VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,135
- 17,802
Nimeshaanza safari ya kurejea Dar es Salaam nikitokea Kinampanda, Iramba mkoani Singida. Narejea Dar es Salaam kwa kazi maalum. Kazi ya kampeni bila 'shampeni'. Kampeni za kutangaza machungu ya wanaKinondoni kuanzia asubuhi hadi jioni. Nitampigia kampeni mgombea wetu wa CCM, Ndugu Mtuulia, kwa nguvu zangu zote.
Bila majukwaa wala kukaa, nitawaambia wanaKinondoni jinsi Mtulia asivyo mkweli na wa kumwamini. Nitawaambia wananchi mitaani na majumbani mwao jinsi Mtulia alivyoharibu hata utaratibu wa kichama kwa kutopitishwa kuwa mgombea ipasavyo. Nitawaambia na kuwapa nyaraka zenye baraka kuhusu kilichojiri alfajiri ya yeye kujiengua CUF na kujiunga CCM.
Mtulia, kaa chonjo. Jiandae. Nakuja 'kukuuza' kwa wananchi kwa maneno matamu ya kinidhamu na yatiayo hamu kwa mwanadamu. Nitapiga kampeni ili USICHAGULIWE. Kukuchagua Mtulia ni kuchagua hasara kwa Taifa kupitia Tume ya Taifa ya Uchaguzi. Ingekuwa nafuu na kueleweka kama usingegombea tena. Ungemuunga mkono Rais nje ya Bunge.
Sitakuwa na mgombea wa kumfagilia Kinondoni. Lakini, nina mgombea wa kumwanika kwa wanaKinondoni ili wakimchagua tena wasije wakachoshwa na kusikitishwa na mchezo wake wa kuhamahama. Mtulia, jiandae. Nakuja kukupigia kampeni za nguvu bila kutumia mabavu wala ukakamavu. Nyaraka zitatosha na kutisha.
Nabii Tito!
Mzee Tupatupa wa Lumumba (safarini kurejea Dar es Salaam)
Bila majukwaa wala kukaa, nitawaambia wanaKinondoni jinsi Mtulia asivyo mkweli na wa kumwamini. Nitawaambia wananchi mitaani na majumbani mwao jinsi Mtulia alivyoharibu hata utaratibu wa kichama kwa kutopitishwa kuwa mgombea ipasavyo. Nitawaambia na kuwapa nyaraka zenye baraka kuhusu kilichojiri alfajiri ya yeye kujiengua CUF na kujiunga CCM.
Mtulia, kaa chonjo. Jiandae. Nakuja 'kukuuza' kwa wananchi kwa maneno matamu ya kinidhamu na yatiayo hamu kwa mwanadamu. Nitapiga kampeni ili USICHAGULIWE. Kukuchagua Mtulia ni kuchagua hasara kwa Taifa kupitia Tume ya Taifa ya Uchaguzi. Ingekuwa nafuu na kueleweka kama usingegombea tena. Ungemuunga mkono Rais nje ya Bunge.
Sitakuwa na mgombea wa kumfagilia Kinondoni. Lakini, nina mgombea wa kumwanika kwa wanaKinondoni ili wakimchagua tena wasije wakachoshwa na kusikitishwa na mchezo wake wa kuhamahama. Mtulia, jiandae. Nakuja kukupigia kampeni za nguvu bila kutumia mabavu wala ukakamavu. Nyaraka zitatosha na kutisha.
Nabii Tito!
Mzee Tupatupa wa Lumumba (safarini kurejea Dar es Salaam)