unprejudiced
JF-Expert Member
- Jan 27, 2017
- 3,505
- 2,862
Hamza hakuwa gaidi kwa sababu zifuatazo:
1. Hamza baada ya kuwatwanga risasi aliendelea kutamba barabarani na bunduki zake zikiwa zimejaa risasi bila ya kudhuru raia ye yote.
2. Mahali ambapo Hamza aliuawa kwa kupigwa risasi na polisi ilikuwa wazi sana kiasi kwamba polisi wenye ujuzi wangeweza kimkamata akiwa hai bila majeraha au kwa kujeruhiwa miguuni.
3. Kitendo cha askari kuendelea kumpiga risasi Hamza hata baada ya kuanguka chini na kuendelea kuipiga risasi maiti ya Hamza inaonyesha polisi wetu ama kukosa weledi wa kazi yao au kupoteza ushahidi kwa makusudi. Kwani polisi waligeuza maiti ya Hamza uwanja wa range wa kujifunzia shabaha.
4. Hamza angekuwa gaidi wa kidini kama DCI Wambura anavyodai angekuwa ameshambulia makanisa mengi na pia angekuwa ameua wakristu wengi sana. Aidha angekuwa ameshambulia misikiti na waislam wasio dhehebu lake.
5. Kwa muda wote ambao amekuwa kada wa CCM, wanachama wenzake na vyombo vya usalama vingekuwa vimeshamtambua. Kumbukeni uovu haujifichi kwa muda mrefu namna hii.
Ugaidi hauendeshwi na mtu mmoja hivyo kama Hamza angekuwa gaidi lazima angekuwa na wenzake ambao muda huu vyombo vya usalama vingekuwa vimewabaini na kuwatia mbaroni.
Nawashauri polisi wafanye kazi yao au waombe msaada wa uchunguzi kubaini ukweli. Katika suala hili polisi ni watuhumiwa hivyo hawana uhalali wa kujichunguza wenyewe na kutoa ukweli.
Mkuu ulikuwa unafanya comparison na movie gani uliyoitazama. Who are you? Tell us more about yourself. We mwanachama wa CHadema?