Nape: Tutaanza kuwatumia vijana wetu kulinda viongozi

Nape kauli yako inaonyesha wazi kwamba mnatafuta sababu za kuvuruga kampeni na kuchakachua matokeo ili mjihamishie ushindi. Leo hii mnatuletea kauli za uchochezi eti mtatumia vijana wenu kuhakikisha ulinzi kwa watu wenu, je vyama vya upinzani navyo vikiamua kujibu mapigo kwa style hiyo mtakuwa mmemtendea nini huyo mwananchi aliyeko hapo Igunga?

Mlianza kwa kuwapokea wale wasaliti wa Arusha na mkawakumbatia, ili kuendeleza unafiki wenu mnajidai kulalamika eti DC hakutendewa haki mbona hamlielezei hilo kosa alilolifanya? Mnapotosha watu kwa kutoa mifano ya Arusha na Mwanza, aliyewambia huo ubaguzi wenu tunautaka ni nani?

Mnashindwa kutoa ulinzi kwenye mambo ya maana, eti mnaanza kulindana nyie kwanza, wizi mtupuuu!
 
Nape tukutane Igunga na vijana wako tuambie watafika lini nasisi tuanze safari...
Ndugu Crashwise; habari za siku nyingi, mimi naona CCM wamechanganyikiwa wanadhani wanaweza kuendelea na matisho yao milele nafikiri sasa itoshe na tusiwaruhusu kuendelea kututambia katika nchi yetu, hapa ndio watanzania hasa vijana inabidi tuonyeshe uwezo wetu wa kukataa kuburuzwa na hao wabunge wetu waliokamatwani lazima tuwatete.
 
Hivi anavyo sema hivyo anafikiri vyama vingine vya siasa havina vijana wao wa kuwatumikia katika ulinzi. nasema niwakati muafaka kwa vyama vya siasa kuanzisha military wings zao. Huko mbele lazima tupigane kuikomboa nchi hii na mkoloni mweusi ambaye ni viongozi wanaotutawala sasa na familia zao.
Kweli kabisa ndugu hawa manyang'au wametufanya sisi kama watu wasio na mwelekeo hawajui kila siku tunazidi kuchoshwa na mambo yao ambayo kwa kiasi kikubwa yazidi kutudidimiza. sasa wameona hatupo pamoja nao wanataka kutumia maguvu hapo na sisi hatukubali safari hii lazima ile kwao tu!
 
Kauli ya kiongozi mwandamizi Nape Nnauye, kwamba watawapeleka Vijana wa Chama Chao waliopewa mafunzo ya kijasusi kulinda Viongozi wao ni la hatari sana na kusikitisha. Tatizo sio kuwa na hao walinzi, tatizo ni nadharia na nia ya kuwa nao. Je kweli Viongozi wa CCM wana hitaji ulinzi kutoka jeshi la kijasusi la CCM?

Je hao majasusi wa CCM watafuta sheria za nchi gani, watawezeshwa vipi watakuwa na mipaka gani ya kutenda kazi zao, je wapo kisheria. Na vyama vingine vinaruhusiwa kuwafundisha vijana wao mafunzo ya kijasusi na kijeshi ndani ya Ardhi ya Tanzania na kufanyakazi sambamba na polisi, usalama wa atifa na JWTZ? Kweli hii ni nchi au imekwisha katika vipande?

Nape Moses Nnauye anatakiwa kujua kuwa CCM ndio inaongoza dola, polisi, Jeshi, na usalama wa taifa wako chini yao. Ni wajibu wa serikali iliyoko madarakani kuhakikishia jamii usalama wake na ulinzi wa mali zao na uzima wao. Leo kama Chama tawala hakiamini vyombo vya ulinzi na usalama nani aviamini? Kauli hizi za kukurupuka zimezifikisha nchini nyingi kubaya. Nilitegemea kauli za kutotumia akili zitolewe na maajuza sio vijana ambao bado tupo sana kwenye nchi hii tukiihitaji amani na utulivu wa usawa mbele ya sheria.

Tunahitaji haki na usawa wa ulinzi, ni vyema wakuu wa mikoa, wilaya, OCD, Rpc nk wakafanya kazi zao bila upendeleo, ratiba zifuatwe na kila chama kipewe mazingira mazuri kufanya shughuli zake za kisiasa, hujuma zilaaniwe na vyama vyote na ustaarabu uwe ndio ngao. Tujenge utamaduni wa kushindanisha hoja sio nguvu. Ikumbukwe kuwa baada ya uchaguzi wananchi wataendelea kuishi maisha yao, siasa za chuki na uadui hazimnufaishi yeyote awe CCM, CDM, CUF au TLP, kama kweli nia ya wagombea wetu ni kuwatumikia wananchi mabomu ya nini? Waacheni wapiga kura waamue. Ukijaribu kuangalia kwa undani siku zote wapiga kura ni watulivu ila wanasiasa hasa wa CCM ndio husababisha fujo pale wanapoona mambo hayaendi Vizuri.

Kiongozi lazima awe kioo cha jamii, swala la dhuluma na mafumanizi yanatakiwe yawe ni matendo ya kukiuka maadili na uenezaji wa ukimwi na magonjwa ya zinaa bila kusahau kuzalilisha wana ndoa na kina dada zetu kwa malipo duni. Kitendo alichokifanya Mwigulu ni cha kulaaniwa na wote na anatakiwa ajiuzulu kwa kudhalilisha utumishi wa wananchi.

Tuijenge Tanzania, vijana tuliowaamini msituangushe, jaribuni kutumia busara, hekima, elimu kwenye maamuzi na matamko yenu sio kila unaloambiwa lazima uliseme, utakuja sema matusi eti sababu chizi alisema useme.
 
  • Thanks
Reactions: MPG
Figganigga,
AIBU SANA WAKATI WENZENU TUNAFANYA SIASA YA NGUVU YA HOJA NYIE MNAFANYA MNAHANGAIKA NA HOJA YA NGUVU, MSHAPIGA PUA, LAKINI KWAKUWA HUMU KUNA WATU ILI WALALE LAZIMA KUMTAJA NAPE, SINA NENO AJENI TU MPAKA MKIPATA USINGIZI LALALENI, MKIAMKA ILI MSNHNDE VIZURI TUKANENI TENA KWA MATUSI YOTE, KARIBUNI SANA SANA
 
Huyu NAPE anaakili mgando ni vijana gani anaowazungumzia,mana vijana wote wenye akili timamu hawaipendi CCM,mana hawana ajiri,hawana maisha bora,NAPE unawazungumzia vijana gani?au unawazunguzia vijana wasiojua kusoma na kuandika ambao mmewasababishia kuwa hivyo kwa sera zenu za maji taka.Limbukeni mkubwa wewe VUVUZERA
 
nape asema sasa wataanza kuwatumia vijana wao kuwalinda viongozi wao.ameongeza kusema haiwezekani watu wa arusha na mwanza waende igunga kubaka watu,kudhalilisha wakina mama na kupigana mapanga.anasema wao hawatakubali.ameongea na waandishi akiwa dar.
my take;
ccm maji yamewafika shingoni na wanashindwa wafanyeje.sasa waameanza siasa za maji taka na ubaguzi wa kusema watu wa arusha hawatakiwi kwenda kwenye kampeni igunga.anafikili ccm ndo ina vijana tu.nape mwaka huu mnalo na limewaganda.
chanzo ch10.mia

Zuluma, zuluma, zuluma, utapeli, utapeli, utapeli, ama kweli ****** nchi imemshinda mpaka Nape anaanzisha jeshi lake, ****** awe macho linawezekana ni lakumpindua bosi wake. Walishajua ya kuwa hata polisi wameshawakimbia wapo wanatapatapa tu. Vurugu zitaanzishwa na wao wenyewe.
 
Wewe nepi, ccm ina vijana? Mmebaki na wazee tu. Makandas wote kitaa ni cdm. Ok waandae hao unaowaita vijana, chagua uwanja wa mapigano, tupambane.
 
Figganigga,
AIBU SANA WAKATI WENZENU TUNAFANYA SIASA YA NGUVU YA HOJA NYIE MNAFANYA MNAHANGAIKA NA HOJA YA NGUVU, MSHAPIGA PUA, LAKINI KWAKUWA HUMU KUNA WATU ILI WALALE LAZIMA KUMTAJA NAPE, SINA NENO AJENI TU MPAKA MKIPATA USINGIZI LALALENI, MKIAMKA ILI MSNHNDE VIZURI TUKANENI TENA KWA MATUSI YOTE, KARIBUNI SANA SANA

Ni hoja gani hizo za kwenu unazoziongelea? Embu zungumza basi ktk hili labda wapo watakaokupigia angalau makofi hata ya vidole viwili vya miguuni! Ukweli unauma eeeh! Huna cha maana cha kuongea Nape sera zako zote zimejaa upupu na ndo maana watu wakikukosoa unaishia kulalamikia matusi na kujifanya Mungu mtu eti watu hawalali bila kukutaja wewe! Hii ndo hoja ambayo umeiona ni ya msingi? Huo uchafu mnaoufanya huko na aibu za kufumaniwa, nyie kwenu ni sifa?

Kama kweli mnajali usalama, ina maana leo hii baada ya vurugu ndo mmegundua kuwa wananchi wanahitaji usalama kama si uongo huo! Wakati mnawapandisha wale watoto kwenye lori la kampeni yenu mlikuwa na maana gani kama kweli lengo lenu ni kulinda usalama?

Hilo jeshi lenu la chama mnalotaka kulipeleka Igunga ni nani analitambua, na lengo lake ni nini kama sio kulinda maslahi ya chama chenu ikiwemo kulinda sana uchakachuaji wa kura? Acheni vyombo husika vya serikali viifanye hiyo kazi na sio muipeleke ki ccm ccm!
 
Hili tangazo la kulinda viongozi litakua ni baada ya lile tifu la Baunsa Shaaban ambapo jamaa alibipu kichapo!!!
 
Kwa mtaji wa tamko hili la dogo Nape ni dhahiri kwamba damu yoyote itakapodondoka Igunga basi CCM wanalo la kutujulisha kama taifa.
 
Kwanza Dar kafuata nini? Si akae Igunga kufanya kampeni?

Mwaka huu wanalia sana tu
 
Nnauye Jr,mimi nilitegemea ukanushe niliyosema.sasa mbona unakimbilia kusema nmekutukana.thread ipi ambayo nilishawahi kukutukana?wewe nakuheshimu kama binadamu mwingine yeyote lakini nakudharau kwa jinsi unavyo rudisha nyuma jitihada za watanzania kujikombo na jinsi usivyokuwa na uchungu na nchi yako.ukiwasiliba CHADEMA kesho utakimbilia wapi?au unafikiri ccm wanakupenda?hapo umewekwa kama boya tu.acha tamaa ya pesa na sifa za kijinga.nafsi yako itakusuta.jiangalie kwenye kioo kabla hujasema neno.mia
 
Nnauye Jr,

Mimi nilitegemea ukanushe niliyosema. Sasa mbona unakimbilia kusema nmekutukana. Thread ipi ambayo nilishawahi kukutukana? Wewe nakuheshimu kama binadamu mwingine yeyote lakini nakudharau kwa jinsi unavyo rudisha nyuma jitihada za watanzania kujikombo na jinsi usivyokuwa na uchungu na nchi yako.

Ukiwasiliba CHADEMA kesho utakimbilia wapi? Au unafikiri CCM wanakupenda? Hapo umewekwa kama boya tu, acha tamaa ya pesa na sifa za kijinga nafsi yako itakusuta.

Jiangalie kwenye kioo kabla hujasema neno.
 
Mbona kashindwa kwenda Igunga kupiga kampeni sianajiona mchafu kwa wana igunga!!??
 
Kwanza kabisa ningependa kumsahihisha Nape. Hakuna kijana mwenye akili timamu ambaye bado anaisupport Magamba. Labda angefafanua kwa hili ni kwamba wanawapeleka Wavuta bangi wao kufanya fujo Igunga.

Taadhari: Hivi kila chama kikipeleka Vijana wake Igunga, amani itakuwepo kweli! Acheni kutumia Masaburi kufikiri. CCM lazima mkubali kwamba kushindwa kwenu Igunga si dhambi na wala si tatizo pekee mlilonalo kwa sasa. Lazima mtambue kwamba kwa sasa chama chenu kipo ICU. Jitieni moyo maana mlivyo na moyo wa ajabu, mnaweza hata kumkorogea maiti uji mkitegemea atafufuka.Igunga kwenu ni la kuvunda.
 
Nape! ipo siku utachezea kichapo hadharani na kama lengo lako ni kupeleka hao majasusi wenu huko Igunga nakwambia siku zako za kuishi hapa duniani zinahesabika utakufa kwa tamaa zako za pesa na urafi wa madaraka...
pole sana kijana mwenzangu nilitegemea maneno uliyoyaongea jana uyaongelee Igunga, unaongea huku umejichinbia DSM...
haa haaa pole sana
 
Back
Top Bottom