Technician
JF-Expert Member
- Mar 30, 2010
- 841
- 222
Nape ampiga vijembe Mrema
na Rodrick Mushi, Moshi
KATIBU wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, ametupa vijembe vingine kwa Mbunge wa Vunjo Augustine Mrema, akisema hatambuliki kuwa ni wa chama cha Tanzania Labour Party (TLP) au ni Chama cha Mapinduzi (CCM).
Nape alitoa kauli hiyo kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika eneo lililoko karibu na stendi kuu ya mabasi mjini Moshi, mkoani Kilimanjaro.
Licha ya upinzani kujigamba kuwa wana nguvu ya umma lakini tukiangalia bado tunaongoza kwa kila kitu, mkoa wa Kilimanjaro tuna wabunge watano wa CCM na watatu wa CHADEMA lakini huyo mmoja wa TLP yeye hajulikani wa CCM au TLP, alikejeli Nape.
Akijibu tuhuma hizo Mrema alisema hiyo ni mipango michafu ya kumchafua na kumtaka Nape kutolea ufafanuzi kuhusu kutajwa kwake kuwa mwanzilishi wa Chma cha Jamii (CCJ).
Sisi tunajua Nape amekuwa akitajwa kuwa muanzilishi wa CCJ lakini amekuwa akishindwa kukanusha tuhuma hizo yeye inakuwaje anitaje mimi kama siyo kukashifiana kusingiziana na kunivurugia? alisema Mrema.
Mrema alieleza kuwa Nape anataka kumharibia chama chake na lengo la kusema maneno hayo dhidi yake ni hatua ya mikakati mibovu iliyowekwa kwa ajili ya kuhakikisha jimbo la Vunjo linarudi CCM kitu ambacho alisema hakitafanikiwa.
Mimi ni mwanachama wa TLP tena mwenyekiti na mbunge; Nape mdomo ni wake wa kusema anayotaka..sasa naona ameamua kulipizia kwangu kama yeye alivyokuwa akitajwa muanzilishi wa CCJ..kama anataka kujua mimi ni mbunge wa chama gani akawaulize wapiga kura wangu Vunjo, alisisitiza Mrema.
MY PIC:
Nape kakosea kumtaja Mrema kama mshirika wa Kikwete.
na Rodrick Mushi, Moshi
KATIBU wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, ametupa vijembe vingine kwa Mbunge wa Vunjo Augustine Mrema, akisema hatambuliki kuwa ni wa chama cha Tanzania Labour Party (TLP) au ni Chama cha Mapinduzi (CCM).
Nape alitoa kauli hiyo kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika eneo lililoko karibu na stendi kuu ya mabasi mjini Moshi, mkoani Kilimanjaro.
Licha ya upinzani kujigamba kuwa wana nguvu ya umma lakini tukiangalia bado tunaongoza kwa kila kitu, mkoa wa Kilimanjaro tuna wabunge watano wa CCM na watatu wa CHADEMA lakini huyo mmoja wa TLP yeye hajulikani wa CCM au TLP, alikejeli Nape.
Akijibu tuhuma hizo Mrema alisema hiyo ni mipango michafu ya kumchafua na kumtaka Nape kutolea ufafanuzi kuhusu kutajwa kwake kuwa mwanzilishi wa Chma cha Jamii (CCJ).
Sisi tunajua Nape amekuwa akitajwa kuwa muanzilishi wa CCJ lakini amekuwa akishindwa kukanusha tuhuma hizo yeye inakuwaje anitaje mimi kama siyo kukashifiana kusingiziana na kunivurugia? alisema Mrema.
Mrema alieleza kuwa Nape anataka kumharibia chama chake na lengo la kusema maneno hayo dhidi yake ni hatua ya mikakati mibovu iliyowekwa kwa ajili ya kuhakikisha jimbo la Vunjo linarudi CCM kitu ambacho alisema hakitafanikiwa.
Mimi ni mwanachama wa TLP tena mwenyekiti na mbunge; Nape mdomo ni wake wa kusema anayotaka..sasa naona ameamua kulipizia kwangu kama yeye alivyokuwa akitajwa muanzilishi wa CCJ..kama anataka kujua mimi ni mbunge wa chama gani akawaulize wapiga kura wangu Vunjo, alisisitiza Mrema.
MY PIC:
Nape kakosea kumtaja Mrema kama mshirika wa Kikwete.