kapotolo
JF-Expert Member
- Sep 19, 2010
- 3,727
- 2,214
Nilimsikiliza Nape Juzi akihojiwa Mlimani TV, moja kati ya mikakati yao ni kuwafikia vijana wengi popote walipo. Kati ya njia wanazozitumia ni kutuma vijana waingie kwenye mitandao ya kijamii ambako wanaamini kuna vijana wengi na hii itawasaidia kuwapata.
Hili wimbi la wanachama wapya kwenye hii mitandao, hususani jamiiforums, ambao wana itikadi za kimagamba limenifanya niamini kauli hii ya Nape. Lakini waje wakitambua vijana wa kileo wanajitambua na propaganda za magamba haziwezi tena kuwashawishi.
Hongera Nape lakini hii strategy, kama zilivyo nyingine, naamini haitafanya kazi kwa kuwa mfumo wa uendeshaji wa chama chenu cha magamba ni mbovu na ndio tatizo.
Hili wimbi la wanachama wapya kwenye hii mitandao, hususani jamiiforums, ambao wana itikadi za kimagamba limenifanya niamini kauli hii ya Nape. Lakini waje wakitambua vijana wa kileo wanajitambua na propaganda za magamba haziwezi tena kuwashawishi.
Hongera Nape lakini hii strategy, kama zilivyo nyingine, naamini haitafanya kazi kwa kuwa mfumo wa uendeshaji wa chama chenu cha magamba ni mbovu na ndio tatizo.