Nape: Huwezi kuwatumikia mabwana wawili

PISTO LERO

JF-Expert Member
Mar 8, 2011
2,819
1,454
SIKU chache baada ya Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk. Willibrod Slaa, kumtaka Katibu wa Halmashauri Kuu (NEC) Itikadi na Uenezi ya CCM kuacha kupiga mayowe na badala yake awaeleze wananchi hatua zinazofanywa na serikali yao kuondoa umaskini, ni dhahiri sasa kada huyo ameanza kuweweseka kisiasa.

Nape ambaye aliibua mjadala ambao hata hivyo alishindwa kuuthibitisha kuhusu madai kuwa Dk. Slaa anamiliki kadi ya CCM na anaendelea kuilipia ada ya uanachama, ameamua kuhamishia siasa za uzushi na matusi kwenye mtandao wa kijamii.

Katika maoni yake aliyoandika kwenye ukurasa wa mtandnao wa Jamii Forum, Nape ameendelea kuupotosha umma kwa kuwaponda waliomtetea Dk. Slaa katika uzushi huo na kuzua uongo mwingine kuwa gazeti la Tanzania Daima linamilikiwa na operesheni ya Vuguvugu la Mabadiliko (M4C) inayoendeshwa na CHADEMA.

“Nazitambua juhudi za wafuasi wa babu (akimaanisha Dk. Slaa) na mashabiki wake katika kujaribu kumtetea ionekane ni jambo la kawaida sana kwake kuwa na kadi ya CCM mpaka leo.

“Juhudi za kutumia ‘social media’ na magazeti mengine hasa gazeti la M4C (TanzaniaDaima) kujaribu kumtetea Dk. Slaa na wakati huo kunikejeli na kunitukana japo kuwa kwa matusi ambayo lazima nikiri si mapya,” aliongopa Nape.

Katika utetezi wake huo, Nape anajikologa akisema katika matamshi yake hakuna mahali alipohusisha kuwa na kadi na uanachama wa mtu.....hivyo wanaojaribu kubwabwaja kuwa sijui katiba ya CCM, wanakurupuka kwa sababu ndogo sana.

“Kukaririshwa lazima kumtukana Nape hata bila kupima kwa makini hoja....nilichosema Dk. Slaa na baadhi ya vigogo wa CHADEMA wana kadi za CCM na baadhi yao wanazilipia mpaka leo,” alisema.

Aliongeza kuwa hajazungumzia uanachama wao, kwamba anajua kuwa kwa katiba ya CCM ukishakuwa mwanachama wa chama kingine uanachama wako CCM unakufa hapohapo.

“Ni kweli kuwa hakuna mahusiano ya moja kwa moja kati ya kuwa na kadi ya CCM kwa Dk. Slaa na maendeleo ya wananchi maskini, lakini Dk. Salaa anatafuta kuwa kiongozi wa nchi anapaswa kuishi yale anayoyasema na kuwa mwaminifu kwa nafsi yake mwenyewe,” alijitetea.
 
Nadhani muda umefika kwa waandishi wa habari kuwa ni chanzo cha mabadiliko ya uchumi, siasa na kijamii katika Taifa letu. Hizi Mada za majibizano yasiyokuwa na tija tuyaweke pembeni hazina manufaa kwa mtanzania yoyote, zinatujazia nafasi na zinatuwekea ukakasi wa kuzisoma.

Hii habari ya nani mwanachama wa chama gani anamiliki kadi ya chama gani, si za kuzungumza leo kwenye karne hii ya mabadiliko ya kasi. Tuache propaganda na uenezui usiyo na tija kwa walalahoi. Andikeni nini kinatakiwa kufanyika Tanzania ili kuondoa/kupunguza wimbi hili kubwa la umaskini lililotanda miongoni mwetu.. Waandishi wa habari tumien weled wenu wa uandishi kuelimisha na kuwaambia watu hali halisi na mustakabadhi wa Taifa. Tuna mambo mengi sana tunategemea kuyaona waandishi wa habari kama kioo cha jamii wakiyapigia kelele na kuyakeme kwa kutumia kalamu zenu kwa mfano.

  • Umaskini
  • Unyanyapaa,
  • Ufisadi
  • Uonevu wa polis kwa raia wasio na hatia na kwenu ninyi waandishi wa habari
  • Ubadhifu wa rasilimali za Nchi kwa kutumia watoto wa vigogo kumiliki share kubwa kwenye makapuni ya madini
  • Bidhaa mbalimbali kupanda bei kila kukicha( Petrol) na mazao.
  • Msongamano wa magari jijini
  • Msongamano wa wawagonjwa mawodini katka mahospitali yetu
  • Wanafunzi kufaulu darasa la saba bila kujua kusoma na kuandika
  • Ufinyu wa maabara na library katka shule zetu za kata na zisizo za kata.
  • Vurugu zinazobabishwa na vikundi vya watu kwa kisingizio cha dini.
  • Katiba mpya
Nadhani kama waandishi wa habari mkikazia haya mambo na mkayaanika na kuyaandika kwa mapana yake, basi hata muda wa kusoma mawazo yanayoandikwa na wenye uchu wa madaraka na ufinyu wa mawazo, poor vision people na ubinafsi humu JF hatampata kamwe. Tufike mahali tuwe na uchungu na uzalendo kwanza then ubinafsi baadae..

Asanten
 
katibu mwenezi wa CCJ.pia ukiwa katibu mwenezi wa CCM.
wahenga walisema ukiwa mnafiki ujanani,ukiwa mzee kama wasira lazima uwe mchawi.
Chagua moja ubaki katibu mwenezi wa CCJ au uendeleze kampeni ya kumnadi marehemu CCM .chama kilichofikwa na umauti kwa kusheheni wanafiki kama wewe.ambapo licha ya propaganda zako 2015.utakuwa katibu mwenezi wa hivi vyama viwili.
Nakuandikia kwa kuwa hujawahi kukanusha maneno thabiti ya kamanda FREDIRICK MPENDAZOE. ALIYEKUANIKA HADHARANI PALE VIWANJA NZOVWE MBEYA.KUWA WEWE NI MWENEZI WA CCJ.
AMA LA KANUSHA HUMU JF.
 
Nape hana babu?
hivi kweli kwenye ukoo wote wa nape amekosa mtu wa kumuita babu, Inawezekana amekosa hivi anafahahamu tofauti ya umri wa kinana na slaa wote hawa ni makatibu kwa nini asihamishie utani wake kwa wazee wa ccm. kimsingi kama ni mababu wapo wengi ccm
 
Nape ana chuki na dr slaa kwasbbu alitaka sana awe mgombea wa chadema ubungo, alipogomewa na mnyika kuchukua nafasi ana gubu zito rohoni, mwacheni tu mpaka hapo atakapotulia
 
Nape ana chuki na dr slaa kwasbbu alitaka sana awe mgombea wa chadema ubungo, alipogomewa na mnyika kuchukua nafasi ana gubu zito rohoni, mwacheni atakua tu
 
Nape ni vuvuzela hana lolote jipya wala la maana...sidhani kama cheo cha uenezi na propaganda anakiweza
 
Nadhani muda umefika kwa waandishi wa habari kuwa ni chanzo cha mabadiliko ya uchumi, siasa na kijamii katika Taifa letu. Hizi Mada za majibizano yasiyokuwa na tija tuyaweke pembeni hazina manufaa kwa mtanzania yoyote, zinatujazia nafasi na zinatuwekea ukakasi wa kuzisoma.

Hii habari ya nani mwanachama wa chama gani anamiliki kadi ya chama gani, si za kuzungumza leo kwenye karne hii ya mabadiliko ya kasi. Tuache propaganda na uenezui usiyo na tija kwa walalahoi. Andikeni nini kinatakiwa kufanyika Tanzania ili kuondoa/kupunguza wimbi hili kubwa la umaskini lililotanda miongoni mwetu.. Waandishi wa habari tumien weled wenu wa uandishi kuelimisha na kuwaambia watu hali halisi na mustakabadhi wa Taifa. Tuna mambo mengi sana tunategemea kuyaona waandishi wa habari kama kioo cha jamii wakiyapigia kelele na kuyakeme kwa kutumia kalamu zenu kwa mfano.

