Nasa artemis 1: Kesho kuanza safari ya kuelekea katika mwezi

mike2k

JF-Expert Member
May 12, 2016
1,458
3,126
ROCKET YA MWEZINI KURUSHWA SIKU YA KESHO 29 AUGUST

Shirika la uchunguzi na tafiti zinazohusu anga za juu kwa ujumla NASA kufanya majaribio ya rocket itakayoweza kutumika katika safari za kuwapeleka wanaanga na vifaa mwezini katika masiku yajayo kwenye mission mbalimbali za kwenda kwenye gimba hilo

Kufanywa majaribio ya rocket ya Space launch system (SLS) kutafungua panzia jipya la ARTEMIS mara baada ya panzia la APOLLO kufungwa katika miaka 1972 ambapo tuliweza kushuhudia mwanadamu wa kwanza kabisa kukanyaga katika uso wa mwezi na kuendelea kushuhudia mwanaanga kadhaa katika mission mbalimbali za apollo kufanikiwa kufika katika gimba hilo la karibu zaidi na Dunia yetu

Katika mission ya Artemis itatuwezesha kushuhudia wanaanga wengine wapya wakiweza kukanyaga uso wa mwezi na kufanya mission mbalimbali mwezini huko huku kubwa zaidi likiwa ni lile la kutengeneza kambi yenye makazi mbalimbali ambayo itatumiwa na wanaanga na Raia wa kawaida watakao tembelea mwezini

Mataifa zaidi ya 20 yameungana na Nasa katika kuhakikisha jambo hili linafanikiwa mataifa ya kila pande za dunia yetu kwakuwa kulikuwa na makubaliano hapo mwanzo kwamba kwa masuala ya tafiti za anga za mbali basi mashirikiano yanatakiwa yadumishwe kwakuwa faida itakuwa ni kwa dunia nzima si kwa mtu mmoja mmoja au taifa moja moja

🔳 Majaribio yataanza kesho muda wa tisa na dakika thelathini mchana kwa masaa ya ya afrika mshariki

🔳Rocket itarushwa kutokea katika kambi ya Kennedy space center katika Launch pad complex 39B , kumbuka chamber hii ndio imetumika sana katika mission zote zinazohusu rocket zinazobeba watu tangu miaka ya nyuma

🔳Rocket ni kubwa kwa makadirio ya haraka haraka ina urefu wa Futi 212 ambayo ni sawa na mita 70 huku ikiwa na iwezo wa kubeba mizigo yenye uzito wa hadi tani 100-150 kwenda kwenye orbit ya kwanza ya dunia yetu

🔳Rocket hiyo itatumia engine 4 kubwa za Rs25 huku ikisaidiwa na Busta mbili zitakazokuwa pembezoni mwa rocket hiyo ambapo kwa majumuisho ya mashine zote hizo zitakuwa zinatumia takribani magaloni 1500-2000 kwa dakika 2 za kwanza ambapo rocket hutumia nishati kubwa sana ili kuweza kuzalisha nguvu ya kuweza kushinda kani ya uvutano ya dunia yetu (Galoni moja huwa na ujazo wa lita 3 )

🔳 Rocket nzima itakuwa na uwezo wa kubeba magaloni zaidi ya laki 780 ya nishati ambapo nishati kubwa ya humo itakuwa ikitumia gesi ya Liquid hydrogen na Liquid oxygen

🙌 Kesho nitadondosha link ya kuweza kutazama matukio yote juu ya urushwaji wa rocket hii

🙌 Kumbuka rocket haitabeba watu bali itabebshwa satellite ndogo kadhaa kamera za kushukua matukio yote kuanzia kwenda hadi kurudi , kumbuka rocket itakuwa ikijiongoza yenyewe yaani autonomous na kwa msaada wa maelekezo kutoka duniani itakayoiwezesha kwenda na kurudi tena mpaka na kutua.

