Narudia tena ,hatutakubali Rais Magufuli atukanwe kwa kisingizio cha ukosoaji

Kwanza naunga mkono hoja ya ukosoaji ,Kukosolewa kwa kiongozi au raia yoyote yule ni jambo linalokubalika kabisa ,na wala halina mjadala wowote.

Kwani kukosoa humfanya yule aliekosolewa kujitathimni utendaji wake au mwenenendo wake,kisha kufanya marekebisho kama ataona kuna umuhimu wa kufanya hivyo,halazimishwi hata kidogo.
Na ukosoaji mzuri,au mkosoaji mzuri ni ule/yule wenye Lugha ya staha na wenye kuweka njia mbadala (way foward),duniani kote wakosoaji hufanya namna hii.

Kumezuka tabia ya baadhi ya watu kupitia mgongo wa siasa, kufanya utovu wa nidhamu kwa kumtusi rais kwa kigezo cha kwamba wanakosoa ,na wakishughulikiwa ipasavyo kwa mujibu wa kanuni na sheria hudai wanaonewa,wanazibwa midomo,si kweli ,kama unatukana utazibwa mdomo tu,utake usitake,Rais ni kiongozi mkuu wa nchi ,ni alama ya taifa ,kumtukana ni kosa la jinai,si jinai tu,inakwenda mbali zaidi ,unapoonyesha utukutu uliokomaa.

Ushauri wangu kwa vijana hasa ndio ambao damu inachemka na mara nyingi ndio lika lenye misukosuko,kama kuna watu wanakutumieni kumtukana rais Magufuli ili mpate umaarufu na chochote kile ,kisha wao kuwatumia kama jukwaa lao kufikia malengo yao , mjichunge sana ,ni hatari kwa future yenu.

Naamini vijana nyie ni wasomi wazuri na mna elimu nzuri ya kukosoa yenye kuonyesha njia mbadala,itumieni ipasavyo sehemu ambayo mnaona haiendi sawa kwa kukosoa kupitia staha na si matusi.

Kumbukeni rais huyu alichaguliwa na watazania wengi,unapomtukana umetukana wale waliomchagua na wale wote wanaokubaliana na kazi yake,hivyo kujikuta wewe unajitengenezea wigo mpana wa maadui.

Badilikeni wakati ni sasa.kuna vijana ambao nawapongeza na ni vizuri mkawaiga,kuna Zitto kabwe,Hussein Bashe,hawa vijana wanaikosoa sana serikali bila ya matusi na huja na way foward,ndivyo inavyotakiwa,vinginevyo kosoaji ya umagharibi si asili yetu,mtaumia tu.
Upo sahihi Lakini pia hata hao wakubwa wetu wawe wanatumia maneno mazuri na siyo ya kuudhi
 
Shetani ambelezwi upewa makavu live,Congo Kenya viongozi wa dini kule uwachana live watu waovu,MTU muovu yapaswa atengwe Na jamii ili aujutie Na kuuacha uovu wake,mnaposhirikiana Na MTU muovu hadi madhabauni hamsaidii kuuacha uovu, tunache unafiki kuwapambapamba Na kuwapaka mafuta watu waovu,wapewe za USO wapewe makavu watengwe Na jamii.Kushirikiana Na watu waovu ni kuzidi kuwapa nguvu ya kuzidi kutenda uovu ktk jamii, nanyi mtakinywea kikombe cha Baba Kwa kuwa sehemu ya uovu.
 
Cha kuchekesha kile kinachoitwa ni kumtakana Rais watuhumiwa wakikamatwa na kupelekwa mahakamani waliotukanwa wanagaragazwa mahakamani kwa kushindwa kuthibitisha matusi waliotukanwa kutokana na kubainika kuwa waliosema ni matusi hayakuwa matusi.

Thus uwateka wakijua watashindwa mahakamani
 
Siku Madaraka yakikoma wakiwa nje ya system watalimia meno,hawana Madaraka, hawana walinzi,hawana amri ndipo hapo watakapovuna kisasi sawa Na walivowatendea wenzao Mali zao zikitaifishwa,kesi za uhujumu uchumi, matumizi mabaya ya Madaraka, upotevu wa watu,matumizi mabaya ya fedha za umma.Kuna watu ni vipofu twawasikitikia kesho yao.Leo Katumbi karudi Congo Kwa mapokezi ya mafuriko Dikteta Kabila limemshuka anaona aibu alidhani ana hatimiliki ya madaraka,yu ngali kijana ngoja Tsekedi amalize mda wake aingie mwingine avune malipo yake, dikteta Moi kaambiwa alipe fidia bilioni 16 Kwa uporaji wa Shamba la MTU,dikteta Mugabe Mali zake zikipigwa mnada kulipia madeni ya aliyokuwa madarakani. Mwafrika ni species yenye kiwango cha chini sana cha kufikiri hata awe ni PhD plusplus kadri anavosoma ndivo uzidi kupotea kwenye ujinga kabisa,tofauti Na jamii zingine
katika hayo usemayo ni kiongozi gani wa nchi namba moja ambae mpaka sasa analimia meno ,tuanzie kwa mzee Mwinyi mpaka Kikwete
 
Mkuu naye anayetukana ana madhaifu yake kama Rais aliyekuwepo NAYO,,Suala kwa nini wajichukulie sheria mkononi kutesa na kuua?kwa nini huyo MTU asishitakiwe akaadhibiwa kwa sheria zilizopo?hapo ndiyo tatizo,mkuu wangapi huku mtaani tunauwezo wa kuua wanaotukosea lakini hatufanyi kwa kuheshimu sheria.
Wenye hiyo roho ya mleta mada ya kuua wapo wachache sana.
Siku itafika ambapo kila Familia itakua imkumbwa na kadhia ya kutekwa kwa mpendwa wao ndipo Msako wa hao magaidi na majambazi yanayoteka watu utakapoanza.
Hakika halitasalia jiwe juu ya jiwe la wahuni na mashetani yasiyojulikana kwa sasa.
Siku yaja watageukana na kuuana wenyewe ili kupoteza ushahidi.

Hakuna uovu mzuri.
 
katika hayo usemayo ni kiongozi gani wa nchi namba moja ambae mpaka sasa analimia meno ,tuanzie kwa mzee Mwinyi mpaka Kikwete
Awakupanda miba njiani, walitazama kesho yao Leo wako Salama, walipanda mema wanakula mema,wako huru wakijichanganya Na jamii.
 
Najaribu kuwaasa,kama unaona sifai,jaribu ujinga
Harafu bado mkiambiwa mnateka na kua watu mnanunaaa. Ukiona umetukanwa njia za kistaarabu ni mahakamani tuu.hizo njia zingine ni uhawayani tuuu.

Zakaria wa tarime ndio kiboko yenu.
 
Siku Madaraka yakikoma wakiwa nje ya system watalimia meno,hawana Madaraka, hawana walinzi,hawana amri ndipo hapo watakapovuna kisasi sawa Na walivowatendea wenzao Mali zao zikitaifishwa,kesi za uhujumu uchumi, matumizi mabaya ya Madaraka, upotevu wa watu,matumizi mabaya ya fedha za umma.Kuna watu ni vipofu twawasikitikia kesho yao.Leo Katumbi karudi Congo Kwa mapokezi ya mafuriko Dikteta Kabila limemshuka anaona aibu alidhani ana hatimiliki ya madaraka,yu ngali kijana ngoja Tsekedi amalize mda wake aingie mwingine avune malipo yake, dikteta Moi kaambiwa alipe fidia bilioni 16 Kwa uporaji wa Shamba la MTU,dikteta Mugabe Mali zake zikipigwa mnada kulipia madeni ya aliyokuwa madarakani. Mwafrika ni species yenye kiwango cha chini sana cha kufikiri hata awe ni PhD plusplus kadri anavosoma ndivo uzidi kupotea kwenye ujinga kabisa,tofauti Na jamii zingine
Aha!!! Hapo mwisho umeharibu kabisa. Yaani Nyerere na Mimi umetuweka kapu moja na Madikteta washenzi!!!? Adolf Hitler na Augusto Pinnochet hawakuwa Waafrika ila walikuwa ni Madikteta!!!! Roho mbaya haina rangi.
 
Wenye hiyo roho ya mleta mada ya kuua wapo wachache sana.
Siku itafika ambapo kila Familia itakua imkumbwa na kadhia ya kutekwa kwa mpendwa wao ndipo Msako wa hao magaidi na majambazi yanayoteka watu utakapoanza.
Hakika halitasalia jiwe juu ya jiwe la wahuni na mashetani yasiyojulikana kwa sasa.
Siku yaja watageukana na kuuana wenyewe ili kupoteza ushahidi.

Hakuna uovu mzuri.
Kweli Mkuu ukisoma kitabu cha Marara behind the curtain ile hit squad ya Kagame mle ndani wengi walikuwa wanauana hata wao ili kupoteza ushahidi.
 
Watu kama wewe ndio mnamchanganya sana mkuu kwa kweli. Unaposema kuwa kuna watu wanamtukana huku hata mfano huutoi huoni haya?? Jamani, tujikombe sana lakini tutumie basi hoja nzito. Hivi unajua kuwa neno; Shikamoo mzee ni tusi japo uliyemsalimia ni mzee kweli?? Wenzio wanasema; Uzee mwisho Chalinze!!!! Sasa unaposema kuwa kuna watu wanamtukana mkuu bila kutoa hata ka mfano kadogo tu hapa mmbeya ni nani?? Basi na sisi tunakuonya kuwa; Acha kupeleka umbeya kwa mkuu. Wewe sio msemaji wake. Hakuna hata siku moja alishawahi kusema; Nimetukanwa nikanyamaza. Wewe ulipolisikia hilo tusi mbaona hukumkanya aliyetukana?? Ombeni u dc kwa njia nyingine
 
Bora ungeshauri iwepo siku ya matusi Tz kama ilivyo siku ya wajimga au sehemu ya kutukana kama ilivyosehemu ya kuvuta sigara, mtu unaenda hiyo sehemu unatukana weeeee ukichoka unarudi kwenu kulala au siku ya matusi kila mtu anatukana yeyote yule kadri anavyoweza kama ilivyo marekani wakati wa kampeni za uchaguzi na zile katuni zao.
 
Back
Top Bottom