  • Umaskini
  • Unyanyapaa,
  • Ufisadi
  • Uonevu wa polis kwa raia wasio na hatia na kwenu ninyi waandishi wa habari
  • Ubadhifu wa rasilimali za Nchi kwa kutumia watoto wa vigogo kumiliki share kubwa kwenye makapuni ya madini
  • Bidhaa mbalimbali kupanda bei kila kukicha( Petrol) na mazao.
  • Msongamano wa magari jijini
  • Msongamano wa wawagonjwa mawodini katka mahospitali yetu
  • Wanafunzi kufaulu darasa la saba bila kujua kusoma na kuandika
  • Ufinyu wa maabara na library katka shule zetu za kata na zisizo za kata.
  • Vurugu zinazobabishwa na vikundi vya watu kwa kisingizio cha dini.
  • Katiba mpya
Nadhani kama waandishi wa habari mkikazia haya mambo na mkayaanika na kuyaandika kwa mapana yake, basi hata muda wa kusoma mawazo yanayoandikwa na wenye uchu wa madaraka na ufinyu wa mawazo, poor vision people na ubinafsi humu JF hatampata kamwe. Tufike mahali tuwe na uchungu na uzalendo kwanza then ubinafsi baadae..

Asanten

Mwanadamu hataishi kwa mkate tu! In life there is a time to take on serious issues, a time to joke, a time to cry, a time to fool around, a time decompress and relax!!!

Man do not take life too seriously afterall you shall never come out of it alive. ha haha ha!!
 
The best way kumshinda Nape ni kum-ignore,
Kumjibu Nape ni bure, hana kitu chochote huyo, Hana Jipya.
 
Nape ana chuki na dr slaa kwasbbu alitaka sana awe mgombea wa chadema ubungo, alipogomewa na mnyika kuchukua nafasi ana gubu zito rohoni, mwacheni tu mpaka hapo atakapotulia

ndio mnavodanganyana kwenye vijiwe vya kahawa?
 
Nadhani muda umefika kwa waandishi wa habari kuwa ni chanzo cha mabadiliko ya uchumi, siasa na kijamii katika Taifa letu. Hizi Mada za majibizano yasiyokuwa na tija tuyaweke pembeni hazina manufaa kwa mtanzania yoyote, zinatujazia nafasi na zinatuwekea ukakasi wa kuzisoma.

Hii habari ya nani mwanachama wa chama gani anamiliki kadi ya chama gani, si za kuzungumza leo kwenye karne hii ya mabadiliko ya kasi. Tuache propaganda na uenezui usiyo na tija kwa walalahoi. Andikeni nini kinatakiwa kufanyika Tanzania ili kuondoa/kupunguza wimbi hili kubwa la umaskini lililotanda miongoni mwetu.. Waandishi wa habari tumien weled wenu wa uandishi kuelimisha na kuwaambia watu hali halisi na mustakabadhi wa Taifa. Tuna mambo mengi sana tunategemea kuyaona waandishi wa habari kama kioo cha jamii wakiyapigia kelele na kuyakeme kwa kutumia kalamu zenu kwa mfano.

  • Umaskini
  • Unyanyapaa,
  • Ufisadi
  • Uonevu wa polis kwa raia wasio na hatia na kwenu ninyi waandishi wa habari
  • Ubadhifu wa rasilimali za Nchi kwa kutumia watoto wa vigogo kumiliki share kubwa kwenye makapuni ya madini
  • Bidhaa mbalimbali kupanda bei kila kukicha( Petrol) na mazao.
  • Msongamano wa magari jijini
  • Msongamano wa wawagonjwa mawodini katka mahospitali yetu
  • Wanafunzi kufaulu darasa la saba bila kujua kusoma na kuandika
  • Ufinyu wa maabara na library katka shule zetu za kata na zisizo za kata.
  • Vurugu zinazobabishwa na vikundi vya watu kwa kisingizio cha dini.
  • Katiba mpya
Nadhani kama waandishi wa habari mkikazia haya mambo na mkayaanika na kuyaandika kwa mapana yake, basi hata muda wa kusoma mawazo yanayoandikwa na wenye uchu wa madaraka na ufinyu wa mawazo, poor vision people na ubinafsi humu JF hatampata kamwe. Tufike mahali tuwe na uchungu na uzalendo kwanza then ubinafsi baadae..

Asanten
Una akili sana,haya ndiyo mambo ambayo watu wenye fikra pevu wanatakiwa kujadili,siyo upuuzi wa VUVUZELA Nnauye Jr &co.
 
Hana jipya huko magamba kuna-mababu wangapi? yeye mwenyewe babu tu kama chama lake la kijani+njano. Vijana wote ki-umri na kifikra wapo upinzani specifically M4C. Wamempa cheo gagari awe kivutio lakini badala yake anazidi kuwaharibia.
 
Nadhani muda umefika kwa waandishi wa habari kuwa ni chanzo cha mabadiliko ya uchumi, siasa na kijamii katika Taifa letu. Hizi Mada za majibizano yasiyokuwa na tija tuyaweke pembeni hazina manufaa kwa mtanzania yoyote, zinatujazia nafasi na zinatuwekea ukakasi wa kuzisoma.

Hii habari ya nani mwanachama wa chama gani anamiliki kadi ya chama gani, si za kuzungumza leo kwenye karne hii ya mabadiliko ya kasi. Tuache propaganda na uenezui usiyo na tija kwa walalahoi. Andikeni nini kinatakiwa kufanyika Tanzania ili kuondoa/kupunguza wimbi hili kubwa la umaskini lililotanda miongoni mwetu.. Waandishi wa habari tumien weled wenu wa uandishi kuelimisha na kuwaambia watu hali halisi na mustakabadhi wa Taifa. Tuna mambo mengi sana tunategemea kuyaona waandishi wa habari kama kioo cha jamii wakiyapigia kelele na kuyakeme kwa kutumia kalamu zenu kwa mfano.

  • Umaskini
  • Unyanyapaa,
  • Ufisadi
  • Uonevu wa polis kwa raia wasio na hatia na kwenu ninyi waandishi wa habari
  • Ubadhifu wa rasilimali za Nchi kwa kutumia watoto wa vigogo kumiliki share kubwa kwenye makapuni ya madini
  • Bidhaa mbalimbali kupanda bei kila kukicha( Petrol) na mazao.
  • Msongamano wa magari jijini
  • Msongamano wa wawagonjwa mawodini katka mahospitali yetu
  • Wanafunzi kufaulu darasa la saba bila kujua kusoma na kuandika
  • Ufinyu wa maabara na library katka shule zetu za kata na zisizo za kata.
  • Vurugu zinazobabishwa na vikundi vya watu kwa kisingizio cha dini.
  • Katiba mpya
Nadhani kama waandishi wa habari mkikazia haya mambo na mkayaanika na kuyaandika kwa mapana yake, basi hata muda wa kusoma mawazo yanayoandikwa na wenye uchu wa madaraka na ufinyu wa mawazo, poor vision people na ubinafsi humu JF hatampata kamwe. Tufike mahali tuwe na uchungu na uzalendo kwanza then ubinafsi baadae..

Asanten
Mimi naamini kabisa tatizo sio Nape kwani yeye analipwa kwa kuzungumza ila ni WAANDISHI wa habari ambao HAWAPIMI/KUCHUJA habari gani yenye TIJA kwa wananchi anayoisema na hii sio tu kwake Nape.
 
Nape anapaswa kuchapwa ile k2 ya 0713....... Koz ndio dawa ya wanasiasa wenye siasa za majitaka.
 
Nape hana babu?
hivi kweli kwenye ukoo wote wa nape amekosa mtu wa kumuita babu, Inawezekana amekosa hivi anafahahamu tofauti ya umri wa kinana na slaa wote hawa ni makatibu kwa nini asihamishie utani wake kwa wazee wa ccm. kimsingi kama ni mababu wapo wengi ccm

Achilia mbali kinana , Moses Nnauye ambaye ni baba yake kama angekuwa hai angekuwa ni Mtoto wa Dr Slaa kiumri ? Heshima ni kitu cha bure ndugu Nape , hivi vyeo vya kuteuliwa visikufanye ushindwe kujiheshimu kaka !
 
Achilia mbali kinana , Moses Nnauye ambaye ni baba yake kama angekuwa hai angekuwa ni Mtoto wa Dr Slaa kiumri ? Heshima ni kitu cha bure ndugu Nape , hivi vyeo vya kuteuliwa visikufanye ushindwe kujiheshimu kaka !
Baba yake wa kuzaa wa Nape sio Moses Nnauye bali Mwandosya... Iwapo Nape anapinga aje hapa athibitishe!!! Sasa anaweza kumuita Mwandosya babu?
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom