Nape hajui Augustino Mrema ni wa chama gani, CCM au TLP

Technician

JF-Expert Member
Mar 30, 2010
841
222
Nape ampiga vijembe Mrema



na Rodrick Mushi, Moshi




KATIBU wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, ametupa vijembe vingine kwa Mbunge wa Vunjo Augustine Mrema, akisema hatambuliki kuwa ni wa chama cha Tanzania Labour Party (TLP) au ni Chama cha Mapinduzi (CCM).

Nape alitoa kauli hiyo kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika eneo lililoko karibu na stendi kuu ya mabasi mjini Moshi, mkoani Kilimanjaro.
“Licha ya upinzani kujigamba kuwa wana nguvu ya umma…lakini tukiangalia bado tunaongoza kwa kila kitu, mkoa wa Kilimanjaro tuna wabunge watano wa CCM na watatu wa CHADEMA lakini huyo mmoja wa TLP yeye hajulikani wa CCM au TLP,” alikejeli Nape.
Akijibu tuhuma hizo Mrema alisema hiyo ni mipango michafu ya kumchafua na kumtaka Nape kutolea ufafanuzi kuhusu kutajwa kwake kuwa mwanzilishi wa Chma cha Jamii (CCJ).
“Sisi tunajua Nape amekuwa akitajwa kuwa muanzilishi wa CCJ lakini amekuwa akishindwa kukanusha tuhuma hizo…yeye inakuwaje anitaje mimi kama siyo kukashifiana kusingiziana na kunivurugia?” alisema Mrema.
Mrema alieleza kuwa Nape anataka kumharibia chama chake na lengo la kusema maneno hayo dhidi yake ni hatua ya mikakati mibovu iliyowekwa kwa ajili ya kuhakikisha jimbo la Vunjo linarudi CCM kitu ambacho alisema hakitafanikiwa.
“Mimi ni mwanachama wa TLP tena mwenyekiti na mbunge; Nape mdomo ni wake wa kusema anayotaka..sasa naona ameamua kulipizia kwangu kama yeye alivyokuwa akitajwa muanzilishi wa CCJ..kama anataka kujua mimi ni mbunge wa chama gani akawaulize wapiga kura wangu Vunjo,” alisisitiza Mrema.

MY PIC:
Nape kakosea kumtaja Mrema kama mshirika wa Kikwete.
 
Nape ampiga vijembe Mrema



na Rodrick Mushi, Moshi




KATIBU wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, ametupa vijembe vingine kwa Mbunge wa Vunjo Augustine Mrema, akisema hatambuliki kuwa ni wa chama cha Tanzania Labour Party (TLP) au ni Chama cha Mapinduzi (CCM).

Nape alitoa kauli hiyo kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika eneo lililoko karibu na stendi kuu ya mabasi mjini Moshi, mkoani Kilimanjaro.
"Licha ya upinzani kujigamba kuwa wana nguvu ya umma…lakini tukiangalia bado tunaongoza kwa kila kitu, mkoa wa Kilimanjaro tuna wabunge watano wa CCM na watatu wa CHADEMA lakini huyo mmoja wa TLP yeye hajulikani wa CCM au TLP," alikejeli Nape.
Akijibu tuhuma hizo Mrema alisema hiyo ni mipango michafu ya kumchafua na kumtaka Nape kutolea ufafanuzi kuhusu kutajwa kwake kuwa mwanzilishi wa Chma cha Jamii (CCJ).
"Sisi tunajua Nape amekuwa akitajwa kuwa muanzilishi wa CCJ lakini amekuwa akishindwa kukanusha tuhuma hizo…yeye inakuwaje anitaje mimi kama siyo kukashifiana kusingiziana na kunivurugia?" alisema Mrema.
Mrema alieleza kuwa Nape anataka kumharibia chama chake na lengo la kusema maneno hayo dhidi yake ni hatua ya mikakati mibovu iliyowekwa kwa ajili ya kuhakikisha jimbo la Vunjo linarudi CCM kitu ambacho alisema hakitafanikiwa.
"Mimi ni mwanachama wa TLP tena mwenyekiti na mbunge; Nape mdomo ni wake wa kusema anayotaka..sasa naona ameamua kulipizia kwangu kama yeye alivyokuwa akitajwa muanzilishi wa CCJ..kama anataka kujua mimi ni mbunge wa chama gani akawaulize wapiga kura wangu Vunjo," alisisitiza Mrema.

MY PIC:
Nape kakosea kumtaja Mrema kama mshirika wa Kikwete.
hata kama nimshirika wake wa kweli haya nimakosa nakubaliana na wewe mkuu! sijui kwanini ccm hawaoni mambo anayofanya nape na wakamrekebisha, MAGAMBA YANAENDELEA!
 
Kwa hili Nape hajakosea hata chembe, alichokiongea Nape ndio ukweli wenyewe, hata kama sikubaliani na baadhi ya upuuzi wa Nape lakini kwenye hili namuunga mkono kwa 100%
 
Kwa hili Nape hajakosea hata chembe, alichokiongea Nape ndio ukweli wenyewe, hata kama sikubaliani na baadhi ya upuuzi wa Nape lakini kwenye hili namuunga mkono kwa 100%

Ina maana Nape anapingana na M/Kiti wake?
Kitendo cha Nape kuwazodoa washirika wa bosi wake kwa mgongo wa upinzani kinamkera sana?....
 
Nape ampiga vijembe Mrema



na Rodrick Mushi, Moshi




KATIBU wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, ametupa vijembe vingine kwa Mbunge wa Vunjo Augustine Mrema, akisema hatambuliki kuwa ni wa chama cha Tanzania Labour Party (TLP) au ni Chama cha Mapinduzi (CCM).

Nape alitoa kauli hiyo kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika eneo lililoko karibu na stendi kuu ya mabasi mjini Moshi, mkoani Kilimanjaro.
"Licha ya upinzani kujigamba kuwa wana nguvu ya umma…lakini tukiangalia bado tunaongoza kwa kila kitu, mkoa wa Kilimanjaro tuna wabunge watano wa CCM na watatu wa CHADEMA lakini huyo mmoja wa TLP yeye hajulikani wa CCM au TLP," alikejeli Nape.Akijibu tuhuma hizo Mrema alisema hiyo ni mipango michafu ya kumchafua na kumtaka Nape kutolea ufafanuzi kuhusu kutajwa kwake kuwa mwanzilishi wa Chma cha Jamii (CCJ).
"Sisi tunajua Nape amekuwa akitajwa kuwa muanzilishi wa CCJ lakini amekuwa akishindwa kukanusha tuhuma hizo…yeye inakuwaje anitaje mimi kama siyo kukashifiana kusingiziana na kunivurugia?" alisema Mrema.
Mrema alieleza kuwa Nape anataka kumharibia chama chake na lengo la kusema maneno hayo dhidi yake ni hatua ya mikakati mibovu iliyowekwa kwa ajili ya kuhakikisha jimbo la Vunjo linarudi CCM kitu ambacho alisema hakitafanikiwa.
"Mimi ni mwanachama wa TLP tena mwenyekiti na mbunge; Nape mdomo ni wake wa kusema anayotaka..sasa naona ameamua kulipizia kwangu kama yeye alivyokuwa akitajwa muanzilishi wa CCJ..kama anataka kujua mimi ni mbunge wa chama gani akawaulize wapiga kura wangu Vunjo," alisisitiza Mrema.

MY PIC:
Nape kakosea kumtaja Mrema kama mshirika wa Kikwete.

Mzee Mrema tulikwambia ukatubishia sasa angalia aibu hii - kijana wa juzi juzi tu anakwambia maneno haya? mzee inabidi siasa uachane nazo kabisa. Huyu kijana wakati unaanzisha ulinzi shirikishi yaani sungu sungu jijini na wakati huo ukiwa Naibu waziri mkuu kama sikosei huyu kijana alikuwa O'level - hata analysis ya mambo ya siasa alikuwa bado kabisa.

