Kiba hana office unataka amutembelee pale michikichiniNi suala la kutoa elimu tu kuwa kumpa bendera Diamond kulikuwa ni jambo jema kabisa kwa sanaa ya muziki wa Tanzania. Anapoingizia ishu ya ushindan wa Diamond na Kiba anaanza kuvua viatu wa uwaziri na kuvaa vya ushabiki.
Kwa kauli yake nimegundua yuko timu Mond na anaonyesha upendeleo wa wazi. Jiulizeni ni lini aliwahi kwenda kwa Kiba kujionea kazi zake za muziki?
Tatizo ni kumpa kazi ya uwaziri mtu aliyekuwa Katibu mwenezi wa chama. Kazi ya katibu mwenezi ni kuona rangi mbili tu-rangi ya watawala na ya wapinzani. Kama huna rangi ya chama tawala basi wewe ni wa upinzani. Kama unaponda Diamond kupewa bendera basi wewe timu Kiba. Hajui wengine wanakosoa kwa sababu hawajazoea tu, ndo tunafanya mara ya kwanza. Hawa wanahitaji kuelimishwa kwamba Diamond ana nafasi nzuri zaid ya kuutambulisha muziki wa Tanzania kwa Africa nzima maana Misri, Algeria, Tunisia na wengineo watakuwa wanafuatilia na njia rahisi kutambulisha nchi kwenye tamasha ni bendera.