Nape, 'Kujivua Gamba' ni danganya toto??

Kila siku mnatugeuzia maneno kuhusu hayo magamba, anyway I'm not a CCM fan lakini I would rather listen to January Makamba, he makes sense.
 
Nape tufafanulie kuhusu mabadiliko yaliyofanyika punde, nimekuona ukifafanua kwenye TV ila sikupata wasaa wa kufuatilia....

Pls Jembe
 
Nnauye Jr,

..zaidi ya hayo ya kujivua gamba, hivi CCM mmeridhika na matokeo ya mitihani ya kitaifa na mwenendo mzima wa sekta ya elimu hapa nchini?

..naona kama vile chama chako kinaliangamiza taifa letu kutokana na sera yake mbovu ya elimu. CCM na serikali zake imetufikisha mahali ambapo wahitimu wa mfumo wetu wa elimu hawaaminiki tena, na hiyo inadhihirishwa na matokeo ya mitihani na feedback tunayopata toka kwa waajiri[wawekezaji].

Aliyeleta huu uzi hajauliza hili wewe unauliza tu kwa sababu umemuona NAPE yuko jamvini? Wote tunayo maswali mengi ya kumuuliza lakini tukifanya hivyo itakuwa fujo na huyu aliyeleta huu uzi hatajibiwa ipasavyo.
 
Aliyeleta huu uzi hajauliza hili wewe unauliza tu kwa sababu umemuona NAPE yuko jamvini? Wote tunayo maswali mengi ya kumuuliza lakini tukifanya hivyo itakuwa fujo na huyu aliyeleta huu uzi hatajibiwa ipasavyo.

Kengemumaji,

..ni kwasababu Nape ni mtu adimu hapa jamvini.

..halafu hii hoja ya ufisadi imeshachuja sasa.

..CCM wana "dili-dali" tu na mafisadi hamna chochote wanachofanya.
 
Hoja nyingin: NAPE KAPUNGUZA UVUVUZELA...

Sina hakika uvuvzela upi uusemao, kama kelele zangu juu ya mijitu iliyojidanganya kuwa inaweza kupewa dhamana ikatumia dhamana hiyo kuifilisi nchi kwa kutumia wao na watoto wao kuingia mikataba ya hovyo ambayo inalazimu Watanzania wavuja jasho walipe, ni uvuvuzela basi nadhani uvuvuzela ni jambo jema sana na hapa nilipo nipo stage ya juu kabisa ya uvuvuzela. Maana nina hasira nao sana, kila nikikumbuka kuwa pengine wangekuwa makini na kutumia dhamana walizopewa vizuri tatizo la umeme leo ingekuwa historia, nasikia hasira sana...

Kila nikikumbuka kuna kina mama wanakufa kwa kukosa aspirini tu, wakati kuna watu walipewa dhamana wakaiingiza nchi kuwalipa bila huruma zaidi ya 152 Mill. Kwa siku, nasikia hasira sana.

Kuna vijana leo wanakaa chini, pesa walizofuja na kulipana bila huruma hao unaowatetea leo zingetatua tatizo hilo kwa kiasi gani?

Tatizo huyu Nova na wenzake hawaamini kama CCM inaweza kutokomeza ufisadi na mafisadi na kuzani kuwa kipo chama mbadala kinachoweza kufanya kazi hiyo.
 
Kenge.....
Nape yuko hapa acha kumsemea, wewe si msemaji wa chama chetu pls.......
Tatizo huyu Nova na wenzake hawaamini kama CCM inaweza kutokomeza ufisadi na mafisadi na kuzani kuwa kipo chama mbadala kinachoweza kufanya kazi hiyo.
 
Kengemumaji,

..ni kwasababu Nape ni mtu adimu hapa jamvini.

..halafu hii hoja ya ufisadi imeshachuja sasa.

..CCM wana "dili-dali" tu na mafisadi hamna chochote wanachofanya.



