Nape naye ang'atuka ugombea NEC, adai anajikita kusimamia uchaguzi (HAKUNA UTHIBITISHO)

Status
Not open for further replies.
huyu muongo atakuwa kaambiwa aiondoe maana watamkata jina lake ..hahaaa Nepi bana
 
Mh! lipo jambo nyuma ya pazia, sio bure.

Si jambo, yapo mambo kadhaa. Kwanza, anategesha. Anajua kuwa mwezi novemba utafanyika uchaguzi wa mwenyekiti na ni dhahiri kuwa secretariat itavunjwa na kuundwa upya, anategesha akiamini kuwa atapata tu Cheops hapo.
Lakini pia uchaguzi wa mwaka huu ndani ya CCM umekuwa na ushindani Mlaki ambaonhaujawahi kuonekana miaka ya nyuma. Wagombea wamekuwa wengi, malalamiko mayo ni Mengi kiasi kuwa hata kamati ya maadili ambayo ilikuwa ikae kwa siku moja Leo ni siku ya nne bado haina Aliza kazi hapa Dodoma.
Baada ya kurudishs utaratibu wa kugombea kupitia wilaya, Nape amejikuta Hana base ambayo angeweza kugombea na kuwa na uhakikaa wa kushindana nakuhsinda hivyo ilikuwa ninhatarisana kwake na muafaka Ali wake imp angegombea na kushindwa, hata uteuzinwa novemba ungeruka mbawa
 
Katiba ya CCM inampa Mwenyekiti nafasi kadhaa( kumi nadhani ) kuteua wajumbe wa NEC. Mwenyekiti atakayechaguliwa anajulikana na hata wajumbe atakaowateua kuingia NEC, CC na sekretariet haihitaji akili kuuubwa kuwabaini. Mmojawapo ni huyu Nape.
 
Hivi mnavyosema kugombea miaka kumi mfululizo na kushinda mnamaanisha nini? yaani kila mwaka anagombea ujumbe wa NEC na kuhinda kwa miak kumi mfululizo? maana hata kwenye thread ya kujiuzulu kwa Kinana imesemwa hivyohiyo "kugombea kwa miaka 25 mfululizo"
Nape ameamua kutogombea ujumbe wa NEC kwenye uchaguzi wa ndani ya chama hicho mwaka huu, baada ya kugombea kwa miaka kumi mfululizo na kushinda, sasa ameamua kutogombea ILI APATE MUDA WA KUSIMAMIA UCHAGUZI HUO VIZURI NDANI YA CHAMA..........." si rahisi kuwa refa na mchezaji kwa wakati mmoja, ukatenda haki ipasavyo, hivyo nimeona bora kutogombea ili nipate muda wa kutosha kusimamia mchakato, ili haki itendeke zaidi" alisema Nape.


Source. Habari Leo
 
Hivi asipokuwa mjumbe wa NEC nini hasara na faida yake?
Ni lazima awe M-NEC ili aweze kuendelea na nafasi hii aliyonayo ambayo kwa maoni yangu ameimudu sana. Sidhani kama JK halioni hili akashindwa kumteua kuwa MNEC kupitia zile nafasi za Mwenyekiti ambazo ni mahsusi kwa ajili ya wasaidizi wake wa karibu ndani ya CCM.
 
Nape ameamua kutogombea ujumbe wa NEC kwenye uchaguzi wa ndani ya chama hicho mwaka huu, baada ya kugombea kwa miaka kumi mfululizo na kushinda, sasa ameamua kutogombea ILI APATE MUDA WA KUSIMAMIA UCHAGUZI HUO VIZURI NDANI YA CHAMA..........." si rahisi kuwa refa na mchezaji kwa wakati mmoja, ukatenda haki ipasavyo, hivyo nimeona bora kutogombea ili nipate muda wa kutosha kusimamia mchakato, ili haki itendeke zaidi" alisema Nape.


Source. Habari Leo

Nape hana jimbo la kugombea. Asiwadanganye. Alitaka kugombea ujumbe wa NEC kupitia wilaya ya Kinondoni – akajipima akaona hawezi kupenya. Hapa yupo Londa na mwanachama mmoja yule mwizi wa TRA.

Akataka kwenda Masasi, nako akakumbana na kizingiti kutoka kwa familia ya Mosesi Nnauye ambaye yeye anajiita mwanawe. Wale watoto wake na baadhi ya ndugu wa NNauye wamegoma kumtambua. Wanasema Nape siyo mtoto wao, bali ni mtoto wa yule waziri …..wa JK

Ndiyo sababu akajifanya ameamua kutogombea ili kusimamia uchaguzi.

Ndiyo kisingizio ambacho ameona aje nacho. Katibu mwenezi na kusimamia uchaguzi wapi na wapi? Uchaguzi unasimamia na ofisi ya katibu mkuu? Hata yeye naye akiamua hugombea. Ndivyo Makamba, Chiligati na wengine wote walivyofanya. Nape acha kuweweseka. Umeogopa muziki wa kamanda Lowassa.
 
Nape hana jimbo la kugombea. Asiwadanganye. Alitaka kugombea ujumbe wa NEC kupitia wilaya ya Kinondoni – akajipima akaona hawezi kupenya. Hapa yupo Londa na mwanachama mmoja yule mwizi wa TRA.

Akataka kwenda Masasi, nako akakumbana na kizingiti kutoka kwa familia ya Mosesi Nnauye ambaye yeye anajiita mwanawe. Wale watoto wake na baadhi ya ndugu wa NNauye wamegoma kumtambua. Wanasema Nape siyo mtoto wao, bali ni mtoto wa yule waziri …..wa JK

Ndiyo sababu akajifanya ameamua kutogombea ili kusimamia uchaguzi.

Ndiyo kisingizio ambacho ameona aje nacho. Katibu mwenezi na kusimamia uchaguzi wapi na wapi? Uchaguzi unasimamia na ofisi ya katibu mkuu? Hata yeye naye akiamua hugombea. Ndivyo Makamba, Chiligati na wengine wote walivyofanya. Nape acha kuweweseka. Umeogopa muziki wa kamanda Lowassa.
Unaongopa sana tu. Kwa nafasi yake ya sasa, Nape angeweza kugombea kupitia vile viti kumi vya Bara na angepita kwa kishindo kwa kuwa kura za mkutano mkuu wa CCM zinapigwa kiitifaki miaka yote ya chaguzi zao. Nape atateuliwa na Mwenyekiti mpya wa CCM ambaye tayari anajulikana.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom