Allen Kilewella
JF-Expert Member
- Sep 30, 2011
- 18,300
- 33,913
Mkono mtupu haulambwi ndugu yangu!!Nilimuonea huruma sana Nape kipindi kile, kakini alipokuwa waziri undugu ulirudi alikuwa sibling kabisa kaka Nape 😂
Mkono mtupu haulambwi ndugu yangu!!Nilimuonea huruma sana Nape kipindi kile, kakini alipokuwa waziri undugu ulirudi alikuwa sibling kabisa kaka Nape 😂
Kwani amekosea wapi? Kama hujui jambo bora ukae kimya maana una jitia aibu bure!Mahaba hajawahi kumuacha mtu salama.
Kavurugwa huyo na mahaba kwa Tundulisu Msaliti, ndiyomaana anahamishia mihemuko yake ya siasa uchwara za mitandaoni hadi kwa Nape.
Sent using Jamii Forums mobile app
Kama ni kweli anatakiwa afukuzwe kabisa kwenye chama
Ardhi ni mali ya Jamhuri ya muungano,sheria ipo wazi ukimilikishwa unatakiwa kuendeleza ndani ya muda fulani
Watu wamepewa malaki ya ekari,ili walime na kutoa ajira,matokeo yake wamekopa benki za nje huku wameacha mapori na wananchi hawaruhusiwi kulima
Hata Sumaye alinyang'anywa mashamba Mabwepande na Morogoro kwa hila na husda tu. Chuki na visasi kuna siku vitakuja kumla jiwe mwenyewe na washirika wake.Mo alinyang'anywa mashamba huko Tanga
This is very sad!
Nani aliwapa wawekezaji hewa hayo mashamba!? Ni chechemee au Nape?? Kuweni siriasi banaKwa hiyo kawa mtetezi wa wawekezaji hewa?
Nape anaikosi na amb yanayohusu Ripoti.Mhe Nape amejiuzulu uenyekiti wa kamati ya mali asili baada ya kuwekwa kitimoto na chama. Habari zinasema ni baada ya kukata kuondoa taarifa ya uchukuaji wa mashamba ya wawekezaji kinyume na sheria.
--------------
Mbunge wa Mtama, Nape Nnauye amejiuzulu Uenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maliasili na Utalii. Kujiuzulu kwake, kunatokana kile kinachoitwa, “Kugoma kuondoa taarifa ya uchukuaji wa mashamba ya wawekezaji, kinyume na sheria.”
Kwa mujibu wa taarifa kutoka ndani ya Kamati ya Bunge ya Maliasili na Utalii zinasema, Nape amejiuzulu baada ya kutofautiana na serikali kuhusu ripoti ya Kamati yake.
“Nape alitaka ripoti ya Kamati ya Bunge ya Maliasili na Utalii, iliombe Bunge kuundwa kwa Kamati Teule ya Bunge ili kuchunguza utaratibu uliotumika wa kufuta mashamba ya watu,” ameeleza mjumbe mmoja wa kamati hiyo.
Ameongeza, “Serikali haitaki kuundwa kwa Kamati hiyo. Hivyo imeamua kuitumia Kamati ya wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), kumlazimisha Nape kujiuzulu.”
Taarifa kutoka ndani ya Kamati ya Bunge ya Maliasili na Utalii zinasema, tayari Nape amemuandikia barua rasmi ya Spika kumjulisha kujiuzulu kwake.
Nape alihuhutubia waandishi wa habari leo akiwa chini ya vyombo vya usalama na kutetea msimamo wake.
Kupatikana kwa taarifa hizi kumekuja siku moja kabla ya Kamati yake kuwasilisha ripoti yake na zinaeleza kuwa Kamati hiyo ilikuwa inaleta mapendekezo ya kuundwa kwa Kamati Teule, jambo ambalo lilihofiwa kuwaumbua baadhi ya wakubwa.
Machi mwaka 2017, Nape aling’olewa kwenye nafasi ya uwaziri wa habari, utamaduni, Sanaa na michezo.
Mbunge huyo wa Mtama mkoani Lindi, alivuliwa wadhifa wake siku moja baada ya kupokea ripoti ya Kamati ya uchunguzi juu ya tukio uvamizi wa kituo cha televisheni cha Clouds kwa kutumia silaha uliofanywa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda.
Ripoti ya kamati aliyoiunda Nape kuchunguza tukio hilo, ilithibitisha kuwa Makonda alivamia kituo hicho majira ya saa 5 usiku wa Ijumaa ya tarehe 17 Machi 2017 na alifanya uvamizi huo akitumia askari wenye silaha. Nape aliahidi kulifikisha ripoti yake kwa mamlaka ya juu yake. Haijajulikana mpaka sasa, ripoti hiyo amekabidhiwa nani.
Nape ambaye aliwahi kuwa Katibu wa Idara ya Uenezi ya CCM, amesema atapata nafasi nzuri ya kutumikia wananchi wa jimboni wake baada ya kuachia nafasi hii.
HAWA GHASIA MWAKA WA JANA ALIJIUZURU KAMA MWENYEKITI KAMATI YA BAJETITanzania yngu
We unadhani ulikuwa uamuzi wa nape ule? Mbona sasa halioneshwi live baada ya nape kutokaNape hata ajidai Mwema namna gani, simsamehi kosa la kukataa Bunge kwenda live kwa sababu za kijinga sana!
Watanzania ni watu wa ajabu sana, rahis sana kuhadaiwa na wanasiasa uchwara, eti leo kweli Mwanahabari Huru anamuona Nape mtu mwema??!
mshahara wa goli la mkono..... inaitwa karma.Mhe Nape amejiuzulu uenyekiti wa kamati ya mali asili baada ya kuwekwa kitimoto na chama. Habari zinasema ni baada ya kukata kuondoa taarifa ya uchukuaji wa mashamba ya wawekezaji kinyume na sheria.
--------------
Mbunge wa Mtama, Nape Nnauye amejiuzulu Uenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maliasili na Utalii. Kujiuzulu kwake, kunatokana kile kinachoitwa, “Kugoma kuondoa taarifa ya uchukuaji wa mashamba ya wawekezaji, kinyume na sheria.”
Kwa mujibu wa taarifa kutoka ndani ya Kamati ya Bunge ya Maliasili na Utalii zinasema, Nape amejiuzulu baada ya kutofautiana na serikali kuhusu ripoti ya Kamati yake.
“Nape alitaka ripoti ya Kamati ya Bunge ya Maliasili na Utalii, iliombe Bunge kuundwa kwa Kamati Teule ya Bunge ili kuchunguza utaratibu uliotumika wa kufuta mashamba ya watu,” ameeleza mjumbe mmoja wa kamati hiyo.
Ameongeza, “Serikali haitaki kuundwa kwa Kamati hiyo. Hivyo imeamua kuitumia Kamati ya wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), kumlazimisha Nape kujiuzulu.”
Taarifa kutoka ndani ya Kamati ya Bunge ya Maliasili na Utalii zinasema, tayari Nape amemuandikia barua rasmi ya Spika kumjulisha kujiuzulu kwake.
Nape alihuhutubia waandishi wa habari leo akiwa chini ya vyombo vya usalama na kutetea msimamo wake.
Kupatikana kwa taarifa hizi kumekuja siku moja kabla ya Kamati yake kuwasilisha ripoti yake na zinaeleza kuwa Kamati hiyo ilikuwa inaleta mapendekezo ya kuundwa kwa Kamati Teule, jambo ambalo lilihofiwa kuwaumbua baadhi ya wakubwa.
Machi mwaka 2017, Nape aling’olewa kwenye nafasi ya uwaziri wa habari, utamaduni, Sanaa na michezo.
Mbunge huyo wa Mtama mkoani Lindi, alivuliwa wadhifa wake siku moja baada ya kupokea ripoti ya Kamati ya uchunguzi juu ya tukio uvamizi wa kituo cha televisheni cha Clouds kwa kutumia silaha uliofanywa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda.
Ripoti ya kamati aliyoiunda Nape kuchunguza tukio hilo, ilithibitisha kuwa Makonda alivamia kituo hicho majira ya saa 5 usiku wa Ijumaa ya tarehe 17 Machi 2017 na alifanya uvamizi huo akitumia askari wenye silaha. Nape aliahidi kulifikisha ripoti yake kwa mamlaka ya juu yake. Haijajulikana mpaka sasa, ripoti hiyo amekabidhiwa nani.
Nape ambaye aliwahi kuwa Katibu wa Idara ya Uenezi ya CCM, amesema atapata nafasi nzuri ya kutumikia wananchi wa jimboni wake baada ya kuachia nafasi hii.
Acha mkwara wewe atamaliza zaidi ya kumi wewe unajua utamaliza dakika ngapi?
Usipojua kitu kaa kaa kimya hutaitwa mpumbavu!