Nash MC hakika album yako ya Diwani Y Maalim umekata kiu ya wengi

aka2030

JF-Expert Member
Jan 5, 2013
2,630
3,577
1DB75E81-988A-496E-B16B-7E6E0F0CCAEE.jpeg


Hakika album yako imesheheni sana madini ambayo kwa kipindi hiki ni ngumu kuyapata kwa wanamuziki wengne

Nmpenda pia ubunifu wako wa njia ya usambazaji wa watu kulipia kwanza mwezi mmoja kabla kwani kwa njia hiyo hata sasa watu wakisambaziana nyimbo zao angalau jasho lako utakuwa umelifaidi

Nimependa pia bei ya album 7000 si kubwa ambayo kila mtu ambaye anapenda muziki anaimudu

Nimependa kusikia baadhi ya wanamuziki wakubwa kama jay dee na fatma kwenye album yako

Nmependa kusikia uchambuzi mzuri wa lugha na fasihi ya kweli kwenye nyimbo zako

Nimependa jinsi ulivyogusa nyanja mbalimbali ya jamii kama maradhi, elimu,uchumi,siasa, na sanaaa huku ukiwa na nyimbo yenye ujumbe mzito wa makamanda wetu walinda nchi <barua kutoka bangui>

Mwisho my best song ambayo hakika umenikumbusha mbali ni Salaam za Amani

Nyimbo ni nzuri ila zingne biti zipo oldschool sana pamoja na chorus mda mwngne hilo hebu lifanyie kazi
 
Hiphop anayo fanya Nash na lunduno tukimtoa unju ni ya kizamani sana ilishafanywa miaka ya 90 Arusha ndio maana wakifikaga sua wanachorwa tuu.Abadilike afanye swagah kidogo na content.
 
Mkuu jamaa nimemkubali sana
Nikiwa ubelgiji naenda kama beberu/

Nikija tanzania nakuja kama zeruzeru/

Sijui mmenielewa/

Au nirudie narudi kama nimelewa/

Nikija na mtaji naenda kama muwekezaji/

nakandamiza wanyonge naenda kama mnyonyaji/
 
Kila mtu anapenda fleva tofauti,mbona souljer boy amechokwa na swaga zake mpya na Kendrick Lamar anafanya hip hop kama zamani na ana tuzo nyingi,tatizo wabongo hampendi mziki wa kufikirisha ubongo mnapenda beat(mdundo) na swaga zisizo na maana.
Hiphop anayo fanya Nash na lunduno tukimtoa unju ni ya kizamani sana ilishafanywa miaka ya 90 Arusha ndio maana wakifikaga sua wanachorwa tuu.Abadilike afanye swagah kidogo na content.
 
Kila mtu anapenda fleva tofauti,mbona souljer boy amechokwa na swaga zake mpya na Kendrick Lamar anafanya hip hop kama zamani na ana tuzo nyingi,tatizo wabongo hampendi mziki wa kufikirisha ubongo mnapenda beat(mdundo) na swaga zisizo na maana.
Kendrick anafanya new school tofautisha na ujinga anaoufanya mansulii,Nashiri na songa wanajifanya wanajua Hiphop zaidi ya kina Hashim dogo.Hiphop yako ya kishamba sana kwa producer mzuri awezi wapa beat wachafue maana hawana flow nzuri kwenye beat wanafoka mono kwanzia intro hadi outro hakuna stereo.
Ukimnyanyang'anya kiswahili maalim utagundua haangii kwenye kundi la rapper wala mcee.
 
Mkuu Mansuli alishakwama tangu nimemsikia 2006 hivi na bado yuko kwenye mziki na hasikiki,yeye ni kama block 41 kina kalapina ambao hawasikiki,Mbona Nash anazungumzia mambo ya sasa ,ni media tu zinaangalia kick,ila Nash kazungumzia vitu vingi vya sasa,...sema tu akili za watu wengi sasa hivi bongo hawasikilizi vitu vya maana zaidi ya inama,nyege nyegezi
Kendrick anafanya new school tofautisha na ujinga anaoufanya mansulii,Nashiri na songa wanajifanya wanajua Hiphop zaidi ya kina Hashim dogo.Hiphop yako ya kishamba sana kwa producer mzuri awezi wapa beat wachafue maana hawana flow nzuri kwenye beat wanafoka mono kwanzia intro hadi outro hakuna stereo.
Ukimnyanyang'anya kiswahili maalim utagundua haangii kwenye kundi la rapper wala mcee.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom