Hongera sana Mtangazaji Harris Kapiga na ' Binafsi ' huwa unanivutia sana na endelea hivyo hivyo Mtu wangu kwani unapatia na upo vizuri kuliko Watangazaji wote ninaowajua ' duniani '. Pia pongezi kubwa ziende kwa Uongozi mzima wa CMG ( Clouds Media Group ) kwa kuwa ' Wabunifu ' na kutuletea huyu ' Mtangazi ' ambaye naamini mpaka sasa lazima tu atakuwa amewavutia wengi kutazama taarifa zenu za Habari.
- Anatangaza huku anatabasamu na sometime anacheka cheka
- Anatangaza huku kila mara akiwa anachezea chezea Kalamu yake
- Anatangaza huku kila mara akiwa ' anachomekea ' maneno yasiyoendana na Habari husika
- Anatangaza huku sometimes akiwa ' anatuhubiria ' pengine akijua wengi wetu ' tunaomkodolea ' tuna dhambi za ' Kutukuka '.
- Anatangaza huku mara zingine akitupa ushauri nasaha
- Anatangaza huku mara zingine ' anatubinyia ' macho ' Watazamaji ' wake hali ambayo kiukweli hutuvitia sana hasa sisi ' Watazamaji ' wake wa Kiume.
- Anatangaza huku mara nyingi akiwasifu mno wale waliopo ' Madarakani ' wa Lumumba street na kuwaponda wale wa ' Biafra ' street.
Niwaombe tu ' Watangazaji ' wengine wote wa ' Luninga ' nchini Tanzania muweze ' Kumuiga ' huyu ' Mtangazaji ' mwenzenu Harris Kapiga.
Nawasilisha.