Artemis the New Era of explorer our Moon
 
ROCKET YA MWEZINI KURUSHWA SIKU YA KESHO 29 AUGUST

Shirika la uchunguzi na tafiti zinazohusu anga za juu kwa ujumla NASA kufanya majaribio ya rocket itakayoweza kutumika katika safari za kuwapeleka wanaanga na vifaa mwezini katika masiku yajayo kwenye mission mbalimbali za kwenda kwenye gimba hilo

Kufanywa majaribio ya rocket ya Space launch system (SLS) kutafungua panzia jipya la ARTEMIS mara baada ya panzia la APOLLO kufungwa katika miaka 1972 ambapo tuliweza kushuhudia mwanadamu wa kwanza kabisa kukanyaga katika uso wa mwezi na kuendelea kushuhudia mwanaanga kadhaa katika mission mbalimbali za apollo kufanikiwa kufika katika gimba hilo la karibu zaidi na Dunia yetu

Katika mission ya Artemis itatuwezesha kushuhudia wanaanga wengine wapya wakiweza kukanyaga uso wa mwezi na kufanya mission mbalimbali mwezini huko huku kubwa zaidi likiwa ni lile la kutengeneza kambi yenye makazi mbalimbali ambayo itatumiwa na wanaanga na Raia wa kawaida watakao tembelea mwezini

Mataifa zaidi ya 20 yameungana na Nasa katika kuhakikisha jambo hili linafanikiwa mataifa ya kila pande za dunia yetu kwakuwa kulikuwa na makubaliano hapo mwanzo kwamba kwa masuala ya tafiti za anga za mbali basi mashirikiano yanatakiwa yadumishwe kwakuwa faida itakuwa ni kwa dunia nzima si kwa mtu mmoja mmoja au taifa moja moja

Majaribio yataanza kesho muda wa tisa na dakika thelathini mchana kwa masaa ya ya afrika mshariki

Rocket itarushwa kutokea katika kambi ya Kennedy space center katika Launch pad complex 39B , kumbuka chamber hii ndio imetumika sana katika mission zote zinazohusu rocket zinazobeba watu tangu miaka ya nyuma

Rocket ni kubwa kwa makadirio ya haraka haraka ina urefu wa Futi 212 ambayo ni sawa na mita 70 huku ikiwa na iwezo wa kubeba mizigo yenye uzito wa hadi tani 100-150 kwenda kwenye orbit ya kwanza ya dunia yetu

Rocket hiyo itatumia engine 4 kubwa za Rs25 huku ikisaidiwa na Busta mbili zitakazokuwa pembezoni mwa rocket hiyo ambapo kwa majumuisho ya mashine zote hizo zitakuwa zinatumia takribani magaloni 1500-2000 kwa dakika 2 za kwanza ambapo rocket hutumia nishati kubwa sana ili kuweza kuzalisha nguvu ya kuweza kushinda kani ya uvutano ya dunia yetu (Galoni moja huwa na ujazo wa lita 3 )

Rocket nzima itakuwa na uwezo wa kubeba magaloni zaidi ya laki 780 ya nishati ambapo nishati kubwa ya humo itakuwa ikitumia gesi ya Liquid hydrogen na Liquid oxygen

Kesho nitadondosha link ya kuweza kutazama matukio yote juu ya urushwaji wa rocket hii

Kumbuka rocket haitabeba watu bali itabebshwa satellite ndogo kadhaa kamera za kushukua matukio yote kuanzia kwenda hadi kurudi , kumbuka rocket itakuwa ikijiongoza yenyewe yaani autonomous na kwa msaada wa maelekezo kutoka duniani itakayoiwezesha kwenda na kurudi tena mpaka na kutua.

Artemis the New Era of explorer our Moon
Nasubiri Link.
 
Alafu mungu anakwambia yeye yupo mbingu ya Saba.
Wakati binadamu hata hiiya Kwanza hajaivuka
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom