Narudi kijijini kutafuta mke

Nyani Ngabu

Platinum Member
May 15, 2006
92,216
113,519
Wana MMU....

Kwa heshima na taadhima bila taraghani wala tahanani naomba mniweke kwenye sala zenu ili safari yangu iwe ya mafanikio.

Ni ombi la dhati kabisa na nawasihi msilichukulie kuwa takriri wala tashtiti za Ngabu.

Hii si mara yangu ya kwanza kujaribu bakhti yangu katika medani za wapendanao.

Miaka takriban hamstaashara ilopita nilijaribu lakini mambo yakaenda mrama.

Sasa napiga tena moyo konde nijaribu nione.

Naomba niwashirikishe kwa picha mtiririko wa safari yangu kuanzia Ubungo hadi Ikungulyabashashi....karibuni sana.

Safari ni hatua na yangu ilianza jana saa kumi na mbili asubuhi pale Ubungo....

20160522_063922.jpg


Mishale ya saa tano hivi tukaigongea hodi Morogoro.....mimi huyo hapo naongea na mchepuko kwenye simu.

20160522_120510.jpg


Shinyanga tukaingia usiku....nikalala hapo hapo stendi kwenye vibanda na asubuhi nikajidamka na kupanda Ally's hadi Ikungu....

20160509_063933.jpg


20160509_063845.jpg


Hatimaye majira ya alasiri nikakanyaga nyumbani Ikungulyabashashi...

20160510_174104_001.jpg


Karibuni nyumbani. Karibuni sana. Na karibuni wanzuki.
 
Samahani wacha nicheke tuu maana nimeshindwa kujizuia hahahahahahahahahahaaaa eehehehehehehehehhehehehheeeee uuhuhuhuhuhuuuhuhuhuuuuuuu iihihihihihihihhihihihiiii aahahahahahahhahahahaaaa

Baada ya cheko kila la kheri hahahahahahahahahahahahaaaa mbavu zangu mie looh.
 
Go away Kasinde.

Or else if I catch you gonna get it hot.

I said off I am man......was just having my last blast looh

There's no way you gonna catch me hahahahahahahhaaaaaaaa

Don't quote me......
Endelea na search yako
Napita tuu na sirudi tena hapa

Again don't quote me

Hahahahahahahahahahahahaaaa
 
Mkuu hata huku Daslam si wapo kina Mwallu na Masunga na wenzake? Au unamtaka aliyelelewa kijijini akiona gari anakimbia? Akiona mtu kwenye TV anamwamkia? Viatu anaweka kwenye fridge?

Nini hasa lengo lako la kumwacha Dotto Mayala hapa Daslam uende kuchagulaga kwa kina Nyanzala, Mabula, Jishuli????

Au ndo nyani mzee.tricks za mjini zimekushinda!??? Au hekaya za mungu wa kabili zimekuogofya? Why brother...???
 
Mkuu hata huku Daslam si wapo kina Mwallu na Masunga na wenzake? Au unamtaka aliyelelewa kijijini akiona gari anakimbia? Akiona mtu kwenye TV anamwamkia? Viatu anaweka kwenye fridge?

Nini hasa lengo lako la kumwacha Dotto Mayala hapa Daslam uende kuchagulaga kwa kina Nyanzala, Mabula, Jishuli????

Au ndo nyani mzee.tricks za mjini zimekushinda!??? Au hekaya za mungu wa kabili zimekuogofya? Why brother...???
Nyanzala mpaka azoee kubadili subway na kula bugger USA baby atakua amekomaa.
 
Back
Top Bottom