Nashauri Serikali iajiri Walimu wenye ufaulu wa daraja la kwanza au la pili kwenye vyeti vya elimu ya sekondari(Kidato cha nne na sita)

Hashimu lwenje

JF-Expert Member
Oct 2, 2017
415
359
Naishauri Serikali yangu iajiri Walimu wenye division two na One kwenye vyeti vyao vya kidato cha nne (olevel) na kidato cha sita (Alevel) kwenye shule zetu za Serikali, kwa sababu Walimu hawa ndio wenye mbinu za kujisomea na kufaulu mtihani. Ikiwaajiri hao watawapatia Wanafunzi wetu mbinu za kujisomea na kufaulu mitihani.

Naishauri pia Serikali yangu ijaribu kuwachukua Wahitimu wa vyuo vikuu walio somea fani mbalimbali walio faulu vizuri kidato cha nne na sita (division 2 na division 1) wakafundishe shule za Serikali kwa sababu wanazo hizo mbinu za kujisomea na kufaulu mtihani. Wawalipe mshahara ule ule wa kawaida.

Ili Serikali iweze kushindana na shule za binafsi (private) iajiri Walimu wenye uwezo (competent teachers), ambao kiukweli kuwapata ni ngumu sana katika kada ya ualimu, wanafunzi wengi wanao somea ualimu ni wale wenye ufaulu mdogo (division three).

Mimi ningelikuwa Mwalimu wa Serikali Mwanafunzi wangu asingepata F, kwenye somo langu, kwa sababu Serikali huwa inachukua wanafunzi walio faulu sana mtihani wa darasa la saba, kinacho tokea ni kwamba walimu wao ndio wanao waharibu mpaka wanafeli kwasababu walimu wengi kule hawana material kichwani.

Nitoe tu ushuhuda huu kipindi tunafundisha shule moja ya binafsi (private), tulikua tukimpata mwanafunzi anayetoka shule ya serikali kuja shule yetu, tunahesabu hiyo ni A, kwasababu mwanafunzi wa serikali huwa analewa haraka mno akipata mwalimu mwenye uwezo.

Asilimia 90 ya shule za binafsi (private) zinachukua wanafunzi wasio elewa haraka (slow learners) lakini kwasababu wana walimu wenye uwezo (competent teachers), wana wabadili wanafunzi hao wanapata one, na two. Walimu wengi wa private ni wale wenye one na two, katika mitihani yao ya olevel na advance, ni walimu wenye historia fulani ya kujituma kimasomo wakiwa shuleni wanasoma, mwanafunzi mwingine historia tu ya mwalim inatosha kumfaurisha.

Mimi nae ongea nimewahi kufundisha private, na hicho ndicho nilicho kiona. Serikali inatumia walimu walio feli mno, mwalimu aliye feli, huyo maana yake hakuwa na bidii wakati anasoma, kwa hiyo hawezi kuwavisha roho ya bidii wanafunzi wake.

Mwalimu aliye pata division one na two anazo mbinu za kufauru mtihani, mbinu za kufauru mtihani hatusomei chuoni, mbinu za kufauru mtihani anazo yule mwalimu aliye fauru mtihani huo. Tutumie walimu wenye ushuhuda.

Mwalimu aliye pata S au E ya physics au math au chemistry, au history advance huo hana mbinu za kufaulu mtihani, hivyo hawezi mshuhudia mwanafunzi akafaulu mtihani.

Wanafunzi wengine wanapo fundishwa na mwalimu aliye perform vizuri nao wanapata hamasa wanasoma kwa bidii ili wanafaulu.

Ni hayo tu.
Ahsanteni sana
Mungu ibariki Tanzania.
 
TOHATO

Mwandiko ni media tu ya kufikisha Ujumbe. Toa maoni au mtazamo wako juu ya hoja aliyoitoa sio mwandiko. Nchi za ulimwengu wa kwanza waliofaulu vizuri go to teaching and health sciences and ndio wanaongoza kwa pay. Hapa koromije nia opposite.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wasiwasi wangu huyu jamaa hajui alichoandika hapa, tafiti yake ya kimajinuni ame conclude kwa poor facts labda division one na two ya sekondari inaweza faulisha watoto, ngoja niishie hapo. Ila kwa thinking hii we need one more century nchini kwetu kupata wasomi, maana jamaa analicheti lake la form four linataka ajila na cheti cha o level
 
We unafikir wanaweza kutosheleza hao waliopata I Na II Kwa shule zote zilizopo Tz .. Na ili kuwapata hao watakaoenda kusomea ualimu wenye I na II ni lazima kwwnza serikali iboreshe maslahi ya Walimu sabab ni taaluma ambayo kiUhalisia imezaraulika kupita maelezo wachache sana ambao watawapta na hawatotosheleza hata robo ya uhitaji Wa walimu... Na vipi kwa hao walimu Wa sayans hakuna mwanafnz Wa sayans aliepta one au two atakuelewa ukimwambia akasomee ualimu.. Elimu ya kbongo ina changamoto Nyingi mnoo haswaa kwa wale ambao wamepitia shule za govrnmt...
SERIKALI LAZIMA ELIMU IWE NDO KIPAUMBELE CHAKE CHA KWANZA CHA PILI NA CHA TATU..


Sent using Jamii Forums mobile app
 
I think swala la kufeli sio la walimu peke yake,

mie naona mazingira yanachangia,

boresha mazingira ya shule za serikali utaona matokeo chanya,

boresha maabara,

ongeza vitabu

,punguza kazi za shule kama kilimo

wanafunzi wa concentrate na masomo peke yake.

.utapata positive results

...mimi ni mmoja ya watu nisioamini uwezo wa kiakili ni unarithishwa,

mie naamini MAZINGIRA yakiboreshwa mtoto wa shule za kata ana uwezo sawa na wa Marian Boys...
 
Hashimu lwenje,

Ndugu, wewe unayesema ukipewa wanafunzi uwafundishe hawatopata "F" haujui kuandika kwa ufasaha, umerudia kuandika kimakosa neno "faulu" kwa kuliandika "fauru", ziada umerudia kuvunja neno moja na ukatoa mawili mara kadhaa " nae ongea" badala ya "ninayeongea" (wanapo fundishwa=wanapofundishwa), na umeunganisha maneno mawili kutengeneza moja "kwasababu" badala ya "kwa sababu"..
Hayo ni kwa uchache sana, hivyo basi wewe nawe yakustahiki kuwa katika hilo kundi la walimu wasio na weledi na kwa ukweli mweupe na mweusi wewe haustahili kuwa mwalimu kabisa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
We unafikir wanaweza kutosheleza hao waliopata I Na II Kwa shule zote zilizopo Tz .. Na ili kuwapata hao watakaoenda kusomea ualimu wenye I na II ni lazima kwwnza serikali iboreshe maslahi ya Walimu sabab ni taaluma ambayo kiUhalisia imezaraulika kupita maelezo wachache sana ambao watawapta na hawatotosheleza hata robo ya uhitaji Wa walimu... Na vipi kwa hao walimu Wa sayans hakuna mwanafnz Wa sayans aliepta one au two atakuelewa ukimwambia akasomee ualimu.. Elimu ya kbongo ina changamoto Nyingi mnoo haswaa kwa wale ambao wamepitia shule za govrnmt...
SERIKALI LAZIMA ELIMU IWE NDO KIPAUMBELE CHAKE CHA KWANZA CHA PILI NA CHA TATU..


Sent using Jamii Forums mobile app

I agree with you...

Walimu walipaswa huwa na payscale sawa na majudge!

yes walitakiwa walipwe Zaidi...

hii ingewa attract watu makini, wenye uwezo mkubwa kufundisha na wenye uwelewa kubwa,in terms of qualifications,...

sio kama sasa hivi,ualimu ni kwa wale failures ,,,ni kama label vile,ukichukua ualimu inaonyesha Marks zako huko nyuma zilikua kwa mbinde...

yaani katika jamii yetu uwalimu=failure in academic achievement.

we have to change this attitude,

ba tutafanya hivyo pale ambapo walimu watapewa mishahara inayostahili,na pale ambapo Fani ya uwalimu imefanikiwa kuchota walimu ambao wako competent,wana qualifications sawa na profession nyingine kama doctor,lawyer etc

Serikali ibadilishe vigezo vya kuombea uwalimu,waweka tighter system,waliofaulu tu ndio waruhusiwe kufundisha
 
serikali iboreshe maslahi ya Walimu sabab ni taaluma ambayo kiUhalisia imezaraulika
Hii kweli mkuu, waalimu wangekua na maslahi mazuri kama ya Daktari tu kwa mfano, nina imani watu wengi wangeseoma ualimu vilevile nawangekuwa wanajituma katika ufundishaji wao.

Asilimia kubwa ya watu wanaosomea ualimu utakuta wamekosa kuchaguliwa au wanaona uwezekano wa kupata course nyingine ni mdogo hii yote ni kwa sababu hakuna incentives za mtu kusoma ualimu.

Kwa mfano miaka ya 2009 hadi 2013 kama sikosei walipotoa mikopo asilimia nyingi kama sio 100% kwa waalimu, watu wengi walivutiwa kusoma course za ualimu, hiki kitu kifanyike kwenye maslahi waone kama hata watu wa taaluma zingine hawatahamia kwenye ualimu.
 
Geology
Mafuta na gesi.
Electrical engineering na watu wa mechanical engineering
Bila kusahau civil engineering.

In UDSM pale wanachukulia cream. Haswa mafuta na gesi ni div 1.
Very competitive sna.

Sasa mtu akiangalia amepata div 1. Halaf aende ualimu wkt kuna coz kama hizo ambazo ni hot cake mjini. Kwann asiende hizo?
Nitajie hizo kozi kubwa kubwa hata tano tu.
Hi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hashimu lwenje,

Hoja yako dhaifu sana!! Kuwa na division one na two ndiyo kunakufanya kuwa mwalimu mzuri?

Walimu wote waliokufundisha na kukufaulisha wewe walipata division one na two?

Ukipata divison one na two ndiyo unaweza kufundisha?

Udsm, Sua, Udom, Mzumbe n.k wote wanaosomea ualimu hawajapata division one na two?

Walimu wote wanaofundisha private schools wana divison one na two?

Umeangalia mazingira ya utoaji elimu kati ya private na public schools?

Hizo unazozoiita 'cream' za sayansi zote zilipata division one na two?

Wote wanaosomea kozi zingine ukitoa ualimu walipata division one na two?

Acha dharau na kidivision chako feki ambacho hakina tija yoyote kwa taifa!!!
 
10 Reactions
Reply
Back
Top Bottom