Mkwawa
JF-Expert Member
- Jun 8, 2011
- 1,334
- 1,464
Ukiwa kijana uliyeonyesha uwezo wa kuwa mwanasiasa. Ulikubali kujitoa mhanga kutetea jengo la umoja wa vijana lisiuzwe kwa ulaghai kwa nguvu ya mafisadi. Hapo ndipo ulipoanza kuonyesha kuwa unaweza kupambana na nguvu kubwa ndani ya chama chako. Umeridhi siasa kutoka kwa mzazi mwadilifu, mnyenyekevu na mwenye maadili, alichukia rushwa na kuonea watu, alichukia kugandamiza masikini na kuwatenga. namkumbuka mzee Moses Mnauye kijijini kwetu alicheza na watoto na aliwaacha wachezee kinananda chake ishara ya upendo.
Kijana Nape najua unamatumaini makubwa sana ya kisiasa na kukwea ngazi kufikia ubunge, waziri hata juu zaidi. Ila kaka yangu ulipofikia sasa inabidi utumie busara na hekima kuamua.
Ukiwa tu umeteuliwa katibu mwenezi wa CCM ulikuja na kauli mbiu ya kuvua watu magamba na uliwataja kwa majina Rostam Azizi, Chenge na E lowasa. ulienda mbali zaidi na kusema wana siku tisini lazima wajivue gamba au chama kitawavua magamba. Mheshimiwa siku tisini zilikwisha na hakuna kinachojulika ziadi. kauli hizi zilipingwa na Mukama mbele ya vyombo vya habari kuwa hakuna swala la siku tisini. Wakati anaachia ubunge wa igunga Rostom azizi alisema anaachana na siasa uchwara ambazo kwa tafsiri yangu wewe ndiye unaziendesha.
Kikao cha kamti kilichokaa juzi juzi inasemakana kilikupiga marufuku usihudhurie kampeni za Igunga kitu ambacho kwa tafsiri yangu nina amini kwani mpaka sasa hujahudhuria kampeni yeyote Igunga hata ile ya ufunguzi ikizingatiwe hapo ndio pangekuwa mahala pako. Hilo haliajinishtua katu.
Mshtuko wango ni pale ninapoona ulikazwa usiende Igunga ili gamba mlilokuwa mnalipigia kelele liweze kuchukua nafasi yenu nyite kuwasaidia kushinda uchaguzi mliosema mnafukuza mafisadi wanaoharibu taswira ya chama mbele ya jamii. Je ni jamii ipi tena wakati hao hao ndio mnawahitaji mnapoona hamyawezi?????
Ndugu Nape ulisema chama ni zaidi ya mtu na mtu hawezi kuwa maarafu kuliko chama. je bado unaona vita vya kutoa magamba vipo? Je si kweli kwamba kamati kuu ilimwomba Rostam Aziz kusaidia kampeni za Igunga? na kama ni kweli nini yeye atapata ? ameahidiwa nini kutoka kamati kuu au Rostam alijipeleka mwenyewe Igunga??? Nape huoni wenzako wamekusaliti kwa kiwango kikubwa sana, huoni umeachwa kama yatima nyikani, huoni utu wako umedhalilishwa kwa kutetea wasiyoamini wala labda kututma kutoka mioyoni mwao, huoni unatumiwa kama dodoki na mwisho utatupwa jalalani???
Nape Nnauye kama mimi ningekuwa wewe ningejiuzulu wadhifa wangu huo kwani ni kazi ya kinafiki na isiyotekelezeka, kupewa maagizo ya kinafiki na majukumu ya uongo ni unafiki mkubwa sana.
Kama kweli wewe ni mwana mapinduzi pima yote yanayotokea, kama hayo ndiyo yanatoa picha ya Nape Nnauye endelea ila kama una utu na unasimamia unayoongea ni muda wa kujiuzulu.
najua siasa ni kazi na mshahara na marupu rupu ndio yanayoangamiza dhamiri zetu za ndani, wamekukamata pazuri. wamejua huna jinsi ya kupata mkate wamekutumia kama dodoki sasa wanakucheka ujinga. Leo wanamhitaji Rostam kuliko wewe kesho watamhitaji Chenge Mwanza kuliko wewe kesho watamhitaji E lowasa Arusha kuliko wewe kesho kutwa watamhitaji Manji kuliko wewe, wewe utangojea kutumwa tu pale wasipotaka kuharibu urafiki wao. Hapo ndipo elimu na uelewa binafsi unapohitajika unapigania nini??
Mambo kama haya ndio chanzo cha vijana wengi makini kuamua kuachana na CCM na kujiunga na vyama vya upinzani. Ni heri kufa masikini na kulinda utu na uelewa wangu kuliko kudhalilisha utu wangu kwa kibaba cha mchele.
Kwa kumpandisha Gamba ambalo mnalia nalo na kukushusha wewe huhitaji miujiza mingine zaidi ya kujua unatumika kama kifuu.
Akili ni nyele kila mtu ana zake. Ukistaabu ya musa utaona ya firauni. Muungwana ni vitendo.
Viongozi makini hutoa maamuzi makini
Kijana Nape najua unamatumaini makubwa sana ya kisiasa na kukwea ngazi kufikia ubunge, waziri hata juu zaidi. Ila kaka yangu ulipofikia sasa inabidi utumie busara na hekima kuamua.
Ukiwa tu umeteuliwa katibu mwenezi wa CCM ulikuja na kauli mbiu ya kuvua watu magamba na uliwataja kwa majina Rostam Azizi, Chenge na E lowasa. ulienda mbali zaidi na kusema wana siku tisini lazima wajivue gamba au chama kitawavua magamba. Mheshimiwa siku tisini zilikwisha na hakuna kinachojulika ziadi. kauli hizi zilipingwa na Mukama mbele ya vyombo vya habari kuwa hakuna swala la siku tisini. Wakati anaachia ubunge wa igunga Rostom azizi alisema anaachana na siasa uchwara ambazo kwa tafsiri yangu wewe ndiye unaziendesha.
Kikao cha kamti kilichokaa juzi juzi inasemakana kilikupiga marufuku usihudhurie kampeni za Igunga kitu ambacho kwa tafsiri yangu nina amini kwani mpaka sasa hujahudhuria kampeni yeyote Igunga hata ile ya ufunguzi ikizingatiwe hapo ndio pangekuwa mahala pako. Hilo haliajinishtua katu.
Mshtuko wango ni pale ninapoona ulikazwa usiende Igunga ili gamba mlilokuwa mnalipigia kelele liweze kuchukua nafasi yenu nyite kuwasaidia kushinda uchaguzi mliosema mnafukuza mafisadi wanaoharibu taswira ya chama mbele ya jamii. Je ni jamii ipi tena wakati hao hao ndio mnawahitaji mnapoona hamyawezi?????
Ndugu Nape ulisema chama ni zaidi ya mtu na mtu hawezi kuwa maarafu kuliko chama. je bado unaona vita vya kutoa magamba vipo? Je si kweli kwamba kamati kuu ilimwomba Rostam Aziz kusaidia kampeni za Igunga? na kama ni kweli nini yeye atapata ? ameahidiwa nini kutoka kamati kuu au Rostam alijipeleka mwenyewe Igunga??? Nape huoni wenzako wamekusaliti kwa kiwango kikubwa sana, huoni umeachwa kama yatima nyikani, huoni utu wako umedhalilishwa kwa kutetea wasiyoamini wala labda kututma kutoka mioyoni mwao, huoni unatumiwa kama dodoki na mwisho utatupwa jalalani???
Nape Nnauye kama mimi ningekuwa wewe ningejiuzulu wadhifa wangu huo kwani ni kazi ya kinafiki na isiyotekelezeka, kupewa maagizo ya kinafiki na majukumu ya uongo ni unafiki mkubwa sana.
Kama kweli wewe ni mwana mapinduzi pima yote yanayotokea, kama hayo ndiyo yanatoa picha ya Nape Nnauye endelea ila kama una utu na unasimamia unayoongea ni muda wa kujiuzulu.
najua siasa ni kazi na mshahara na marupu rupu ndio yanayoangamiza dhamiri zetu za ndani, wamekukamata pazuri. wamejua huna jinsi ya kupata mkate wamekutumia kama dodoki sasa wanakucheka ujinga. Leo wanamhitaji Rostam kuliko wewe kesho watamhitaji Chenge Mwanza kuliko wewe kesho watamhitaji E lowasa Arusha kuliko wewe kesho kutwa watamhitaji Manji kuliko wewe, wewe utangojea kutumwa tu pale wasipotaka kuharibu urafiki wao. Hapo ndipo elimu na uelewa binafsi unapohitajika unapigania nini??
Mambo kama haya ndio chanzo cha vijana wengi makini kuamua kuachana na CCM na kujiunga na vyama vya upinzani. Ni heri kufa masikini na kulinda utu na uelewa wangu kuliko kudhalilisha utu wangu kwa kibaba cha mchele.
Kwa kumpandisha Gamba ambalo mnalia nalo na kukushusha wewe huhitaji miujiza mingine zaidi ya kujua unatumika kama kifuu.
Akili ni nyele kila mtu ana zake. Ukistaabu ya musa utaona ya firauni. Muungwana ni vitendo.
Viongozi makini hutoa maamuzi makini