Nashauri Ikulu ikutane na Waandishi wa Habari mara kwa mara kwa ajili ya taarifa na ufafanuzi (Press Briefing Room)

Interest

JF-Expert Member
Apr 11, 2015
3,434
7,055
Nchi yetu inakua. Kwa maana, siasa na matukio makubwa ya nchi yanachukua nafasi kubwa kwenye maisha ya watanzania ya kila siku. Kwa sasa, hakuna mwananchi anayetaka kupitwa na tukio lolote la kisiasa na kijamii hasa matukio ya kisiasa ambayo yanalenga utekelezaji wa sera za serikali na mambo mengine ya nchi kwa ujumla.

Kwa kutambua umuhimu huo, naamini imefikia hatua sasa Ikulu ya Tanzania iongeze utaratibu wa kualika waandishi wa habari kwa ajili ya kutolea ufafanuzi juu ya masuala yanayoendelea nchini, hasa yanayogusa maamuzi ya kisera ndani na nje ya nchi.

Tunafahamu kuwa hivi karibuni nchi yetu imekuwa popular zaidi tangu Rais JPM aingie madarakani. Maamuzi yake magumu na mengine 'tata' yamefanikiwa kutengeneza vichwa vya habari katika mataifa makubwa duniani pengine kuliko kipindi chochote. Huu ni mtaji mkubwa sana wa taifa kutangaza sera, propaganda na mipango yake.

Ikulu itumie vyema fursa hii kwa kuweka utaratibu wa kupokea waandishi wa vyombo vyote vya habari vya ndani na vile vyenye uwakilishi wa kimataifa, ili panapotokea jambo, basi Kurugenzi ya Mawasiliano inaita waandishi na kuwabrief kisha kuruhusu maswali kadhaa ambayo aidha yatajibiwa moja kwa moja na Rais au wasaidizi wake pale Ikulu.

Kwa sasa, upo utaratibu wa press release za Gerson Msigwa ambazo ni one way. Hazina changamoto ya maswali na majibu. Ni aidha makanusho tu au utetezi. Hii haiisaidii sana serikali mara zote kwani kuna mambo aidha huchelewa kufafanuliwa au ufafanuzi hauridhishi.

Naona utaratibu huu unatumika zaidi nchini Marekani. Ni wazi hapa pia unawezekana.

Obamaaaa.jpg

Rais mstaafu, Barack Obama akizungumza na media akiwa kwenye podium katika chumba cha habari kilichopo Ikulu ya Marekani

Ninaamini, kwa kuwa na news room inayofanya kazi hivi, kutasaidia serikali kuzika rasmi zile fununu kwamba haiko rafiki na vyombo vya habari pamoja na kusambaratisha taarifa za uongo dhidi ya Serikali na hata kufafanua baadhi ya maelezo ya Rais ambayo mara nyingi hunukuliwa out of context.

Najua kuna wadau na wataalamu wataliweka vyema zaidi pendekezo hili.

Nawasilisha!
 
Msigwa na yule msemaji mkuu wa serikali Dr. Abbas, hawana uwezo kuzungumza na kujibu maswali ya vyombo vya habari vya kigeni. Niliona video clip moja Dr. Abbas akihojiwa na Al Jazeera alipwaya sana pamoja ya kuwa na PhD.

Wasemaji wote hao wawili hawana imani na sera za awamu wanayoitumikia. Maana kutetea kitu usicho amini ni kazi kweli kweli.

Bora sisi wanaJF tunasema tunachoamini kuwa awamu hii mambo hayaendi inavyotakiwa katika maeneo mengi muhimu mfano : kikatiba, kidemokrasia, uchumi-kilimo, uchumi - viwanda, economic diplomacy bila kusahau utawala usio - bora.
 
Sahau kabisa hizo press conference za akina Barack Obama au za Mwalimu Nyerere enzi zake kwa watawala hawa wa awamu ya tano

Kwa kuwa wanajua kuwa watalazimika kupiga "fix" Press conference yote, jambo ambalo ni lazima tu wataaibika, kwa kuwa wanajua pia kuwa njia ya mwongo ni fupi!
 