Jokakuu, naomba nikwambie kuwa hoja ya ufisadi haijachuja na itachuja tu pale mafisadi watakapochuliwa hatua japo siku zote mimi huwa najiuliza swali kwamba hivi fisadi hasa ni nani.... jibu silipati.
 
" Nape ni aina ya wanasiasa wanaopenda kubebwa kwa mbeleko"

HIVI KWELI NAPE NINGEKUWA MWANASIASA NINAYEBEBWA KWA MBELEKO NINGEWATOA KAMASI MAFISADI??? LINI NA WAPI NI MEWAHI KUBEBWA ACHILIA MBALI HATA KUOMBA KUBEBWA?

FUATILIA VIZURI HISTORIA YA SIASA YANGU, NILIINGIA KWENYE ACTIVE POLITICS MWAKA MMOJA BAADA YA BABA YANGU MZAZI MZEE MOSES NNAUYE KUFARIKI. TOKEA NIMEINGIA NIMEKUWA NIKIPAMBANA KUSHINDANA NA HAO WANAODHANI KWA PESA ZAO KILA KIJANA WATAMUWEKA MFUKONI, MIE NI MOJA YA VIJANA WENGI WANAOSEMA HAPANA KUWEKWA MFUKONI... NA NDIO CHANZO CHA MAFISADI KUJARIBU BILA MAFANIKIO KUNIKATISHA TAMAA, NASEMA KILA JUHUDI WAFANYAYO NI SAWA NA KUMWAGIA PETROLI KWENYE MOTO....ITAKULA KWENU.
 
Tatizo huyu Nova na wenzake hawaamini kama CCM inaweza kutokomeza ufisadi na mafisadi na kuzani kuwa kipo chama mbadala kinachoweza kufanya kazi hiyo.

Kengemumaji,

..sasa wewe na Nape mnatakiwa mjiulize CCM imefikaje hapo mpaka watu hawaiamini tena?

..hiki chama kimechoka. CCM sasa hivi imesheheni wachumia tumbo na watafuta madaraka kwa njia ya ukwasi.

..CCM used to be a party of ideas, hali siyo hivyo tena, na ndiyo maana unaona hakuna viongozi wa CCM ktk majukwaa ya uchambuzi wa fikra kama JF.
 
Nova,
Waambie mafisadi, tafadhali fikisha salaam hizi kama ulivyozifikisha kwangu kutoka kwao, wao ndio watoke tu wawaombe radhi watanzania kwa unyama waliowafanyia badala ya kudhani hawana akili kiasi cha kutaka eti wanaowatetea wananchi ndio wakaombe radhi... Shame on you fisadis...
 
JokaKuu naomba nijibu ya Nova nikimaliza tutajadili la elimu, pengine ukilianzishia thread yake itakuwa bora zaidi

Nape, I commend the way you are urgently reacting on issues raised - I like this kind of reaction it helps to clear issues outright without wasting G/thinkers times. Imagine if you delayed to react on this matter probably Nova would continue to post but now he is nowhere to be seen. I have seen several CDM leaders including Secretary General reacting in the same way they help to clear some issues of public concerns that require urgency. Hence spare time of great thinkers to other critical issues thereafter.

Gossiping is no good, Nova. You better show up and make your case while the alleged is online.
 
Jokakuu, naomba nikwambie kuwa hoja ya ufisadi haijachuja na itachuja tu pale mafisadi watakapochuliwa hatua japo siku zote mimi huwa najiuliza swali kwamba hivi fisadi hasa ni nani.... jibu silipati.

Kengemumaji,

..lakini Nape anazungumza kama vile anawajua mafisadi ni nani haswa.

..lakini zaidi ya ufisadi ni kwamba life doesnt seem to get any better kwa wananchi wa kawaida.

..nadhani hiyo ndiyo changamoto kubwa zaidi kwa CCM na serikali yake.
 
