Kiboko ya Jiwe
JF-Expert Member
- Apr 7, 2020
- 12,701
- 36,119
Habari wanajukwaa!
Natumaini hamjambo,
Hii sio kashfa bali ni ukweli mtupu.
Usafiri wa daladala hapa Dar ni kwaajili ya maskini.
Vijana tutafute pesa huku tukimwomba Mungu atuepushe na Usafiri huu uliojaa karaha na kadhia.
Haiwekani mtu una pesa zako usimame Kariakoo mpaka Mbagala, au usimame Kariakoo mpaka Tegeta.
Jioni ukitoka mjini kwenda pembezoni mwa jiji unavizia basi la kugeuka nalo ili upate siti, nako ukishangaa hupati.
Makonda jioni wanaringa kama wasichana mabikira.
Watu wananuka sigara mnapumuliana.
Mwendokasi nako niliwahi kupanda jioni nako hali ni ngumu. Kuna mfanyakazi mwenzangu alikatwa kidole na mlango wa mwendokasi asubuhi wakati anakuja kazini.
Hii picha chini haina uhusiano na mada bali iko hapo kuchangamsha mada.
Ni mimi mwanadaladala mwenzenu.
Natumaini hamjambo,
Hii sio kashfa bali ni ukweli mtupu.
Usafiri wa daladala hapa Dar ni kwaajili ya maskini.
Vijana tutafute pesa huku tukimwomba Mungu atuepushe na Usafiri huu uliojaa karaha na kadhia.
Haiwekani mtu una pesa zako usimame Kariakoo mpaka Mbagala, au usimame Kariakoo mpaka Tegeta.
Jioni ukitoka mjini kwenda pembezoni mwa jiji unavizia basi la kugeuka nalo ili upate siti, nako ukishangaa hupati.
Makonda jioni wanaringa kama wasichana mabikira.
Watu wananuka sigara mnapumuliana.
Mwendokasi nako niliwahi kupanda jioni nako hali ni ngumu. Kuna mfanyakazi mwenzangu alikatwa kidole na mlango wa mwendokasi asubuhi wakati anakuja kazini.
Hii picha chini haina uhusiano na mada bali iko hapo kuchangamsha mada.
Ni mimi mwanadaladala mwenzenu.