Ukiwa mpika dayt huwezi kukubali press zenye wauliza maswali wasio na hofu. Kwanza ufahamu rais wetu hana uwezo wa kujibu maswali ya waandishi hasa wa nje wasio na hofu naye. Hao wasaidizi wake hawana uwezo wa kujibu bila kuzua utata kwani taarifa nyingi ni za kupika na kuna shida ya demokrasia.
 
Msigwa na yule msemaji mkuu wa serikali Dr. Abbas, hawana uwezo kuzungumza na kujibu maswali ya vyombo vya habari vya kigeni. Niliona video clip moja Dr. Abbas akihojiwa na Al Jazeera alipwaya sana pamoja ya kuwa na PhD.

Wasemaji wote hao wawili hawana imani na sera za awamu wanayoitumikia. Maana kutetea kitu usicho amini ni kazi kweli kweli.

Bora sisi wanaJF tunasema tunachoamini kuwa awamu hii mambo hayaendi inavyotakiwa katika maeneo mengi muhimu mfano : kikatiba, kidemokrasia, uchumi-kilimo, uchumi - viwanda, economic diplomacy bila kusahau utawala usio - bora.
Wasiomudu ni kwa sababu hawajazoea. Naamini wanaweza kujifunza na kumudu through the process.

Kuhusu mambo kwenda ndivyo sivyo, hii sasa ndio tiba yake. Rais na hata subordinates wake sasa wataweza kufanya kazi kwa weledi na umakini kwa kuwa watajua kuna maswali watahojiwa.
 
Sahau kabisa hizo press conference za akina Barack Obama au za Mwalimu Nyerere enzi zake kwa watawala hawa wa awamu ya tano

Kwa kuwa wanajua kuwa watalazimika kupiga "fix" Press conference yote, jambo ambalo ni lazima tu wataaibika, kwa kuwa wanajua pia kuwa njia ya mwongo ni fupi!

Kupiga fix kwenye siasa ni jambo la kawaida. Hata diplomasia ni unafiki fulani hivi. Siamini kama kutapigwa fix kwenye kila jambo. Mengine ni uzushi na uvumi wa wanasiasa tu, hii ndio itakuwa dawa ya kupangua hoja zote.
 
Ukiwa mpika dayt huwezi kukubali press zenye wauliza maswali wasio na hofu. Kwanza ufahamu rais wetu hana uwezo wa kujibu maswali ya waandishi hasa wa nje wasio na hofu naye. Hao wasaidizi wake hawana uwezo wa kujibu bila kuzua utata kwani taarifa nyingi ni za kupika na kuna shida ya demokrasia.
Sasa mfumo huu utabadili hiyo status quo. Rais hawezi kukubali kulishwa matango pori halafu aaibike kwenye media. Ni wazi kwa sasa huenda akawa anadanganywa kwa sababu hakuna sehemu ambayo Rais atajipima. Maswali konki ya waandishi yatamsaidia kupitia upya info anazolishwa na wasaidizi wake makanjanja!
 
Sasa mfumo huu utabadili hiyo status quo. Rais hawezi kukubali kulishwa matango pori halafu aaibike kwenye media. Ni wazi kwa sasa huenda akawa anadanganywa kwa sababu hakuna sehemu ambayo Rais atajipima. Maswali konki ya waandishi yatamsaidia kupitia upya info anazolishwa na wasaidizi wake makanjanja!

Hata asipolishwa hayo Matango pori hana uwezo wa kujieleza kwani hawezi kutoa ufafanuzi zaidi ya amri. Atakapokutana na waandishi wasiohofia cheo chake atajikuta kwenye wakati mgumu. Kumbuka siku ile kaitisha waandishi wa habari aliishia kujibu kwa kiwango cha chini na kuonyesha zaidi kuwa yeye ni rais.
 
Hata asipolishwa hayo Matango pori hana uwezo wa kujieleza kwani hawezi kutoa ufafanuzi zaidi ya amri. Atakapokutana na waandishi wasiohofia cheo chake atajikuta kwenye wakati mgumu. Kumbuka siku ile kaitisha waandishi wa habari aliishia kujibu kwa kiwango cha chini na kuonyesha zaidi kuwa yeye ni rais.
With time atamudu tu. Bora tuanze kuliko kubaki tulipo.
 
