NAPE: Kukabidhi nchi kwa wapinzani ni sawa na kumkabidhi Fisi Bucha

Nisingependa kuamini kwamba Mwenyekiti alipomsifia Nape pale Mnazi Mmoja kwamba anafanya kazi nzuri sana na ya kusaidia Chama kwa kuwajibu wapinzani, alikuwa ana maana ya kauli za ovyo ovyo kama hizi; Haya ni matusi sio kwa wapinzani bali watanzania wanaotumia haki yao ya kikatiba kuunga mkono chama cha siasa wanachoona kinawafaa, bila ya kujalisha kama wanafanikiwa kukiweka chama hicho madarakani au hapana; Hii ni aibu sana kwa chama chetu, na sisi huku 'site' tumekuwa tunapata sana shida na maneno ya Nape, tunaonekana majuha kuunga CCM mkono, hata hoja za kukitetea zinaisha kwani mbali na chama kuvurunda kwenye mambo ya msingi, sasa kinaingia nguoni mwa watu na kuwavujinia heshima; kilichobakia ni kuwapiga tu na kuwapora mali zao;

Bora umesema.

Swali kwa Nape. Ikiwa CCM (angalau makada wakubwa waliobarikiwa na Mwenyekiti kukisemea chama)wanapinga kukabidhi nchi kwa wapinzani hivi, halafu ikatokea wananchi wakawapa wapinzani kura nyingi zaidi ya CCM, CCM (uongozi) watakubali kuheshimu maamuzi ya watu na kukabidhi uongozi wa nchi kwa wapinzani au la?
 
Mkuu mbona mlianza kuaminiwa toka mwaka 1961.. wakati huo ikiitwa TANU..! Umegeuka wimbo..?

Huyo Kinana c ndo anasafirisha meno ya tembo kwenda mashariki ya mbali huko..? Leo unadai ni kiongozi kiboko..? Labda kwa wizi wa nyara za nchi..!



Kinana ni Msomali damu, hivyo hana uchungu na nchi, chochote kitakachotokea hapa nchini kwake ni sawa kwani muda wowote ataukana uraia wa Tanzania.
 
Mkuu mimi sijui hilo na wala sio hoja yangu hiyo,hayo ya meno ya Tembo unayajua wewe na Kinana wako labda unafanya nae mimi sijui na wala si jukumu langu.

Mkuu kama kampuni inayomilikiwa na Katibu mkuu anaeonekana msafi imetumika kusafirisha meno ya tembo.. itamuwekaje huru huyu..? Pointi yangu ni kwamba Kinana hana usafi wa kucimama na kukemea wakati ana kashfa hiyo..
 
Mkuu kama kampuni inayomilikiwa na Katibu mkuu anaeonekana msafi imetumika kusafirisha meno ya tembo.. itamuwekaje huru huyu..? Pointi yangu ni kwamba Kinana hana usafi wa kucimama na kukemea wakati ana kashfa hiyo..

Narudia tena kwamba yawezekana unayoyasema ni kweli sipo kwa ajili ya kumtetea Kinana wala mtu yeyote humu JF isipokuwa napenda zaidi kujifunza mambo,na ili kunifanya niwe mfuasi wako hebu anza kwa kuanika hiyo Kampuni humu itanisaidia hata mimi kuingia BRELA na kubaini hilo Mkuu,tafadhali sana.
 
ni bora nchi ikabidhiwe fisi maana angalau fisi anaangalia nini cha kula na nini cha kuacha...CCM sasa hivi wao ni nguruwe...wanakula kila kitu mpaka kinyesi chao chenyewe...sasa yupi mbaya hapo..

mkuu hapo umeniacha hoi aise kwahilo bora fisi kama ngurue wanakula mpaka kinyesi chao bora 2 hii nchi 2ikabizi fisi
 
Nape, kwa nini mnauchu wa madraka namna hiyo? Mnajua mmeshindwa lakini bado mnagangania nchi. Hamjui kwamba Tanzania ni ya wa Tanzania? Au unadhani ni ya ccm tu?
 
Narudia tena kwamba yawezekana unayoyasema ni kweli sipo kwa ajili ya kumtetea Kinana wala mtu yeyote humu JF isipokuwa napenda zaidi kujifunza mambo,na ili kunifanya niwe mfuasi wako hebu anza kwa kuanika hiyo Kampuni humu itanisaidia hata mimi kuingia BRELA na kubaini hilo Mkuu,tafadhali sana.

Mkuu wala ucipate shida kwenda BRELA kutafuta umiliki wa kampuni hiyo.. Kinana mwenyewe amekiri kuimiliki kampuni hiyo.. Akasema ila hauciki kwenye uendeshaji wa kampuni hiyo..! Umenipata mkuu..? Sio kwamba ni majungu haya.. Inawezekana kweli hakuhucika kwenye usafirishaji huo but kutumika kwa kampuni yake ni tosha kutompa platform ya kisiasa kupita majukwaani na kuhubiri usafi na uadilifu..
 
Mkuu mimi sijui hilo na wala sio hoja yangu hiyo,hayo ya meno ya Tembo unayajua wewe na Kinana wako labda unafanya nae mimi sijui na wala si jukumu langu.
Kama wewe hujui na si jukumu lako, washukuru wenye majukumu hayo wanaokupatia uzi. Unajitetea utadhani upo mahakamani.
 
Mkuu wala ucipate shida kwenda BRELA kutafuta umiliki wa kampuni hiyo.. Kinana mwenyewe amekiri kuimiliki kampuni hiyo.. Akasema ila hauciki kwenye uendeshaji wa kampuni hiyo..! Umenipata mkuu..? Sio kwamba ni majungu haya.. Inawezekana kweli hakuhucika kwenye usafirishaji huo but kutumika kwa kampuni yake ni tosha kutompa platform ya kisiasa kupita majukwaani na kuhubiri usafi na uadilifu..

Mkuu nashukuru kwa taarifa nzuri,unajua sisi wachimbaji wa dhahabu mara nyingi tunashinda kwenye machimbo yetu huku porini Nyarugusu,na mara nyingi nakuwa ndani ya mashimo nikisaka dhahabu,kwa hiyo sehemu yangu pekee ya kuburudika na kupata taarifa ni humu JF ndio maana unaona natumia muda wangu mwingi Mkuu.

Sasa unaweza kunipasia hilo jina la kampuni yake,ila uwe makini na wengine wasione kama umenipa wewe Mkuu.
 
katibu wa itikadi siasa na uenezi wa ccm nape nauye amesema kuikabidhi nchi kwa wapinzani ni sawa na kumkabidhi fisi bucha,ambaye mwisho wa siku bada ya kula na kushiba atakimbia na kuiacha bucha kama ilivyo.

Nape alitoa kauli hiyo mchana huu wakati akihutubia mkutano wa hadhara katika mji mdogo wa katoro wilayani geita mkoani geita,ambapo alihutubia mamia ya wananchi waliohudhuria mkutano huo.

Alisema serikali ya chama cha mapinduzi ka sasa inafanya mikakati ya kuhakikisha kamba inatekeleza ahadi zake zote ilizozitoa kwenye uchaguzi uliopita,na kwamba propaganda ambazo zimekuwa zikitolewa na wapinzani hazitakuwa na nguvu mwaka 2015 kwa sababu ccm itakuwa imetekeleza ahadi zake.

Amewataka wananchi kuiamini ccm kwa sababu kwa sasa imepata viongozi makini ambao wako mstari wa mbele kusimamia maslahi ya wanyonge,huku akimfagilia katibu mkuu mpya wa chama hicho abdulhaman kinana kwamba ni kiboko ya viongozi wabovu ndani na nje ya chama.

Wilaya ya geita na haa katika majimbo ya busanda na geita yamekaliwa vibaya na upinzani,na inavyoonekana ziara ya nape pamoja na katibu mkuu ambaye yeye alikuwa amebaki mjini geita kwenye jimbo la geita ni moja ya mkakati wa kuhakikisha kwamba wanazima harakati za vyama vya upinzani na hasa cdm katika kujikita kwenye majimbo hayo.
hilo jina usilitamke karibu na mbuga za wanyama!! Tembo woteeeee hukimbia na kuficha pembe zao kwa kuzungushia mkonga!! Ni hatari kwa tembo(daudi mchambuzi- jf!)
 
Back
Top Bottom