Napenda kupiga push up

Yeah man uko sawa. Nimefatilia uzi wake tangu mwanzo ikiwa ni pamoja na michango ya watu humu lakini nikaona imekaa vibaya. Ila nilichofanya ni kupiga moyo konde kwa manufaa yetu wote nikaamua kuja na hizo bunduki.

Hii itawasaidia wengi hasa beginners na wazoefu kujifunza machache,tatizo la wadada walio wengi ni waoga na wakati mwingi wanazani kufanya mazoezi ni kujikomaza au kujiumiza. Pia Tanzania hatuna wataalamu wa kutosha wa kuelimisha masuala ya mazoezi na utumiaji wa vifaa mbadala wa vile vya wenzetu.

Habari mkuu, binafsi nina uzito wa 82kg ni kitambi pia. Nahitaji kukata tumbo vile vile kujazia mikono. Nifanye mazoezi gani ?
 
Piga pushups masai dada, mwili haukomai ukishazoea mwili unajicondition.haukomai kama John Cena wala Batista. humwoni Bruce Lee mwili simple.
 
Kukimbia ndio zoezi zuri iwapo unataka kuwa fiti.Kukimbia kutakukinga na magonjwa kama shinikizo la damu ,kiharusi, kisukari na saratani.
Push up itakujenga tu misuri ya mikono na kifua lakini haitokukinga na maradhi.
Iwapo mazingira hayaruhusu kukimbia bora ureke kamba kwa dakika 20-30.
 
Push Ups ni shida aisee....i find it tuff kuliko kupiga chuma. Honestly kuna kipindi i used to do 70 to 80 non stop...like 2 years ago.

Ila saa hvi 30 tu hoi. Lol
 
Pendelea kufanya aerobic exercises,haya ni mazoezi ambayo wakati wa kufanya unaingiza hewa nyingi safi mwilini na kutoa hewa chafu nje na kutoka jasho jingi,mazoezi haya ni kama kukimbia,mchakamchaka,kucheza mpira,kuruka kamba e.t.c....achana na anaerobic exercises ambayo haya ni mazoezi unayofanya ukiwa ndani amboko oxygen ni ndogo kama vile kupiga chuma e.t.c hayana faida sana kwa afya kwani huwa hayaunguzi mafuta mwilini kwa wingi!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom