Narudia tena: Magufuli si wa kuchezea

britanicca

JF-Expert Member
May 20, 2015
15,635
29,967
Wanabodi wanajamii na watanzania kwa ujumla, nawasihi kila Siku kwamba namuona Magufuli kwenye sura za akina sokoine, Nyerere, Mkapa, Tumain el Kihwelu, na saa Nyingine ni kama Mrema Wa enzi zile,

Kwanza tumjue Magufuli ni nani,

Magufuli ni rais Wa jamhuri ya muungano Wa Tanzania,

Mambo yapi yanayoonesha magufuli hana utani kazini wala hataki kukwamishwa,

1. Wakati huu mamlaka zimekuwa active zaid kushughulikia wale wakosaji hata kabla ya yeye kutamka lolote maana wanajua akitamka ni mbaya zaid, bora watende kabla hajatamka

2. Magufuli hataki kutoa ahadi za kuridhisha tu , kama haiwezekan ni haiwezekan, fuatilia hotuba zake nyingi,

3. Magufuli ni mtu asiyependa kukwamishwa wala kubishiwa au kumtoa kwenye misingi anayoamini yeye,

4. Hacheki na MTU na hapendi kujaribiwa na hajaribiwagi

5. Upinzani na watu kwa ujumla wapo.kimya na wanachunguza maneno kabla hawajasema, imekuwa kama mwalimu nyerere vile, ukisema vibaya au kukashfu uko mikononi

6. Wala rushwa na wabadhirifu wanahaha wanashindwa wafanye nini kila kukicha maana njia zote kazibana

7. Magufuli ameweza kuelekeza hela za rambirambi bukoba zifanye mambo ya jamii ya bukoba na hakuna Wa kuhoji wanahoji chini chini,

8. Magufuli anania njema na Tanzania hivyo ukitaka kuleta ujinga tutakutunza sehem Salama kwanaza

9. Magufuli ndo kafanya Maalim seifu kukaa kimya na kuishia kujifariji kuwa kesi iko ICC, na kakataza fyokofyoko.

10. Magufuli ndo kafanya mnyika, mdee na wengine kukaa kimya maana utawala huu hauhitaji ujinga,

11. Magufuli ndo amesababisha Tanzania kujulikana upya uku Nje tulipo na kutambulika sana kama nchi yenye heshima,

12. Kama humjuhi magufuli hebu jaribu kumjaribu maana hata thread nyingi zinafutwa na mods kwa kuogopa,

13. Magufuli kafanya shilling ithaminiwe tena hakuna tip tena kwenya hoteli na bar

14. Mi namuona Magufuli kama MTU sahihi kuongoza nchi ambayo ilikuwa imepinda ,


Dah Magufuli!!!!!!!!!!!
 
Mi nilikuwa naziona flyovers kwa majirani zetu Kenya zikipendezesha jiji la Nairobi..nikahisi kwetu ni kitu ambacho hakitakuja tokea na hakiwezekaniki..khaa Jamaa kuingia naona zinachipua kama uyoga..noma sana..kweli kila kitu kinawezekana chini ya jua.
Ingawa dizaini kama umeandika kwa kejeli ila ukweli ni kwamba zinachipua. Nenda Kurasini ukaone, na sasa ujenzi unaendelea Tazara,makutano ya Mandela road na Nyerere road
 
Magufuli ni chaguo la Mungu anayesema ni dikteta aende Gambia akaone mfano.
Mungu yupi? au Mungu wa ccm au wa kabila lenu au wa dini yenu? Kama una maanisha Mungu wa Ibrahimu, Isaka na Yakobo yaani Mungu wa Biblia na hakika na nakuhakikishia zaidi ya 100% siyo yeye. Wewe una maanisha wa kabila lenu au wa chama chenu ccm. Nenda kasome Wafalme, uone wale waliotokana na Mungu kweli ukianzia na Daudi, walipokuwa wakitawala Israel ilikuwa inapatwa na nini? harafu ulinganishe na rais unaemsifia. Kabla hatujafika mbali tu democracy yenyewe tu ni mfumo wa kishetani, sasa rais anayewekwa na mfumo wa kishetani atokane na Mungu kweli?. Acha kabisa kudhihaki jina la Mungu, wee vipi? Franklin Roosevelt 33rd degree member marson na Rais wa 32nd wa Marekeni anasema hivi "Presidents are selected and not elected". So marais wengi huwa hawatokani wa matakwa ya wananchi, kuna kundi dogo tu katika nchi yoyote duniani ndo huwa lina amua nani wampe urais kwa interest zao. So usitake kuleta zako hapa. Unataka kuwa kipofu kama viongozi wa dini wa nchi hii? Toka usingizini na fumbua macho na uyaoshe.
 
80 Reactions
Reply
Back
Top Bottom