Nakushauri mzee wangu uachane na hizi siasa hawa vijana hawana nia njema na wewe, mpe ujumbe Kingunge pia, wakati umeshawatupa - Pumzikeni muwe washauri tu.

Na wewe Nape mbona hata sisi hatujui upo chama gani, CCM au CCJ ?
 
ccm wamekitumia kibabu hiki sasa hivi wamekiona sio mtaji tena,wanamdump kama maalim seif,..msiwe wabishi kukubali,nape ni mdomo wa JK,kwa kuwa hana guts za kufanya maamuzi magumu,jk anamtumia nape kuongea,...kwanza alimpa udc masasi ili baadae akija kumpa hii kazi ya uvuvuzela asiweze kuikataa..,ccm ina permanent interest not permanent friends,..ila ina permanent enemy,..CDM,hawaongeki kwa miafaka ya kipumbavu,..nape hongera kwa kuwachana hao wasaliti wa wananchi(mrema,seif)ingawa wewe pia ni msaliti wa ccm kwa kuasisi CCJ
 
"Licha ya upinzani kujigamba kuwa wana nguvu ya umma…lakini tukiangalia bado tunaongoza kwa kila kitu, mkoa wa Kilimanjaro tuna wabunge watano wa CCM na watatu wa CHADEMA lakini huyo mmoja wa TLP yeye hajulikani wa CCM au TLP," alikejeli Nape
hapo ndipo akili ya Nape inapoishia kuganga politics tu. haya unao hao wabunge watano wewe ndio mwenye nguvu tumekubali sasa basi umetumia vipi uwingi wa wabunge kutatua matatizo yetu, yako wapi maji ? , huko wapi umeme? wako wapi waalimu? viko wapi vitabu na maabara mashuleni? hayo ndio matatizo ya msingi ya mtanzania na siyo kushindania idadi ya wabunge ina msaada gani kwa mtanzania hiyo??
 
Kweli Nape kaishkia akili sisiemu- hata hawajiulzi uhalali wa kile akiongeacho kwa kfup Nape anafkri kwa niaba ya sisiemu.
 
Majibu mazuri Mrema. Nape i, uropokaji wako utakufilisi kisiasa na ipo siku utajikuta upo kijiweni, yetu macho kwasasa. Waswahli walisema mbio za panya huishia sakafuni.
 
Nape Bwana Mdogo,
Unakumbuka Oktoba 2010 ulipotembelea Mangaka nilikushauri nini? Punguza sana kuongea maneno ambayo hayana mashiko. Tatizo naona zile stori unazopiga na JK off record wewe unazimwaga majukwaaani. Hebu acha hizo usije kuta watu wakikuona umeingia mahali wananyamaza ili usije kuliyapua mazungumzo yao majukwaani.

Otherwise kijana una moyo.........................................
 
"Licha ya upinzani kujigamba kuwa wana nguvu ya umma…lakini tukiangalia bado tunaongoza kwa kila kitu, mkoa wa Kilimanjaro tuna wabunge watano wa CCM na watatu wa CHADEMA lakini huyo mmoja wa TLP yeye hajulikani wa CCM au TLP," alikejeli Nape
hapo ndipo akili ya Nape inapoishia kuganga politics tu. haya unao hao wabunge watano wewe ndio mwenye nguvu tumekubali sasa basi umetumia vipi uwingi wa wabunge kutatua matatizo yetu, yako wapi maji ? , huko wapi umeme? wako wapi waalimu? viko wapi vitabu na maabara mashuleni? hayo ndio matatizo ya msingi ya mtanzania na siyo kushindania idadi ya wabunge ina msaada gani kwa mtanzania hiyo??

Very intelligent point.

Siasa za uchaguzi hizi, ukiuliza mtu, ushachaguliwa sasa, unafanya nini, anakwambia nina viti vingi bungeni!!!!
 
Back
Top Bottom