DSN
JF-Expert Member
- Feb 2, 2011
- 2,837
- 1,674
Nova,
Waambie mafisadi, tafadhali fikisha salaam hizi kama ulivyozifikisha kwangu kutoka kwao, wao ndio watoke tu wawaombe radhi watanzania kwa unyama waliowafanyia badala ya kudhani hawana akili kiasi cha kutaka eti wanaowatetea wananchi ndio wakaombe radhi... Shame on you fisadis...
Jamvini wananijua mi si mwanaccm ama chadema kwangu Tanzania mbele,lakini I always salute to anyone mwenye kupigania Taifa au Mwananchi yoyote wa Taznania ambae ni mpenda haki na mtenda haki,hivyo basi kwa vita vya mafisadi kijana mimi nakupa tano,mkimaliza na madingi na wasure wote wasimamizi wa strategy za ufisadishaji wa Taifa Tanzania njoo kwa recruitment team ya mafisadi viijana.
Mkiwaacha ndani ya vikao vya maamuzi watawageuka na kurecruit vijana innocent hivyo bidii zote zitakuwa hazina maana,wapigeni chini wote na muaanzishe CCM ya vijana wanaotanguliza Tanzania mbele hakika mtakuwa na nafasi nzuri ya kuchuana vyema na Chadema vinginevyo mkiendeleza kuwapa nafasi vijana wa mafisadi hakika kiti cha urais cha mwaka 2015 mtakisikia Radioni hata kama ni sarakasi za mzee kama kinana zitagota ukuta kwa kuwa tayari Watanzania wanafunguka na wanakuwa na ufahamu mkubwa wa dunia inavyokwenda kulinganisha na miaka mitano iliyopita.
My concern to you Nape, be creative and genuine kuwashauri CCM wabadilike enzi ya ubabaishaji na mizengwe kuwa CCM ndicho chama Nchi zimekwisha na sasa kiwape wananchi kile ilicho wahaidi kupitia ilani ya chama chenu,nje ya hapo ITAKULA KWENU kwa kuwa WHAT GOES AROUND COMES AROUND.Unavyoona wewe na kujisikia dhidi ya Nchi yako ndio mamilioni ya vijana Watanzania huko mitaani wanavyojikia.
Tumejifunza kama Taifa na kupitia ufisadi Taifa na Wananchi wamepata mwanga, na ufahamu umeongezeka na kupima tuelekee upande upi je niule wa Taifa kwanza au ni ule wa kikundi cha watu [chama] kwanza?Ustawi wa Taifa unategemea integrity ya waale waliopewa dhamana ya utawala,lakini chama chako kilipotufikisha toka miaka 20 iliyopita hakika umeecha jeraha baya sana ambalo madhara yake itatugharimu miaka kumi na ushee kuyamaliza.
Si pabaya wapigana vita vya kifisadi walipofika na vita nzuri daima ni ile ya wapiganaji wachache,ndio maana Fidel Castro alipofanya mapinduzi Nchini Cuba baadae miaka kadha baada ya mapinduzi alipoulizwa kama angepewa nafasi nyingine ya mapinduzi angesemaje,akasema wakati wa mapinduzi ya wakati huo alikuwa na kikosi cha watu 70 lakini kama angepewa nafasi hiyo leo angeitaji watu 16.Nawe Nape mapambano yako na wenzio haitaji lundo la watu,hivyo watu kama hawa walioanzisha thread hii ni watumwa wape pole,toka lini mtumwa akawa na Free will.
Nami nakukubali kuwa una Free will kitu ambacho ni unique sana kwa vijana wachache walio kwenye siasa za kitanzania kwa kuwa wengi walio huko hasa upande wa CCM wengi wao wamebebwa na kuwa wamefika hapo walipo kwa kuwa na sifa moja huyu n mwenzetu mkono kwa mkono,kisha baadae ukolome, upinge, ukatae, usimamie ukweli, ujipendi wakati umebebwa.Wabebwaji wanawatumikia mabwana zao na si vinginevyo ndio maana tunawaona ni mzigo kwa Taifa.Na daima mtu mwenye Free will daima huwa hana hofu,umuogopa Mungu na kumuheshimu mwanadamu mwenzie.