Nchi yetu inakua. Kwa maana, siasa na matukio makubwa ya nchi yanachukua nafasi kubwa kwenye maisha ya watanzania ya kila siku. Kwa sasa, hakuna mwananchi anayetaka kupitwa na tukio lolote la kisiasa na kijamii hasa matukio ya kisiasa ambayo yanalenga utekelezaji wa sera za serikali na mambo mengine ya nchi kwa ujumla.

Kwa kutambua umuhimu huo, naamini imefikia hatua sasa Ikulu ya Tanzania iongeze utaratibu wa kualika waandishi wa habari kwa ajili ya kutolea ufafanuzi juu ya masuala yanayoendelea nchini, hasa yanayogusa maamuzi ya kisera ndani na nje ya nchi.

Tunafahamu kuwa hivi karibuni nchi yetu imekuwa popular zaidi tangu Rais JPM aingie madarakani. Maamuzi yake magumu na mengine 'tata' yamefanikiwa kutengeneza vichwa vya habari katika mataifa makubwa duniani pengine kuliko kipindi chochote. Huu ni mtaji mkubwa sana wa taifa kutangaza sera, propaganda na mipango yake.

Ikulu itumie vyema fursa hii kwa kuweka utaratibu wa kupokea waandishi wa vyombo vyote vya habari vya ndani na vile vyenye uwakilishi wa kimataifa, ili panapotokea jambo, basi Kurugenzi ya Mawasiliano inaita waandishi na kuwabrief kisha kuruhusu maswali kadhaa ambayo aidha yatajibiwa moja kwa moja na Rais au wasaidizi wake pale Ikulu.

Kwa sasa, upo utaratibu wa press release za Gerson Msigwa ambazo ni one way. Hazina changamoto ya maswali na majibu. Ni aidha makanusho tu au utetezi. Hii haiisaidii sana serikali mara zote kwani kuna mambo aidha huchelewa kufafanuliwa au ufafanuzi hauridhishi.

Naona utaratibu huu unatumika zaidi nchini Marekani. Ni wazi hapa pia unawezekana.

View attachment 991566
Rais mstaafu, Barack Obama akizungumza na media akiwa kwenye podium katika chumba cha habari kilichopo Ikulu ya Marekani

Ninaamini, kwa kuwa na news room inayofanya kazi hivi, kutasaidia serikali kuzika rasmi zile fununu kwamba haiko rafiki na vyombo vya habari pamoja na kusambaratisha taarifa za uongo dhidi ya Serikali na hata kufafanua baadhi ya maelezo ya Rais ambayo mara nyingi hunukuliwa out of context.

Najua kuna wadau na wataalamu wataliweka vyema zaidi pendekezo hili.

Nawasilisha!
Sasa yule Kilaza wa sasa Magogoni ana uwezo huo kujibu maswali ya waandishi wa BBC, Al Jazeera ama CNN?
 
Sasa yule Kilaza wa sasa Magogoni ana uwezo huo kujibu maswali ya waandishi wa BBC, Al Jazeera ama CNN?
Swali la Pascal Mayalla lilimtaabisha hadi akaanza vijembe. Mayalla kwetu ni Njaa.

Na alipoenda kwa Museveni ilibidi Mzee Museveni ageuke mtafasiri wake ikawa kioja
 
Huu mjadala ni mzuri.
Ninachojua ni hiki, learning is literally process of permanent change of behaviour. Huyu rais akiipenda hii aichukue. Akijibu sawa au sio sasa hakumuondolei ukweli kuwa yeye ni rais. Ila itamjenga sans kumuondolea mauongo wanayomlisha k.m maekekezo kutoka juu
 
Nashauri zisiwepo press nyingi sababu matamko mengine yanatolewa tuu out of sight. Sasa vyombo vikinakili na kuchapisha italeta tafrani Kama suala la ushoga linavyotafsiriwa taharuki au mimba za mashuleni kupelekea media Kama The Economist kutuandika vibaya.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huu mjadala ni mzuri.
Ninachojua ni hiki, learning is literally process of permanent change of behaviour. Huyu rais akiipenda hii aichukue. Akijibu sawa au sio sasa hakumuondolei ukweli kuwa yeye ni rais. Ila itamjenga sans kumuondolea mauongo wanayomlisha k.m maekekezo kutoka juu
Asante mkuu.

Nyakati kama hizi hili suala lingetufaa sana.

Bado hatujachelewa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom