaji hasa Kiafya. Wataalam wa Saikolojia ya Mawasiliano hapa najua mnanielewa vyema tu.
Ushauri wangu tu All - Rounder na silazimishi iwe kama nitakavyo ni kwamba ili Kutengeneza mlinganyo wa Haki kwa Mwanadamu basi Ukomo wa Maombolezo kwa Kiongozi wa Kitaifa uwe tu pale (ile Siku) anayozikwa na Kesho yake Ratiba zingine zenye Faida kubwa wale waliobaki duniani ziendelee.
Ingekuwa tunaomboleza Siku 21 na ya 22 anafufuka na kuendelea kuwa nasi ningeona ina tija na mantiki ila tunaomboleza Siku nyingi hizo 21 halafu Mpendwa wetu wala harudi na ndiyo Kwanza anaanza tu Kujishindilia vizuri huko Udongoni tayari kwa Kuoza na kuwa Mbolea ya Ardhi na Mimea iliyopo.
Naipenda sana Falsafa ya Wayahudi ambapo hata afe (afariki) nani wao Kwanza hawalii na hawachelewi Kuzika na Kuomboleza Kwao kunachukua kati ya Siku 1 hadi 3 tu kisha wanafunga Mjadala wa Mazishi na kuendelea na Mambo mengine ya Kujenga nchi yao.
Na ikumbuke hata Kiimani hili ndilo Taifa la Mungu lakini hawana Shobo katika Misiba kama Mataifa mengine duniani. Waisraeli wana Msemo wao Ukifa ndiyo imetoka hiyo hivyo kuna wengine watanyanyuka na Maisha lazima yaendelee kwa Ujenzi na Ustawi wa Kimaendeleo wa Taifa lao Teule la Israeli (Israel)
Tujifunzeni pia kwenda na kasi ya dunia.