Nape Nnauye, Julius Mtatiro na Dr. Shoo Live on Azam tv

idawa

JF-Expert Member
Jan 20, 2012
25,284
38,312
Karibu tuwafutulie hawa wanasiasa vijana na Mwandishi mkongwe juu ya mstakabali wa siasa za Tanzania.

Nappe..
Akizungumzia kuhusu hama hama ya viongozi kwenye vyama amesema yeye sio muumini wa kuhama hama vyama .

Anasema kuna haja hii hama hama iangaliwe upya isiwe kirahisi rahisi.

Nappe anasema yeye hawezi kuhama chama eti kwa sababu ametofautiana na mkubwa fulani.

Nappe anasema kuna haja ya kuchora mstari kutenganisha Taasisi ya Urais na Uenyekiti wa Chama kwa sababu limekuwa likileta migongano mara kwa mara kwenye utendaji wa kazi.

Nappe anasema kuhama hama vyama hakuna tija yoyote kwa Taifa.

Mtatiro.....Bado analaani serikali kuzuia shughuli za kisiasa..anasema jambo ambalo lipo kikatiba hakuna wa kulipinga hata Rais aweje...

Kuhusu hama hama Mtatiro anasema hawezi kuhama CUF kwa sababu ya Lipumba sababu yeye hakujiunga kumfuata mtu.

Akizungumzia wabunge wanaohama anasema wengi ni wale wanaopewa rushwa ama kununuliwa.

Anasema serikali ya Magufuli huko nje inasifiwa kwa kupambana na rushwa Lakini ndani ya nchi hali ni tofauti....na mbaya zaidi serikali hii inachagua wa rushwa za kushughulika nazo....

Mtatiro...anasema upinzani lazima ujenge vijana wake na sio kutegemea wanasiasa wanaohama vyama..

Anasema ni kosa vyama vya upinzani kuwapokea wanachama wa vyama vingine na kuwapa nafasi za juu bila kuwachunguza.

Matokeo yake ndio hao wanaohama hama .

Nappe...anasema ili vyama vya upinzani viwe imara ni lazima wawekeze kwa vijana.

Anasema yeye ni mfano ccm imewekeza toka akiwa mdogo amekulia kwenye itikadi ya chama.

Hiyo hawezi kuhama kwa haya mawimbi madogo madogo yanayomtokea..

Dr.Shoo anahoji wabunge wanaohama vyama na kuacha mamilioni ya ubunge je ni kwa mapenzi yao binafsi.

Anahoji ccm kama kweli wanaowanunua hao watu wanafaidika nini kwa maslahi ya nani.

Anasema chama chochote hakiwezi kushika dola kama hakijawekeza kwenye mashina...

Upinzani lazima uwekeze mashinani kuliko ndio iliko dola.
 
Mtatiro...anasema upinzani lazima ujenge vijana wake na sio kutegemea wanasiasa wanaohama vyama..

Anasema ni kosa vyama vya upinzani kuwapokea wanachama wa vyama vingine na kuwapa nafasi za juu bila kuwachunguza.

Matokeo yake ndio hao wanaohama hama .

Huyo Mtatiro alikuwa ukawa, nafasi urais alipewa Lowassa alikuwa mpinzani? Alichukua hatua gani kupinga hilo? Sisi tulipinga Lowassa kupewa nafasi ile na ukawa kupitia cdm na hadi sasa tunapinga. Iweje yeye aanze kuamka sasa?
 
Huyo Mtatiro alikuwa ukawa, nafasi urais alipewa Lowassa alikuwa mpinzani? Alichukua hatua gani kupinga hilo? Sisi tulipinga Lowassa kupewa nafasi ile na ukawa kupitia cdm na hadi sasa tunapinga. Iweje yeye aanze kuamka sasa?
mkuu watu hujifunza kwa makosa
 
Nappe...anasema ili vyama vya upinzani viwe imara ni lazima wawekeze kwa vijana.

Anasema yeye ni mfano ccm imewekeza toka akiwa mdogo amekulia kwenye itikadi ya chama.

Hiyo hawezi kuhama kwa haya mawimbi madogo madogo yanayomtokea..

Hili wazo lake ni zuri, ila linategemea na utashi binafsi wa muhusika.
 
Nappe.... akizungumzia kuhusu uchaguzi wa kata 43 anawalaumu moja kwa viongozi wa upinzani kuwa kule chini kwenye mashina hakuna upinzani wa kueleweka..hapa anawalaumu viongozi wa upinzani.

Anasema ili ccm iwe imara inabidi kuwe na upinzani madhubuti.... .Analaumu upinzani kususia zile kata tatu akisema ni uamuzi wa ovyo sana... Anasema ilikuwa nafasi ya kujifunza na kujitathamini...
 
1d2082459e23db167c91c8294a371b53.jpg
***** Sana
Nape hana mvuto tena.
 
Nappe anasema kuna haja ya kuchora mstari kutenganisha Taasisi ya Urais na Uenyekiti wa Chama kwa sababu limekuwa likileta migongano mara kwa mara kwenye utendaji wa kazi.
Nape si awe wazi tu aseme mwenyekiti wa sasa hajui wapi awe mwenyekiti na wapi awe rais?
 
Mtatiro....anasema dhambi ni dhambi...anasema hakuna namna yoyote ya kutetea uovu.

Anasema kwenye uchaguzi wa kata 43 hakukuwa na uchaguzi....anasema ccm ya zamani ilikuwa inaiba kura kisayansi lakini sasa hivi wanaiba waziwazi....

Anasema serikali ilisimamia kwa karibu kuhusu wizi wa kura ili serikali ionekane inakubalika.

Wasimamizi wa uchaguzi walitishwa hadharani na viongozi wa serikali kuwa lazima wawatangaze wagombea wa ccm.
 
Nappe.... akizungumzia kuhusu uchaguzi wa kata 43 anawalaumu moja kwa viongozi wa upinzani kuwa kule chini kwenye mashina hakuna upinzani wa kueleweka..hapa anawalaumu viongozi wa upinzani.

Anasema ili ccm iwe imara inabidi kuwe na upinzani madhubuti.... .Analaumu upinzani kususia zile kata tatu akisema ni uamuzi wa ovyo sana... Anasema ilikuwa nafasi ya kujifunza na kujitathamini...
Ule ususiaji hauna impact yoyote ....wanazidi kujididimiza tu ...platform za kuchambua facts zinakuja then wanazikimbia ....nawashangaa hata wanavyomkimbia Msando kwa visingizio vya aibu sana .....sijui nini kinaendelea huko Chadema ....
 
Dr.Shoo anasema kama kweli upinzani unasema unaonewa na wanaushahidi wa juu kuibiwa kura na na kunyanyaswa kwa nini wasiende mahakamani na ushahidi huo.
 
Back
Top Bottom