WABHEJASANA
JF-Expert Member
- Jun 22, 2011
- 4,225
- 869
Katibu wa itikadi siasa na Uenezi wa CCM Nape Nauye amesema kuikabidhi Nchi kwa wapinzani ni sawa na kumkabidhi Fisi Bucha,ambaye mwisho wa siku bada ya kula na kushiba atakimbia na kuiacha bucha kama ilivyo.
Nape alitoa Kauli hiyo mchana huu wakati akihutubia mkutano wa hadhara katika Mji mdogo wa Katoro wilayani Geita Mkoani Geita,ambapo alihutubia mamia ya wananchi waliohudhuria mkutano huo.
Alisema serikali ya Chama cha mapinduzi ka sasa inafanya mikakati ya kuhakikisha kamba inatekeleza ahadi zake zote ilizozitoa kwenye uchaguzi uliopita,na kwamba propaganda ambazo zimekuwa zikitolewa na wapinzani hazitakuwa na nguvu mwaka 2015 kwa sababu CCM itakuwa imetekeleza ahadi zake.
Amewataka wananchi kuiamini CCM kwa sababu kwa sasa imepata viongozi makini ambao wako mstari wa mbele kusimamia maslahi ya wanyonge,huku akimfagilia Katibu mkuu mpya wa Chama hicho Abdulhaman Kinana kwamba ni kiboko ya viongozi wabovu ndani na nje ya chama.
Wilaya ya Geita na haa katika majimbo ya Busanda na Geita yamekaliwa vibaya na upinzani,na inavyoonekana ziara ya Nape pamoja na katibu mkuu ambaye yeye alikuwa amebaki mjini Geita kwenye jimbo la Geita ni moja ya mkakati wa kuhakikisha kwamba wanazima harakati za vyama vya upinzani na hasa cdm katika kujikita kwenye majimbo hayo.
Nape alitoa Kauli hiyo mchana huu wakati akihutubia mkutano wa hadhara katika Mji mdogo wa Katoro wilayani Geita Mkoani Geita,ambapo alihutubia mamia ya wananchi waliohudhuria mkutano huo.
Alisema serikali ya Chama cha mapinduzi ka sasa inafanya mikakati ya kuhakikisha kamba inatekeleza ahadi zake zote ilizozitoa kwenye uchaguzi uliopita,na kwamba propaganda ambazo zimekuwa zikitolewa na wapinzani hazitakuwa na nguvu mwaka 2015 kwa sababu CCM itakuwa imetekeleza ahadi zake.
Amewataka wananchi kuiamini CCM kwa sababu kwa sasa imepata viongozi makini ambao wako mstari wa mbele kusimamia maslahi ya wanyonge,huku akimfagilia Katibu mkuu mpya wa Chama hicho Abdulhaman Kinana kwamba ni kiboko ya viongozi wabovu ndani na nje ya chama.
Wilaya ya Geita na haa katika majimbo ya Busanda na Geita yamekaliwa vibaya na upinzani,na inavyoonekana ziara ya Nape pamoja na katibu mkuu ambaye yeye alikuwa amebaki mjini Geita kwenye jimbo la Geita ni moja ya mkakati wa kuhakikisha kwamba wanazima harakati za vyama vya upinzani na hasa cdm katika kujikita kwenye majimbo hayo.