Nashauri kipindi cha mvua wanafunzi wawe wanavaa buti za plastiki

pisi jacky

Member
Oct 21, 2020
32
141
Ningependa kuiomba serikali yangu tukufu na njema, kwa miezi hii ya Januari hadi Aprili watoto wawe wanavaa buti za plastic shuleni.

Iweke tu sheria ya buti nyeusi, kwa sababu katika kipindi cha mvua watoto hukanyaga sana maji machafu.

Leo nimekutana na katoto ka darasa la kwanza kamevua viatu kameweka kwenye begi kanakanyaga maji machafu mno, ukikauliza kanasema naogopa viatu vipya vitaloa hakawazi kuugua kanawaza viatu vyake.

So ningeomba serikali ingeweka tu sheria kuanzia chekechea hadi secondary miezi hii wanafunzi wavae buti la plastic, na bei yake ni affordable kwasababu madogo ni elfu tano na yale makubwa ni 9000 lakini kwa wanafunzi wengi wataishia saizi ndogo.

Naomba kuwasilisha hoja
 
Kuna aliyekatazwa?

Kama buti zipo nyumbani anavaa viatu vyake "vipya", buti anaweka kwa begi, akifika eneo korofi anavua anavaa buti, akifika shule anavaa "vipya" sioni tabu hapo dada 'pisi Jack'
 
pisi jacky na wewe una mawazo ya ajabuajabu namna hii?

Sio kila sehemu mvua zinanyesha mpaka iwekwe sheria nchi nzima. Kama mwanao anapata tabu huko uliko bora umnunulie buti tu maana kama kuna matope kweli hawezi kuulizwa shuleni kwanini kavaa buti.
 
Kuna aliyekatazwa?

Kama buti zipo nyumbani.. anavaa viatu vyake "vipya", buti anaweka kwa begi, akifika eneo korofi anavua anavaa buti, akifika shule anavaa "vipya" sioni tabu hapo dada 'pisi Jack'
Kuna kuibiwa na kupoteza na mtoto wa darasa la kwanza kumpatia vitu vingi sidhani kama vitarudi salama.
 
pisi jacky na wewe una mawazo ya ajabuajabu namna hii?
Sio kila sehemu mvua zinanyesha mpaka iwekwe sheria nchi nzima. Kama mwanao anapata tabu huko uliko bora umnunulie buti tu maana kama kuna matope kweli hawezi kuulizwa shuleni kwanini kavaa buti.
Sio mwanangu plus nimeongea in general kwa sababu hii ni rain season afu uajabu wa wazo sijauona kama hujala mchana kaa kwa kutulia usije hapa na kelele hujaitwa.
 
Sio mwanangu plus nimeongea in general kwa sababu hii ni rain season afu uajabu wa wazo sijauona kama hujala mchana kaa kwa kutulia usije hapa na kelele hujaitwa
Mada yako inaonesha kabisa hujala mchana kweli.

Eti serikali iweke sheria ya mwezi mmoja wa kuvaa buti shuleni.😄
 
iv mpaka kumnunulia mwanao boot za kukanyagia tope ni mpaka serikali itoe tamko?

We mleta mada zinduka ulipo kabla ujaomba serikali ije ikutandikie kitanda.
 
Ninaunga mkono hoja.

Miundo mbinu nchi nzima ni mibaya sana. Sehemu za kupita kwa miguu na hata magari zote ni kwa hisani ya maji machafu.

Gumboots zingewanusuru madogo na magonjwa yanayo epukika.

Au nasema uongo ndugu zangu?
 
Ningependa kuiomba serikali yangu tukufu na njema, kwa miezi hii ya Januari hadi Aprili watoto wawe wanavaa buti za plastic shuleni.

Iweke tu sheria ya buti nyeusi, kwa sababu katika kipindi cha mvua watoto hukanyaga sana maji machafu.

Leo nimekutana na katoto ka darasa la kwanza kamevua viatu kameweka kwenye begi kanakanyaga maji machafu mno, ukikauliza kanasema naogopa viatu vipya vitaloa hakawazi kuugua kanawaza viatu vyake.

So ningeomba serikali ingeweka tu sheria kuanzia chekechea hadi secondary miezi hii wanafunzi wavae buti la plastic, na bei yake ni affordable kwasababu madogo ni elfu tano na yale makubwa ni 9000 lakini kwa wanafunzi wengi wataishia saizi ndogo.

Naomba kuwasilisha hoja
Watakuambia ni elimu bure
 
Ningependa kuiomba serikali yangu tukufu na njema, kwa miezi hii ya Januari hadi Aprili watoto wawe wanavaa buti za plastic shuleni.

Iweke tu sheria ya buti nyeusi, kwa sababu katika kipindi cha mvua watoto hukanyaga sana maji machafu.

Leo nimekutana na katoto ka darasa la kwanza kamevua viatu kameweka kwenye begi kanakanyaga maji machafu mno, ukikauliza kanasema naogopa viatu vipya vitaloa hakawazi kuugua kanawaza viatu vyake.

So ningeomba serikali ingeweka tu sheria kuanzia chekechea hadi secondary miezi hii wanafunzi wavae buti la plastic, na bei yake ni affordable kwasababu madogo ni elfu tano na yale makubwa ni 9000 lakini kwa wanafunzi wengi wataishia saizi ndogo.

Naomba kuwasilisha hoja
Kwani kuna aliyekatazwa?

Au unataka hili nalo litungiwe sheria?

Wazazi wangapi wanaweza kununua hizo gumboots?

Umeshawahi kufika kijijini au unaongelea watoto wa mijini pekee?

Na ni mtoto gani anayeugua kwa kukanyaga uchafu? Labda hawa mabroila wa kisasa hawa. Uchafu huo ndiyo unachochea mtoto awe na immunity imara. Hawa mnaowalea kwa kila kitu antibacterial wanakuwa na immunity dhaifu akipata homa tu chali watu wanaimba mapambio ya parapanda.

Watoto waachwe wafurahie utoto wao kulingana na mazingira waliyomo!
 
Back
Top Bottom