Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,373
- 217,435
Ni lazima waandaaji wa mechi za soka watambue kwamba , soka ndio mchezo pekee unaounganisha watu wote bila kujali itikadi za kisiasa , Umri , Jinsia , dini , rangi wala makabila yao .
Kuweka kiongozi wa CCM kuwa mgeni rasmi wa mechi ya kimataifa ya CAF ni kitendo ambacho lengo lake ni kumtambulisha Kinana mbele ya Watazamaji , Jambo hili la kutumia soka kupata Ahueni ya kisiasa halikubaliki na tutalipinga kwa nguvu zote , LIWALO NA LIWE !
Kwani ni nani Hamjui Kinana mpaka muanze kuvunja protokali kwa kumpachika asipostahili , Waziri wa Michezo au viongozi wengine wa serikali wako wapi ? Halafu Kinana na Soka wapi na wapi jamani ?
Huyu Rais wa TFF wa sasa Karia ndio kiongozi wa soka wa Tanzania anayejiingiza mno kwenye siasa , jambo hili likiachwa liendelee litavuruga soka na kusababisha Fujo , iko siku tutaleta viongozi wa Chama Chetu ili wawe Wageni Rasmi bila hata kualikwa .
Majuto ni Mjukuu .