Mwigamba Muchimati
Member
- Dec 4, 2018
- 15
- 28
Nakusalimu Nape, salaam. Pole kwa misukosuko ya kwenye Chama chenu. Pole kamanda maana mpaka wakati huu wewe ni mbunge tu wa Mtama. Sio yule Nape msemaji wa CCM, wala Waziri wa habari, utamaduni na michezo.
Wenye kumbukumbu tunakumbuka ukiwa Waziri wa habari ulivyofungia magazeti tuliyoyapenda. Tunakumbuka ulivyokuwa msemaji wa CCM ulivyokuwa unawakejeli wapinzani kwa mbwembwe. Tunakumbuka juu ya goli lako la mkono juu ya maamuzi ya watanzania. Ulijisifia kufunga kwa mkono. Mwanzoni refa aliweka katikati, sasa kaenda kuangalia VAR karudisha mpira. Ni wa adhabu baada ya kugundua wahuni wachache mlishika mpira. Mnalalamika nini?
Huko nyuma mlikuwa untouchables. Leo mnavuna mlichopanda, mnataka tuvune wote kweli? Mlikula mkiwa kivulini, sisi tukiwa juani. Leo nanyi mnaonja jua eti mnataka tuwe wote, kweli? Oteni jua wenyewe sisi tulishazoea! Yaani mnaona mianya yenu ya kupata nafasi za uongozi inazibwa ndo mnajifanya wazalendo. Acheni mambo hayo bwana!
Mlitutahadharisha kubatizwa kwa moto, leo tuliotarajiwa kubatizwa tumeshaokoka, mmegeukiwa nyie baada ya mbatizaji kuwajua mlikuwa wapagani! Batizweni mjue ubatizo wa moto jinsi ulivyo. Ama kweli mwosha huoshwa!
Wenye kumbukumbu tunakumbuka ukiwa Waziri wa habari ulivyofungia magazeti tuliyoyapenda. Tunakumbuka ulivyokuwa msemaji wa CCM ulivyokuwa unawakejeli wapinzani kwa mbwembwe. Tunakumbuka juu ya goli lako la mkono juu ya maamuzi ya watanzania. Ulijisifia kufunga kwa mkono. Mwanzoni refa aliweka katikati, sasa kaenda kuangalia VAR karudisha mpira. Ni wa adhabu baada ya kugundua wahuni wachache mlishika mpira. Mnalalamika nini?
Huko nyuma mlikuwa untouchables. Leo mnavuna mlichopanda, mnataka tuvune wote kweli? Mlikula mkiwa kivulini, sisi tukiwa juani. Leo nanyi mnaonja jua eti mnataka tuwe wote, kweli? Oteni jua wenyewe sisi tulishazoea! Yaani mnaona mianya yenu ya kupata nafasi za uongozi inazibwa ndo mnajifanya wazalendo. Acheni mambo hayo bwana!
Mlitutahadharisha kubatizwa kwa moto, leo tuliotarajiwa kubatizwa tumeshaokoka, mmegeukiwa nyie baada ya mbatizaji kuwajua mlikuwa wapagani! Batizweni mjue ubatizo wa moto jinsi ulivyo. Ama kweli mwosha huoshwa!