Nape, Ndoto zako hizi ziliishia wapi?

babalao 2

JF-Expert Member
Apr 6, 2012
5,399
3,243
KATIBU wa NEC Itikadi na Uenezi-CCM Nape Nnauye amesema, ndoto aliyokuwa nayo ya kazi ambayo angependa kufanya alipokuwa hajawa mwanasiasa ni kuwa askari ambaye rubani wa ndege za kijeshi.

Amesema maandalizi ya kutimiza ndoto hiyo alikuwa ameianza kwa kuweka kipaumbele kwenye masomo ya fani hiyo ikiwemo fizikia na jiografia wakati anamaliza kidato cha nne.

Nape mwenye umri wa miaka 37, sawa na umri wa CCM, amesema hayo leo alasiri alipododoswa na watangazaji kwenye kipindi cha 'Power Jam' katika Kituo cha Radio cha East Africa, kilichopo Mikocheni jijini Dar es Salaam, ambao walitaka awaambie wasikilizaji ni kazi ya fani ipi aliyokuwa akiipenda kuifanya asingekuwa mwanasiasa.

"Kazi niliyopienda zaidi ni kuwa Mwanajeshi, tena Mwanajeshi mwenyewe ambaye ni rubani wa kurusha ndege za kijeshi...Na hata nilipokuwa namaliza kidacho cha nne, nilikuwa nimejiandaa zaidi katika masomo ya fani hiyo ikiwemo fizikia na jiografia", alisema, Nape.

ANAVYOJITOFAUTISHA NA WANASIASA WALIOPO VYAMA VYA UPINZANI
Akizungumzia tofauti iliyopo kati yake na wanasiasa walipo kwenye vyama vya upinzani kama walivyotaka kujua watangazaji hao, Nape alisema, tofauti kubwa iliyopo ni kwamba yeye ni mwanasiasa ndiyo sababu yupo kwenye chama cha CCM ambacho ni cha siasa lakini wapinzani siyo wanasiasa bali ni wana harakati kwa sababu wapo kwenye vyama vya harakati siyo vya siasa.

"Unajua mimi ni mwanasiasa ndiyo sababu nipo kwenye Chama Cha Mapinduzi ambacho ni chama cha siasa, lakini hao wengine ni wana harakati ndiyo sababu wapo kwenye vyama vya harakati. Na hii ndiyo tofauti kubwa ya mimi na wao", alisema Nape.

Nape jipange ili urudishe imani kwa wana CCM wakupitishe Ubungo kura za maoni ili badae uje Umng'oe Mnyika 2015.

Ikishindikana Gandana na Kinana akuachie Mikoba Ya Ukatibu Mkuu maana anakupigisha zoezi.

NAOMBA KUTHIBITISHIWA, ETI:-
MNYIKA VS NAPE, FORM FOUR RESULTS
NAPE NNAUYE
DIV IV-29
KISW D, HIST D, GEOG D, ENG F, B/MATH F, BIOL D,
CHEM D, PHY D, CIV F

JOHN MNYIKA
DIV I-7
PHY A, CHEM A, BIOL A, CIV A, ENGL A, GEOG A, HIST
A, B/MATH A, KISW A, B/KNOW A
 
For one thing imekuwa afadhali hiyo hadithi ya kuwa Mwanajeshi na rubani, iliishia usingizini. Jeshi lingekuwa na hasara sana kuwa na mtu kama Nape. By the way nnaweza kubet kuwa interview angefeli. Na hata angepitishwa depo ingemshinda. Kule waimba taarabu hawamalizi.
 
For one thing imekuwa afadhali hiyo hadithi ya kuwa Mwanajeshi na rubani, iliishia usingizini. Jeshi lingekuwa na hasara sana kuwa na mtu kama Nape. By the way nnaweza kubet kuwa interview angefeli. Na hata angepitishwa depo ingemshinda. Kule waimba taarabu hawamalizi.

Mkuu unafikiri ni ufaulu hafifu ndo ulizima ndoto zake nini?
 
For one thing imekuwa afadhali hiyo hadithi ya kuwa Mwanajeshi na rubani, iliishia usingizini. Jeshi lingekuwa na hasara sana kuwa na mtu kama Nape. By the way nnaweza kubet kuwa interview angefeli. Na hata angepitishwa depo ingemshinda. Kule waimba taarabu hawamalizi.
Mbona na wewe umeandika mipasho sasa?
 
Mkuu unafikiri ni ufaulu hafifu ndo ulizima ndoto zake nini?

Ufaulu hasa siyo tatizo. Tatizo ni kutokuwa na msimamo wa kujua unataka nini na nini ni sahihi. Na bahati mbaya hizo ndizo tabia zinazomtofautisha mwanaume na wengine waliobaki. Na ni hizo sifa, ambazo mpaka kesho Nape anazikosa. Na mpaka atakapoanza kuonyesha dalili za kuwa mwanaume, nadhani ndiyo tunatakiwa kuanza kumuelewa.
 
Mbona na wewe umeandika mipasho sasa?

Nadhani kuna tofauti ya mipasho na ukweli. In case hujanielewa angalia umri wa Nape, halafu husianisha na kauli na matendo yake. Halafu niambie kama kusema ukweli ni mipasho.
 
Nadhani kuna tofauti ya mipasho na ukweli. In case hujanielewa angalia umri wa Nape, halafu husianisha na kauli na matendo yake. Halafu niambie kama kusema ukweli ni mipasho.

Ubongo na mwili jumlisha umri
 


Nape jipange ili urudishe imani kwa wana CCM wakupitishe Ubungo kura za maoni ili badae uje Umng'oe Mnyika 2015.

Ikishindikana Gandana na Kinana akuachie Mikoba Ya Ukatibu Mkuu maana anakupigisha zoezi.

Ingekuwa jeshi la mkoloni sawa lakini jeshi la sasa hivi linahitaji ufaulu mzuri pamoja na busara na wala siyo mtulinga tu.
Kama angefanikiwa kuingia jeshini basi kupanda cheo ingekuwa kazi. Nafasi aliyonayo sasa ni post safi sana kwake kwa uwezo wake, ni nafasi ya kupiga debe tu na wala huhitaji kufikiri hata kidogo.Kimsingi amshukuru Mungu kwa nafasi aliyonayo maana nikiifananisha na jeshini ni sawa na brigedia generali cheo ambacho kukifikia lazima mtu awe na uwezo mkubwa kusoma na kuwa mbunifu na hasa pale ukipewa brigedi kwenda vitani
 
Hayo masomo yenyewe kama kweli alikuwa serious hiyo Geograpy na Physics alipata alama gani za ufaulu? Na pia ina maana siasa alianza alipokuwa anasoma olevel
 
For one thing imekuwa afadhali hiyo hadithi ya kuwa Mwanajeshi na rubani, iliishia usingizini. Jeshi lingekuwa na hasara sana kuwa na mtu kama Nape. By the way nnaweza kubet kuwa interview angefeli. Na hata angepitishwa depo ingemshinda. Kule waimba taarabu hawamalizi.

Yaani,angeweza kupokea fungu na kuwatosa wenzake.Yaani afadhali hakuwa.
 
Hayo masomo yenyewe kama kweli alikuwa serious hiyo Geograpy na Physics alipata alama gani za ufaulu? Na pia ina maana siasa alianza alipokuwa anasoma olevel

Alijitahid akapata D flat ila math. Alipiga F
 
hayo masomo yenyewe kama kweli alikuwa serious hiyo geograpy na physics alipata alama gani za ufaulu? Na pia ina maana siasa alianza alipokuwa anasoma olevel

naomba kuthibitishiwa, eti:-
mnyika vs nape, form four results

nape nnauye
div iv-29
kisw d, hist d, geog d, eng f, b/math f, biol d,
chem d, phy d, civ f

john mnyika
div i-7
phy a, chem a, biol a, civ a, engl a, geog a, hist
a, b/math a, kisw a, b/know a
 
Yaani,angeweza kupokea fungu na kuwatosa wenzake.Yaani afadhali hakuwa.

Kupokea fungu wala isingekuwa tatizo. Wasiwasi wa hizo ndege kupotelea kusikojulikana, na kuwasaliti wenzake kwa kuuza siri za jeshi. Nna maana sioni ni vipi mtu anaweza kuwasaliti wananchi halafu huyohuyo awe kamanda wa kutumainiwa jeshini!
 
Kupokea fungu wala isingekuwa tatizo. Wasiwasi wa hizo ndege kupotelea kusikojulikana, na kuwasaliti wenzake kwa kuuza siri za jeshi. Nna maana sioni ni vipi mtu anaweza kuwasaliti wananchi halafu huyohuyo awe kamanda wa kutumainiwa jeshini!

Tatizo hajui nini anahitaji kukifanya.Alianza na magamba ikashindikana,sasa hivi ukimsikiliza kuanzia mwanza wa hotuba ni wapinzani na hadithi za UKAWA.
 
Kipawa alichopewa huyu jamaa ni Uijiristi, huko kwenye siasa ni mapito tu.
 
naomba kuthibitishiwa, eti:-
mnyika vs nape, form four results

nape nnauye
div iv-29
kisw d, hist d, geog d, eng f, b/math f, biol d,
chem d, phy d, civ f

john mnyika
div i-7
phy a, chem a, biol a, civ a, engl a, geog a, hist
a, b/math a, kisw a, b/know a

Ni ukweli kabisa,sasa huyo Nape na ndoto zake za kuwa rubani wakati hata hayo masomo yenyewe ilikuwa mtihani sana
 
Mkuu Fuso hicho Kipawa Cha Uinjilisti si ndo Wapo Mzee Wa Upako, Kakobe Mama Lwakatare, Kilaini na Wanapiga maisha Vizuri tu.
Askovu Nnauye inaleta picha kiasi.
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom