Hahahaha!!! Mzee wa jicho la tatu.Umesahau sifa moja,kila kitu anakijua yeye
Nasikia jamaa yupo kwenye kundi la Ladies &Gentlemen..... Watoto wa Sinza wengi wanajua hili.. Ni kweli lakn au.!?Hongera sana Mtangazaji Harris Kapiga na ' Binafsi ' huwa unanivutia sana na endelea hivyo hivyo Mtu wangu kwani unapatia na upo vizuri kuliko Watangazaji wote ninaowajua ' duniani '. Pia pongezi kubwa ziende kwa Uongozi mzima wa CMG ( Clouds Media Group ) kwa kuwa ' Wabunifu ' na kutuletea huyu ' Mtangazi ' ambaye naamini mpaka sasa lazima tu atakuwa amewavutia wengi kutazama taarifa zenu za Habari.
- Anatangaza huku anatabasamu na sometime anacheka cheka
- Anatangaza huku kila mara akiwa anachezea chezea Kalamu yake
- Anatangaza huku kila mara akiwa ' anachomekea ' maneno yasiyoendana na Habari husika
- Anatangaza huku sometimes akiwa ' anatuhubiria ' pengine akijua wengi wetu ' tunaomkodolea ' tuna dhambi za ' Kutukuka '.
- Anatangaza huku mara zingine akitupa ushauri nasaha
- Anatangaza huku mara zingine ' anatubinyia ' macho ' Watazamaji ' wake hali ambayo kiukweli hutuvitia sana hasa sisi ' Watazamaji ' wake wa Kiume.
- Anatangaza huku mara nyingi akiwasifu mno wale waliopo ' Madarakani ' wa Lumumba street na kuwaponda wale wa ' Biafra ' street.
Niwaombe tu ' Watangazaji ' wengine wote wa ' Luninga ' nchini Tanzania muweze ' Kumuiga ' huyu ' Mtangazaji ' mwenzenu Harris Kapiga.
Nawasilisha.
Mimi Sam mahela. .....juma pili huwa napata shida sana. Huyo haris bora kumsikiliza kuliko kumtazama. .....japo kwangu baada ya kumuona tu hata kumsiliza siwezi tenaKwangu mimi huyu haris kapiga wa clouds na yule Gabriel Zacharia utangazaji wao haunivutii.... moyo huwa unaenda mbio sana situlii habari sielewi... Watanisamehe ila ndio hivyo....waache papara
Hivi huyo Ruge jina lake kamili huwa ni boss Ruge au ....Maana hata watangazi wa kituo hicho humwita kama wewe.Yaani sijui ndio boss Ruge alivyomfundisha, tatizo wasomaji wengi wa habari wanataka kumcopy Salim Kikeke bahati mbaya wanacopy vibaya
Nasikiaga eti huyu jamaa ni mambo safi.
Nadhani mtoa mada ana matatizo ya akili yaani utangazaji wake unaboa sijawahi kuonaSipendi utangazaji wake kiukweli
Sema papara!Jamaa utafikiri television yake hanaga papala....
CC:joseverest
Ndivyo wamuitavyo watangazaji wakeHivi huyo Ruge jina lake kamili huwa ni boss Ruge au ....Maana hata watangazi wa kituo hicho humwita kama wewe.
Sent from my GT-I9500 using JamiiForums mobile app
Nilimdharau kweli kwa hilo, uzuri Mungu aliona ikafeli mapemaHivi huyu ndo alifungua night club ya walokole? Iliishia wapi?
Yaani mkuu kuna watu wanajipambanua kama Wakristo lakini matendo yao...!Huyu jamaa ndio yule aliyeanzisha Night club (nadhani mnajua ndani ya night club kunafanyika nini ) ambayo anawaalika wasanii wa Gospel wanaenda kuburudisha wateja ????