Nashauri Jen. Venance Mabeyo asome kitabu "Army of None" cha Paul Scharre ili atuondolee aibu ya kubebesha magunia makomandoo kwenye sherehe za uhuru

CreativityCode

Senior Member
Aug 8, 2020
158
653
Shalom from Jerusalem,

Imekuwa ni kawaida sasa kwenye kila sherehe za uhuru wa Tanganyika ama mapinduzi ya Zanzibar jeshi letu la ulinzi la wananchi wa Tanzania kutuonesha siraha na mbinu za kivita. Miongoni mwa mbinu hizo ni makomandoo wetu kubebeshwa mizigo na magunia mazito kuonesha maguvu na mabavu. Hii kwa wengi nadhani imepitwa na wakati kwa sababu vita ya sasa inahitaji teknolojia ya hali ya juu na wanajeshi wanaotumia akili zaidi kuliko mabavu.

Hatuhitaji tena mwanadamu mwenye mabavu kushinda vita bali matumizi ya technolojia ili kubaini mahali alipo adui, kumtageti na kumshambulia bila hata wewe mwenyewe kuwepo eneo la mashambulizi.

Kizazi hiki ni cha vita vya autonomous weapons hivyo sasa umefika wakati jeshi letu watuoneshe mbinu za aina hiyo na si kubeba magunia kama walivyozoea kufanya.

Namshauri Jen. Venance Mabeyo asome kitabu hiki "Army of None: Autonomous Weapons and the Future of War" cha Paul Scharre kitamsaidia kuja na mbinu mpya za kivita na kutuonesha ni namna gani wamejipanga kuzitumia.

Nawatakia siku njema.

1642074661266.png

 
Na wewe nenda kasome " the art of war" by Sun Tzu.

"Pretend to be weak when ur stronger and stronger when ur weak so that u will make ur enemies to focus on the tree instead of the whole forest." Sun Tzu

Mabeyo yupo Sahihi kuliko unavyo weza kufikiri..


Huyo Paul Scharre ni kabulyage
 
Mleta mada hajui vita
Kuna ebeo unahitaji physical presence sio teknolojia tu

Osama kuua kulitumika mbinu zote physical na technological

Kuteka hutumii teknolojia tu au kupambana na magaidi huhitaji teknolojia tu

Hata kupambana mijini na porini na kuteka mijasusi kunahitaji physical
 
Mleta mada hajui vita
Kuna ebeo unahitaji physical presence sio teknolojia tu

Osama kuua kulitumika mbinu zote physical na technological

Kuteka mini hutumii teknolojia tu au kupambana na magaidi huhitaji teknolojia tu

Hata kupambana mijini na porini na kuteka mijasusi kunahitaji physical
Mkuu hii ndiyo namna ya kuwapa watu shule hapa JF, hongera. Huyo amemezeshwa tu na wale watu wa twittter kuwa physical imepitwa na wakati.
 
Na wewe nenda kasome " the art of war" by Sun Tzu.

"Pretend to be weak when ur stronger and stronger when ur weak so that u will make ur enemies to focus on the tree instead of the whole forest." Sun Tzu

Mabeyo yupo Sahihi kuliko unavyo weza kufikiri..


Huyo Paul Scharre ni kabulyage kama wewe tu

 
Na wewe nenda kasome " the art of war" by Sun Tzu.

"Pretend to be weak when ur stronger and stronger when ur weak so that u will make ur enemies to focus on the tree instead of the whole forest." Sun Tzu

Mabeyo yupo Sahihi kuliko unavyo weza kufikiri..


Huyo Paul Scharre ni kabulyage
Ndugu siku hizi ukiwa huwezi kubuni na kuitumia teknolojia kwenye vita wewe ni dhaifu sana, hayo mabavu wala hayakusaidii kitu. UTAPIGWA MA MISULI YAKO. NA HAKIKA NAKWAMBIA NDANI YA MIAKA 20 TU IJAYO HUTOONA WANAJESHI WAKIENDA VITANI BALI WANAKAA OFISINI LAKINI WANAFANYA MAMBO.
 
Unatazama in a narrow way

Kitabu kimoja kama reference ndio unaconculde in that way!?

Vita imehama focus but the threat still persists so challenging in that way you do means you lack basic knowledge ya mambo ya kijeshi
Ndugu siku hizi ukiwa huwezi kubuni na kuitumia teknolojia kwenye vita wewe ni dhaifu sana, hayo mabavu wala hayakusaidii kitu. UTAPIGWA MA MISULI YAKO. NA HAKIKA NAKWAMBIA NDANI YA MIAKA 20 TU IJAYO HUTOONA WANAJESHI WAKIENDA VITANI BALI WANAKAA OFISINI LAKINI WANAFANYA MAMBO.
 
Pretend to be weak when it stronger and stronger when ur weak so that u will make it enemies to focus on the tree instead of the whole forest
Ndugu siku hizi ukiwa huwezi kubuni na kuitumia teknolojia kwenye vita wewe ni dhaifu sana, hayo mabavu wala hayakusaidii kitu. UTAPIGWA MA MISULI YAKO. NA HAKIKA NAKWAMBIA NDANI YA MIAKA 20 TU IJAYO HUTOONA WANAJESHI WAKIENDA VITANI BALI WANAKAA OFISINI LAKINI WANAFANYA MAMBO.
 
Back
Top Bottom