Heavy User
JF-Expert Member
- Feb 2, 2020
- 954
- 1,732
Roho inaniuma sana ninapoona TZ ina wasomi wengi wenye maneno mengi wanaojua kila kitu lakini nchi yetu bado masikini inategemea kuombaomba. Rais kazungukwa na wasomi na washauri wazuri lakini shida zilizotakiwa kutatuliwa miaka mingi iliyopita bado zipo na hazionekani kuisha leo wala kesho.
Shida zote hizi ni kwasababu ya FIKRA ZA KIZEE zinaonekana ni ujanja ukizizungumza mbele za watu, fikra zenyewe ni uchama, usiasa na kusifusifu watu.
Vyama pinzani vinaonekana kuwa na uchungu wa hali mbaya ya nchi, lakini nao ni walewale tu, wakipewa nchi watatanguliza maslahi yao kuliko maendeleo ya nchi.
Vyama pinzani ni masikini, vikipewa nchi vitajineemesha kwanza. Vyama pinzani mkitaka tuwape nchi hakikisheni chama chenu kimojawapo kimekuwa tajiri. La sivyo msahau.
Na mnaopiga makelele mitaani na kwenye social media kwa mawazo mengi mazuri na kukosoa, na ninyi ni walewale, mkipewa hata kacheo kadogo tu mtatanguliza maslahi yenu binafsi.
ROHO INANIUMA SANA
Shida zote hizi ni kwasababu ya FIKRA ZA KIZEE zinaonekana ni ujanja ukizizungumza mbele za watu, fikra zenyewe ni uchama, usiasa na kusifusifu watu.
Vyama pinzani vinaonekana kuwa na uchungu wa hali mbaya ya nchi, lakini nao ni walewale tu, wakipewa nchi watatanguliza maslahi yao kuliko maendeleo ya nchi.
Vyama pinzani ni masikini, vikipewa nchi vitajineemesha kwanza. Vyama pinzani mkitaka tuwape nchi hakikisheni chama chenu kimojawapo kimekuwa tajiri. La sivyo msahau.
Na mnaopiga makelele mitaani na kwenye social media kwa mawazo mengi mazuri na kukosoa, na ninyi ni walewale, mkipewa hata kacheo kadogo tu mtatanguliza maslahi yenu binafsi.
ROHO INANIUMA SANA