Gambo Mrisho
New Member
- Sep 26, 2011
- 3
- 1
Frederick Katulanda, Mwanza
KATIBU Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye, amesisitiza kuwa adhima ya chama chake kuendelea na mpango wake wa kujivua magamba, bado iko palepale ila kinasubiri kumalizika kwa uchaguzi wa Igunga.
Akizungumza mjini Mwanza juzi, Nape alisema katika kikao cha Kamati Kuu kilichofanyika Dodoma Julai 31, mwaka huu, hatma ya makada wa CCM ambao walitakiwa kujivua gamba, ilielezwa kuwa itajulikana kwenye kikao cha Halmashauri kuu ya chama kilichotarajiwa kufanyika Septemba.
Nape alisema ingawa Septemba imefika, kikao hakijafanyika hivyo msimamo wa chama uko palepale kwa vile wanaopaswa kujivua magamba walishaelezewa kupima na kuamua wenyewe.
Jamani hili suala la kujivua gamba, siyo langu ni msimamo wa chama, tuliposema Septemba tulikuwa tukimaanisha kikao kitafanyika muda huo, lakini sasa katika busara ya kawaida huwezi kuwa na kikao huku kuna maafa na uchaguzi, alisema.
Alisema katika kikao kilichopita walijadili jambo hilo na kwamba, litajulikana hatma yake kikao kijacho Septemba, lakini wakati huo Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec), ilikuwa haijatangaza tarehe ya uchaguzi wa Igunga na kubainisha kuwa, adhima ya chaka bado ipo palepale kwa vile kikao hicho cha Septemba hakijafanyika.
Kikao kijacho tutamalizana nao hawa, tatizo ni kuwa watu wanataka tufanye haraka wanavyotaka wao, jamani uamuzi wa kikao kimoja unatoka na kwenda kikao kingine, hatujafanya kikao na kikifika tutajadili jambo hilo kwani litakuwa katika ajenda ya yatokanayo na kikao kilichopita, alisisitiza Nape.
Alisema wanapozungumzia kujivua gamba wanakuwa wamehusisha mpango wa chama kujifanyia mabadiliko katika mambo mengi na kueleza kuwa, hiyo siyo mara ya kwanza kwa CCM kufanya mabadiliko, huku akieleza yaliyofanyika tangu enzi za chama cha Taa, Tanu na mpaka kuzaliwa CCM.
Haya mabadiliko ni ya kila wakati kwa chama toka enzi za Taa, mabadiliko yalifanyika kukazaliwa Tanu ambayo iliunda azimio la Arusha, kisha tukaunganisha vyama ikazaliwa CCM, chama chetu kimepitia mabadiliko na kila baada ya miaka kumi kumekuwa na mabadiliko, alisema.
KATIBU Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye, amesisitiza kuwa adhima ya chama chake kuendelea na mpango wake wa kujivua magamba, bado iko palepale ila kinasubiri kumalizika kwa uchaguzi wa Igunga.
Akizungumza mjini Mwanza juzi, Nape alisema katika kikao cha Kamati Kuu kilichofanyika Dodoma Julai 31, mwaka huu, hatma ya makada wa CCM ambao walitakiwa kujivua gamba, ilielezwa kuwa itajulikana kwenye kikao cha Halmashauri kuu ya chama kilichotarajiwa kufanyika Septemba.
Nape alisema ingawa Septemba imefika, kikao hakijafanyika hivyo msimamo wa chama uko palepale kwa vile wanaopaswa kujivua magamba walishaelezewa kupima na kuamua wenyewe.
Jamani hili suala la kujivua gamba, siyo langu ni msimamo wa chama, tuliposema Septemba tulikuwa tukimaanisha kikao kitafanyika muda huo, lakini sasa katika busara ya kawaida huwezi kuwa na kikao huku kuna maafa na uchaguzi, alisema.
Alisema katika kikao kilichopita walijadili jambo hilo na kwamba, litajulikana hatma yake kikao kijacho Septemba, lakini wakati huo Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec), ilikuwa haijatangaza tarehe ya uchaguzi wa Igunga na kubainisha kuwa, adhima ya chaka bado ipo palepale kwa vile kikao hicho cha Septemba hakijafanyika.
Kikao kijacho tutamalizana nao hawa, tatizo ni kuwa watu wanataka tufanye haraka wanavyotaka wao, jamani uamuzi wa kikao kimoja unatoka na kwenda kikao kingine, hatujafanya kikao na kikifika tutajadili jambo hilo kwani litakuwa katika ajenda ya yatokanayo na kikao kilichopita, alisisitiza Nape.
Alisema wanapozungumzia kujivua gamba wanakuwa wamehusisha mpango wa chama kujifanyia mabadiliko katika mambo mengi na kueleza kuwa, hiyo siyo mara ya kwanza kwa CCM kufanya mabadiliko, huku akieleza yaliyofanyika tangu enzi za chama cha Taa, Tanu na mpaka kuzaliwa CCM.
Haya mabadiliko ni ya kila wakati kwa chama toka enzi za Taa, mabadiliko yalifanyika kukazaliwa Tanu ambayo iliunda azimio la Arusha, kisha tukaunganisha vyama ikazaliwa CCM, chama chetu kimepitia mabadiliko na kila baada ya miaka kumi kumekuwa na mabadiliko, alisema.