Nape: Wapinzani wachukue watuhumiwa ufisadi CCM

U-wenye heri wa Mzee Nyerere ndugu Nape siyo mambo ya siasa ,ili apete hilo daraja inabidi factsheet ijae mambo ya kumpendeza mungu kiukristo siyo hayo uliyoyataja eti ya uadirifu ndani ya chama.Kwa hili wewe kwa mjibi wa kanisa katoliki umeonyesha ni mbumbu kabisa kabisa. Katika huu mchakato wa kupelekea Mzee Nyerere atangazwe ni mwenye heri (bado hajatangazwa) kanisa katoriki (papacy) huko kwa papa wanasubiri sasa mashuhuda washuhudie muujiza mmoja ambao candidate ameufanya , na muujiza huo utatangazwa dunia nzima wajue na wauhakikishe. Nachopenda kukufahamisha Ndugu Nape ni kwamba suala la kumtangaza Mzee Nyerere mwenye heri siyo la chama cha CCM au Kardrinari pengo bali ni la Baba mtakatifu baada ya kupata ushuhuda wa muujiza toka hapa tz au kwingineko.

Hata hivyo Ndugu NAPE Mzee Nyerere anakabiliwa na vikwazo vikubwa vitatu ambavyo kwa mjibu wa canon law vinaweza kumkwamisha kufikia daraja hilo:-

1. Katika wadhifa wake wa urais aliidhinisha kisheria death sentence mbili, ya yule mhindi na ya Mwamwindi yule mhehe aliyemmua Dr, Kreruu.( hii ni kinyume na sheria no 6 ya Mussa alizopewa na mungu).

2. Pia katika maisha yake aliidhinisha vita kati ya tz na uganda, mambo haya huwa hayampendezi mungu,

3. Kumwachia Cassim Hanga kwenda Zanzibar pia inaweza kuwa ni kikwazo,alichotakiwa kufanya ni kumbakiza
hukuhuku bara, kwa kweri huyu jamaa yaliyoenda kumkuta kula zenj Mzee Nyerere hawezi kukosa kuwajibika
mbele ya mungu.

Ninakuambia haya kama Mroma niliyebobea, tutakufa wote hata wale waliozariwa leo Nyerere hajapata daraja la uwenyeheri, Pia ninakukanya Nape usiseme mambo usiyoyajua vizuri;

Huwa tunamalizia na TUMSIFU YESU KRISTO.
Hongera mkuu kwa ufafanuzi, hapa inatosha.
Nape analeta propaganda kwenye mambo ya dini!
 
Hiki ccmafisi na Nepi wao hakuna jipya kweli kama analionea huruma watanganyika tangu achaguliwe katibu mwenezi wa ccmafisi ina maana bado alikuwa amekumbatia ukuu wa wilaya. Wanajilimbikizia vyeo na hata huyo mwenyekiti wao ndio bomu bomu. Kila siku tunamsikia Nepi yuko kwenye shughuli za ccmafisi kwanini. V.Gama akumchagua mkuu wa wilaya mwingine. Halafu Nepi anasema ccmafisi ni chama kisafi, namuuliza hawa wafuatao kama Julius K. Nyerere angelikuwepo waangekuwa kwenye ccmafisi. Mkapa, Chenge, Lowassa, Rostam, Mramba, Ngeleja, Jairo, na wengine wengi tu.
 
Nape bana!!!! Na hao akina Nkapa ,Megawati,Mkulu na wengineo ni wasafi?hata wewe ni fisadi unatakiwa ujivue gamba.
 
huyu jamaa kama angekuwa anayasimamia yale yote anayoyahubiri angekuwa mtu mwenye mafanikio makubwa tu kwa nafasi yake ndani ya chama vinginevyo ni hadith zilezile
 
Huyu ni katibu mwenezi wa CCM hapa anampongeza Makongoro Nyerere kana kwamba wale akina Kimbisa siyo wagombea wa CCM!!

[h=6]Nape Nnauye
[/h][h=6]Kamanda Hongera sana! Jamaa wanalia nguvu walotumia usipite si mchezo! Capt. Unatisha!! Tunawasubiri Mara![/h]

Je wadau hivi hapa mnaweza kusema hiki ni chama kimoja? kwamba Nape yeye wagombea wake aliyeshinda ni mmoja tu!!...hivi je huyu kijana kweli huwa anafikiri kabla ya kutenda au anatenda halfu ndio anafikiri!!??
 
jk na wengine baadhi wameshashituka jinsi 'jahazi' la ccm linavyozama lakini hawawezi sema hadharani kwa vile wanajua wao ndio chanzo cha yote.

huyu nape namfananisha kidogo na watawala wa iliyokuwa Ujerumani Mashariki, walikuwa wakiambiwa kuwa ukuta unaangushwa lakini watu wa 'usalama' wanamhakikishia rais kuwa hali ni shwari mpaka rais alipokuja kuangalia kwenye tv kuwa the wall had gone! Kikubwa zaidi kwa nape nadhani sio uelewa bali ni unafiki uliokithiri
 
Swala la kumpongeza mtu alieshinda ni la kawaida sana, hata aliposhinda Nasari wa CDM alimpongeza pia, isitoshe makongoro ni wa CCM, hivyo sioni ajabu. Nami nampongeza Makongoro na Wabunge wote walioshinda jana
 
Simshangai Nape Nnauye kwa sababu elimu yake na mawazo yake yameshikiliwa na watu. Hana maamuzi kama yeye, afikirii kama kijana na wala hana uzalendo kwa taifa. Tatizo ni kambi na umaskin uliokithiri.
 
Mkuu mi nadhani hao wanakuja CDM ili kuwakomoa CCM na wanajua kabisa hawatapewa kipao mbele,wao ni kama wanachama wa kawaida tu

TIMING kila siku CHADEMA wanakuambia siasa zao ziko juu ya vyama, huelewi; chukua muda ujifunze kuelewa mtu akiongea. Kama hawa watu watakataliwa kila wanakokwenda, basi wafukuzwe nchi, lakini ujue uwe CDM au CCM kinachojalisha kwa CDM ni kosa lako sio uanachama wako; hakuna sehemu yoyote kumeandikwa uanachama ni kinga dhidi ya maovu isipokuwa udhaifu wa CCM ndo unakufanya ufikiri kuwa mwanachama umeukata, subiri uone siasa za juu ya vyama.
 
It could be walikuwa wamekaa pamoja, kwa hiyo akampa mkono wa pongezi kama inavyoonekana ...wewe uliyeshuhudia tupe mazingira yalivyokuwa wengine hatukuona.......Kuhusu kukiua CHAMA, nakubaliana na wewe strongly, nimekuwa nikimfuatilia sana Nnape siasa zake, he is more of muimbaji wa taarabu, mpaka napata wasiwasi na Elimu aliyoipata kama anaitumia vizuri kama inavyotakiwa au lah...Nitakupa mifano michache ya Nnape,,,Jaribu kufuatilia hata posts zake kwenye mitandao ya Kijamii, u wouldnt expect mtu kama yeye mwenye dhamana kubwa kuandika vitu ambavyo havipotray kama yeye ni kiongozi!!Namna anavyowasilisha hoja zake, jamaa ni hopeless kabisa!!Juzi C.C.M wameshindwa uchaguzi Arumeru, aka announce kuwa wameridhika, huo ni ukomavu wa kisisasa lakini haikuonyesha kama alikua ameumia kwa namna yoyote na kuwa wanaweza kufanya kitu ili kurectify the situation kwa wakati mwingine pindi uchaguzi utakapotokea...Juzi James Millya amehama Chama, Kiongozi ambaye ni Kiongozi kweli huwezi kushangilia kuwa member wako amehama chama, tena unasimama na kusema kuwa amekipunguzia chama kazi ya kumfukuza,kwa kauli aliyoitoa ameonyesha kuwa sio kiongozi mzuri, Millya alikuwa kiongozi kama yeye, hakutakiwa kumponda na kumchafua kiasi kile!!Ukomavu wake angesema kuwa tunasikitika amehama lakini tunamkaribisha tena endapo akiamua kurudi nyumbani we will be willing kumkaribisha tena. Alitakiwa aongee in such a way, Millya ikiwezekana a feel guilty kwa kuondoka kwenye familia iliyompenda sana!!! Huo ndio uongozi bora na sio bora uongozi!!! Kwa kauli ya Nnape inaonyesha kuwa yeye na chama chake ni wafa maji ambao hawawezi kuacha kutapatapa, and thus many will follow!!Wengi watajitoa kwenye C.C.M kwa kauli za Nnape...Let's be realistic!!!!!!
 
why NAPE????????????? kweli jamaa anatisha,yaani CHADEMA wanamuogopa huyu jamaa kuliko hata ZITTO...NAPE songa mbele nyota yako inang'aaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa may be u deserve to be our next senior leader...CCM watch out,this guy is capable to handle and tackle all enemies in-out of party for the growth and advancement of our nation.
I can rank him as a leading YOUNG leader for outstanding performance in advocating EQUITY and mutual benefit to our natural resources !
The following are;
ZITTO KABWE
JANUARY MAKAMBA
DEO FILIKUNJOMBE
JOHN MNYIKA

add more...
 
Pongezi za dhati kwa mh.Nape na Sekretarieti kuu ya CCM kwa kuwamwagia tindikali magamba ili yajipukutishe yenyewe.....hakika CCM mpya itazaliwa na kujenga misingi bora ya uongozi.

Hakikisheni mnaisimamia serikali vizuri ili SERA za CCM zitekelezwe bila WOGA kwa manufaa ya TAIFA nzima. CCM inahazina ya wasomi wanaoweza kuleta mageuzi ya kiuchumi bila kuwa tegemezi.

Naombeni msirudi nyuma hata 1mm katika hili,tumieni mbinu zenu kusambaratisha mtandao wa MAGAMBA haraka sana, kwani hilo ndiyo tumaini JIPYA tofauti na CHADEMA kusubiri MAGAMBA yahamie kwao ili wakaandae MAJUNGU na kuwachafua VIONGOZI wa CCM....PENYE ukweli UONGO hujitenga!!!!

Haiwezekani gamba kuwa msafi akihamia CHADEMA hata kwa 1%,kwa vile hata viongozi wana ROHO za magamba ndiyo maana wanafurahia wakiona jumuiya yao inaongezeka.Pia nawashauri kumchunguza SABODO yule mdosi ambaye PESA yake hainakazi xaidi yakutafuta umaarufu kwenye VYOMBO vya HABARI ati anawachangia CDM wakati hapa DSM kuna omba omba kibao wanahitaji misaada ya hali na MALI, kuna wagonjwa wengi sana ambao wana COMPLICATED cases zinazohitaji operation za ma milioni ya FEDHA lakini hawasaidiwi...HUYU ni MNAFIKI, CCM hatupo hivyo, ni heri anyang'anywe uanachama ili ajiunge na hao mgambo wa MTEI. Ni muda MUAFAKA kwa magamba mnao sitasita kuachia ngazi zote mara moja ili msichafuke zaidi...igeni mfano mzuri wa RA.....

Kidumu chama cha MAPINDUZI.......kilaaniwe chama cha wahuni na majambazi na kife mara moja ili kisicheleweshe MAPINDUZI ya KWELI.
 
Greenstar, ikifika 2015 tutakukumbusha kuhusu huu waraka wako uusome wewe mwenyewe. Usifiche kicwa kwenye kichaka wakati kiwiliwili chote kipo nje. Tafuta kijana wa darasa la nne atakuelewesha vizuri.
 
Kweli tuna tatizo kubwa la uelewa na hili linaigharimu sana nchi yetu, sasa twende taratibu ili hata tutusa aelewe nilikusudia kufikisha ujumbe gani.

Nape ni katibu Mwenezi wa CCM yeye wagombea wote wa CCM ni wake, alitakiwa atumie wasaa huu kuwapongeza wote walioshinda na kuwapa faraja wote walioshindwa.

Lakini kwa mtu makini unaweza kusoma saikolojia za binadamu Nape hawakilishi Maslahi ya chama bali maslahi ya Makundi na katika kundi lake ni wazi inaonekana aliyepita ni huyo mmoja tu Makongoro nadhani wote mnafahamu ni nini kilichompata William Malecela.

Hapa Nape amejisahau kabisa kwamba yeye ni taswira ya chama kizima cha CCM na siyo kwamba Makongongoro alikuwa anashindana nakina Lowasa ili awashinde, kwa vyovyote vile iwavyo inaonekana dhahiri kundi la Nape ni majeruhi wa uchaguzi huu wa EA, ningependa kuwahahakikishia kama kuna mgombea mlikuwa mnadhani alistahili kuchaguliwa na hakuchaguliwa jana basi dhambi yake kuu ni kuwa kwenye kundi la huyu Nape Nnauye, Le Mutus ni mmoja wa wahanga wa maamuzi yao ya hovyo.
 
Back
Top Bottom