KakaKiiza
JF-Expert Member
- Feb 16, 2010
- 11,578
- 8,596
Mimi nimekuwa nikifuatilia kwa umakini zaidi kuhusu hii la CCM kujivua Gamba tangu siku ile Nape Nnauye aseme kwamba wale wote walio ndani ya chama hicho na wamezungukwa na kashifa, sasa muda wao umefika wa kujiondoa katika nyadhifa zao au la watatolewa kwa nguvu!
Hakuishia hapo aliwapa miezi mitatu na kwakuwa aliwalenga watu Kama Andrew Change, Rostam Aziz, Edward Lowassa. Nikasubiri mkutano mkuu nikijua watawavua gamba kama walivyo tangaza awali ila chakushangaza CCM iko kimya kama haijawai kusemwa kitu!
Je, CCM inawambia vipi wananchi wa Igunga kuhusu kashifa zinazo waandama viongozi wake?
Je, CCM inajikosha vipi kwa jamii kutokana na kauli yake ya kujivua Gamba?
Je, Nape aliropoka au aliyekuwa akitumiwa na mtu sasa kaona pazito kaamua kukaa kimya mbona sasa hatumsikii?
Au wameamua kuwasamehe watuhumiwa wa kashifa za ufisadi!?
Hakuishia hapo aliwapa miezi mitatu na kwakuwa aliwalenga watu Kama Andrew Change, Rostam Aziz, Edward Lowassa. Nikasubiri mkutano mkuu nikijua watawavua gamba kama walivyo tangaza awali ila chakushangaza CCM iko kimya kama haijawai kusemwa kitu!
Je, CCM inawambia vipi wananchi wa Igunga kuhusu kashifa zinazo waandama viongozi wake?
Je, CCM inajikosha vipi kwa jamii kutokana na kauli yake ya kujivua Gamba?
Je, Nape aliropoka au aliyekuwa akitumiwa na mtu sasa kaona pazito kaamua kukaa kimya mbona sasa hatumsikii?
Au wameamua kuwasamehe watuhumiwa wa kashifa za ufisadi!?