Hivi juzijuzi Nape alisikika akitaka CHADEMA kiombe radhi kwa matamshi aliyotoa Mbunge wa Arumeru Mashariki kwa kauli inayofikiriwa au tafsiriwa ni maneno ya ubaguzi.
Huku akisahau kuwa naye amewahi kutoa kauli za kibaguzi za ukabila pale aliposema " mimi si mchaga mpaka nifikirie kujiunga Chadema" maneno haya aliyasema baada ya kuwapo tuhuma kuwa alitaka kugombea kupitia CHADEMA katika jimbo la Ubungo baada ya kutemwa nadani ya CCM katika kura za maoni.
Na wala hajaomba radhi mpaka leo, kwa kinywa chake aliyazungumza haya leo kinywa hikihiki kinazungumza umuhimu wa radhi ili hali NAPE mwenyewe hakuomba msamaha. Bila shaka Nape anachukulia hili kinafiki na kisiasa uchwara kama ilivyodaiwa kuzifanya na Rostam Aziz.
Huku akisahau kuwa naye amewahi kutoa kauli za kibaguzi za ukabila pale aliposema " mimi si mchaga mpaka nifikirie kujiunga Chadema" maneno haya aliyasema baada ya kuwapo tuhuma kuwa alitaka kugombea kupitia CHADEMA katika jimbo la Ubungo baada ya kutemwa nadani ya CCM katika kura za maoni.
Na wala hajaomba radhi mpaka leo, kwa kinywa chake aliyazungumza haya leo kinywa hikihiki kinazungumza umuhimu wa radhi ili hali NAPE mwenyewe hakuomba msamaha. Bila shaka Nape anachukulia hili kinafiki na kisiasa uchwara kama ilivyodaiwa kuzifanya na Rostam Aziz.