TOKEA NIMEINGIA NIMEKUWA NIKIPAMBANA KUSHINDANA NA HAO WANAODHANI KWA PESA ZAO KILA KIJANA WATAMUWEKA MFUKONI, MIE NI MOJA YA VIJANA WENGI WANAOSEMA HAPANA KUWEKWA MFUKONI... NA NDIO CHANZO CHA MAFISADI KUJARIBU BILA MAFANIKIO KUNIKATISHA TAMAA, NASEMA KILA JUHUDI WAFANYAYO NI SAWA NA KUMWAGIA PETROLI KWENYE MOTO....ITAKULA KWENU.
Nape SASA unaonyesha uanamme wako mambo yakukimbia umeacha HONGERA MKUU!:poa

tunapenda sana hoja zetu zijibiwe.
 
Hoja nyingin: NAPE KAPUNGUZA UVUVUZELA...

Sina hakika uvuvzela upi uusemao, kama kelele zangu juu ya mijitu iliyojidanganya kuwa inaweza kupewa dhamana ikatumia dhamana hiyo kuifilisi nchi kwa kutumia wao na watoto wao kuingia mikataba ya hovyo ambayo inalazimu Watanzania wavuja jasho walipe, ni uvuvuzela basi nadhani uvuvuzela ni jambo jema sana na hapa nilipo nipo stage ya juu kabisa ya uvuvuzela. Maana nina hasira nao sana, kila nikikumbuka kuwa pengine wangekuwa makini na kutumia dhamana walizopewa vizuri tatizo la umeme leo ingekuwa historia, nasikia hasira sana...

Kila nikikumbuka kuna kina mama wanakufa kwa kukosa aspirini tu, wakati kuna watu walipewa dhamana wakaiingiza nchi kuwalipa bila huruma zaidi ya 152 Mill. Kwa siku, nasikia hasira sana.

Kuna vijana leo wanakaa chini, pesa walizofuja na kulipana bila huruma hao unaowatetea leo zingetatua tatizo hilo kwa kiasi gani?
Nape unayoongea ndo ambayo kila siku tunayapigania lakin inaonekana ndani ya ccm kama upo pekeyako hivi unayepinga ufisadi, wengine woote wasanii na waoga. sasa nadhani utafeil brother u cant make it! bwana!
 
Nadhani bado hujajibu kwanini chama kiliwapa mafisadi 90 days kung'atuka otherwise mtafanya wenyewe na stil hatuoni reaction yoyote.
 
TOKEA NIMEINGIA NIMEKUWA NIKIPAMBANA KUSHINDANA NA HAO WANAODHANI KWA PESA ZAO KILA KIJANA WATAMUWEKA MFUKONI, MIE NI MOJA YA VIJANA WENGI WANAOSEMA HAPANA KUWEKWA MFUKONI... NA NDIO CHANZO CHA MAFISADI KUJARIBU BILA MAFANIKIO KUNIKATISHA TAMAA, NASEMA KILA JUHUDI WAFANYAYO NI SAWA NA KUMWAGIA PETROLI KWENYE MOTO....ITAKULA KWENU.

Nimeipenda Lugha hii ni wachache sana waweza jua lugha hii,manake wengi ni tomaso mpaka washike kwanza,hawajui kuwa sisimizi uweza kuua tembo.Na bado !!!!!!!!!!!!!!
 
Hoja nyingin: NAPE KAPUNGUZA UVUVUZELA...

Sina hakika uvuvzela upi uusemao, kama kelele zangu juu ya mijitu iliyojidanganya kuwa inaweza kupewa dhamana ikatumia dhamana hiyo kuifilisi nchi kwa kutumia wao na watoto wao kuingia mikataba ya hovyo ambayo inalazimu Watanzania wavuja jasho walipe, ni uvuvuzela basi nadhani uvuvuzela ni jambo jema sana na hapa nilipo nipo stage ya juu kabisa ya uvuvuzela. Maana nina hasira nao sana, kila nikikumbuka kuwa pengine wangekuwa makini na kutumia dhamana walizopewa vizuri tatizo la umeme leo ingekuwa historia, nasikia hasira sana...

Kila nikikumbuka kuna kina mama wanakufa kwa kukosa aspirini tu, wakati kuna watu walipewa dhamana wakaiingiza nchi kuwalipa bila huruma zaidi ya 152 Mill. Kwa siku, nasikia hasira sana.

Kuna vijana leo wanakaa chini, pesa walizofuja na kulipana bila huruma hao unaowatetea leo zingetatua tatizo hilo kwa kiasi gani?
Ndugu yake nape agenda yako ya kupinga ufisadi ni nzuri na unastahili pongezi, ila unapokesea ni kuwa mafisadi wanaonekana mbele yako ni wale tu ambao hawako kwenye kambi yako ya 2015, ila wale ambao wako upande wako wao sio mafisadi hapo ndipo tunasema kuwa dhana yako ya kupinga ufisadi inalenga 2015
 
Hoja nyingin: NAPE KAPUNGUZA UVUVUZELA...

Sina hakika uvuvzela upi uusemao, kama kelele zangu juu ya mijitu iliyojidanganya kuwa inaweza kupewa dhamana ikatumia dhamana hiyo kuifilisi nchi kwa kutumia wao na watoto wao kuingia mikataba ya hovyo ambayo inalazimu Watanzania wavuja jasho walipe, ni uvuvuzela basi nadhani uvuvuzela ni jambo jema sana na hapa nilipo nipo stage ya juu kabisa ya uvuvuzela. Maana nina hasira nao sana, kila nikikumbuka kuwa pengine wangekuwa makini na kutumia dhamana walizopewa vizuri tatizo la umeme leo ingekuwa historia, nasikia hasira sana...

Kila nikikumbuka kuna kina mama wanakufa kwa kukosa aspirini tu, wakati kuna watu walipewa dhamana wakaiingiza nchi kuwalipa bila huruma zaidi ya 152 Mill. Kwa siku, nasikia hasira sana.

Kuna vijana leo wanakaa chini, pesa walizofuja na kulipana bila huruma hao unaowatetea leo zingetatua tatizo hilo kwa kiasi gani?


Mh! Hakika una uchungu na watanzania!

Ebu fanyeni maamuzi ya kuuza V8 yako na za viongozi waandamizi wa chama,ili aspirin na madawati yapatikane.

Pia rudisheni mali chama chenu kilizojimilikisha toka enzi za chama kimoja. Mali hizo zitaweza kuongeza uwigo wa mapato ya dola.

Lakini ukizungumza hayo juu wakati wewe unachekelea katika V8 pale unapoenda kutembelea shule ya watoto wanaokaa vumbini au zahanati ambayo kina mama zaidi ya 3 wanalala ki tanda kimoja,hakika utakua VUVUZELA.
 
Nnauye Jr

Katika majibu yako kwa Nova umejaribu kujipambanua kama mmoja wa wapambanaji dhidi ya mafisadi, na katika moja ya posts zako umesema kama si mafisadi kusingekuwa na tatizo la umeme bila shaka umelenga ufisadi unaofanywa kupitia mikataba ya Tanesco na wazalishaji hewa.

Hapa bila kuuma maneno swala la Richmond/Dowans liko mstari wa mbele. Hapo ktk ufisadi wa Richmond, kiongozi wa mafisadi atakuwa ni Rais kikwete ambaye alikuwa mwenyekiti wa baraza la mawaziri lililobariki mkataba wa Richmond, aidha Richmond ilipowekwa hadharani kikwete na serikali yake waliruhusu biashara ya kihuni ya richmond kuiuzia mkataba dowans hivyo kuzidi kuthibitisha ushiriki wa wazi wa kikwete ktk ufisadi huo. kwahiyo wewe umewekwa hapo ulipo na fisadi, tutaaminije kuwa wewe sio fisadi mwenzao?

Halafu ni kwanini usianze na aliyekuwa mwenyekiti wa baraza la mawaziri lililobariki ufisadi?
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom