Mtu Asiyejulikana
JF-Expert Member
- Sep 11, 2017
- 1,694
- 3,982
Ule uzinduzi wa Marekani ulikuwa na faida sana kwa wale ambao tulipata nafasi ya kwenda kuhudhuria kule na kuhamasisha. Ingawa tulikaa siku chache sana lakini si haba. Wengi wameweza kufanya kitu nyumbani.
Wengine wamepaua,wamenunua tugari,viwanja n.k mimi nimeangalia wanaopinga hii ni wivu tu. Ni vile wao hawapo kwenye mfumo. Hii idea ilikuwa nzuri na yenye manufaa kwetu watanzania.
Uzinduzi Zanzibar pia ulikuwa mzuri. Ushauri wangu hii Film tuizindue nchi nzima na huko tuhakikishe hata siku za kuonesha zisipungue 10. Watu wajifunze Utalii. Mimi nimeona faida kubwa kwa kweli kwetu tunaopata nafasi ya kizunguka. Ipo kubwa tu.
Haiwezekani wote mkazunguka kuzindua. Wachache tunawakilisha Watanzania wenzetu. Tutafikisha ujumbe hadi vijijini ili watu pia wajifunze kujiajiri. Kama Rais aliamua naye kuwa Msanii ninyi wengine mnashindwaje? Ni kuonesha mfano wa kujiajiri.
Nashauri pia ikiwezekana. Hii Royal Tour ioneshwe hadi "Mashuleni" na wanafunzi wafanyie mtihani. Ni moja ya Filamu bora kuigizwa nchini. Nasi tuzunguke Tanzania kuipromote na pia nchi za nje.
Mimi sijali suala la muda. Ila nipo tayari sasa tukaizundue China, Egypt, South Africa, Kenya, Rwanda ( tena huku tukae hata week mbili kuna watoto wazuri sana) Nigeria, Congo, Djibout, Benin, Uk, Canada, n.k Itatusaidia sana Watanzania.
Wanaopinga nawaambia "UKIONA ZINDUNA NA AMBALI IKO NYUMA"
Wengine wamepaua,wamenunua tugari,viwanja n.k mimi nimeangalia wanaopinga hii ni wivu tu. Ni vile wao hawapo kwenye mfumo. Hii idea ilikuwa nzuri na yenye manufaa kwetu watanzania.
Uzinduzi Zanzibar pia ulikuwa mzuri. Ushauri wangu hii Film tuizindue nchi nzima na huko tuhakikishe hata siku za kuonesha zisipungue 10. Watu wajifunze Utalii. Mimi nimeona faida kubwa kwa kweli kwetu tunaopata nafasi ya kizunguka. Ipo kubwa tu.
Haiwezekani wote mkazunguka kuzindua. Wachache tunawakilisha Watanzania wenzetu. Tutafikisha ujumbe hadi vijijini ili watu pia wajifunze kujiajiri. Kama Rais aliamua naye kuwa Msanii ninyi wengine mnashindwaje? Ni kuonesha mfano wa kujiajiri.
Nashauri pia ikiwezekana. Hii Royal Tour ioneshwe hadi "Mashuleni" na wanafunzi wafanyie mtihani. Ni moja ya Filamu bora kuigizwa nchini. Nasi tuzunguke Tanzania kuipromote na pia nchi za nje.
Mimi sijali suala la muda. Ila nipo tayari sasa tukaizundue China, Egypt, South Africa, Kenya, Rwanda ( tena huku tukae hata week mbili kuna watoto wazuri sana) Nigeria, Congo, Djibout, Benin, Uk, Canada, n.k Itatusaidia sana Watanzania.
Wanaopinga nawaambia "UKIONA ZINDUNA NA AMBALI IKO NYUMA"