Napendekeza kuvuka daraja la Kigamboni iwe bure, then NSSF walipwe na Serikali kwa riba kama mikopo mingine

FRANCIS DA DON

JF-Expert Member
Sep 4, 2013
36,023
40,693
Huu hautakuwa mkopo wa kwanza kwa NSSF kuutoa kwa Serikali, Mabibo hostel, General Tyres upgrading, Machinga Complex na miradi mingine mingi isiyo na tija imepata mikopo toka NSSF, iweje kwa daraja la Kigamboni isiwe tu mkopo na ukalipwa taratibu na serikali kwa riba?

Hii itapanua wigo wa biashara kwa kuruhusu usafirishaji wa abiria na mizigo bila vinzingiti hivyo kuchagiza kasi ya maendeleo kwa ujumla.

Pia wale watumishi wenye degree na masters wanaokaa kaa kihasara hasara pale kwenye vibanda wakikusanya mia mbili mia mbili kama makonda wa daladala watapangiwa kazi zingine zenye tija zaidi.

Vinginevyo hata daraja la Kigongo busisi nao walipishwe? Hii ni haki? Na ukizingatia tayari tunakamuliwa tozo kama zote?

Tujadili.
 
Hapana!
Malipo yaendelee kwasababu kama watu wanafanya biashara na kuchangia kidogo sioni Tatizo.
NB: sometimes ushauri wa design hii ni lawama zisizo msingi
 
Hapana!
Malipo yaendelee kwasababu kama watu wanafanya biashara na kuchangia kidogo sioni Tatizo.
NB: sometimes ushauri wa design hii ni lawama zisizo msingi
Haiwezekani kodi tulipe kama wanavyolipa hao wa kigongo busisi, lakini daraja tulipie na bado tozo tunakatwa kama kawaida, why?!

Tunadumaza maendeleo ya wanachi kwa vitu ambavyo ni counter productive, hao watu wanaoshida hapo kukusanya hizo mia 2 watafutiwe kaziza kufanya, serikali ilipe hilo deni, kwani tozo tunalipa za nini?! Bado madaraja tulipie?!!
 
Ijue kwanza dhana ya PPP.
Serikali za Africa bado ni masikini kuweza kumudu miradi yote ya kimiundombinu inayohitajika ili kukuza uchumi
Hivyo kuhusisha sekta binafsi ni jambo jema na lisilokwepeka kana kweli tuna nia ya Kutoka tulipo
Ni Katika dhana hiyo ndio daraja la kigamboni lilipojengwa, Sasa serikali ikianza tena kuinunua ile miradi itakwama tu kibajeti.

Tujiulize je ni bora ungekaa foleni ya masaa kusubiri pantoni ambayo nayo unalipia, au upite darajani ulipe 1500-2000 bila foleni?Lisingekuwepo Watu tungekuwa tunalalamika ,Lipo Tunalalamika.
Hakuna maisha ya bure bure kwenye ulimwengu wa kibepari
 
Back
Top Bottom