Nape: Dawa ya wezi ni kuwafunga jela, sio kuwakemea!

tpaul

JF-Expert Member
Feb 3, 2008
21,478
17,676
Moja ya tatizo ambalo limepelekea Wizara ya TAMISEMI ya Hawa Ghasia kuonekana mzigo, ni mtandao wa wizi katika halmashauri nyingi nchini. Lakini inasikitisha kwamba kamati kuu ya ccm IMEKEMEA tu wizi huo badala ya kupendekeza/kushauri wezi hao wafungwe jela. Hii kwa mujibu wa maelezo ya Nape Nnauye alipokuwa akihojiwa na waandishi wa habari.

Kwa kweli kamati kuu haijawatendea haki wananchi wanaokosa huduma za jamii kufuatia ufisadi mkubwa unaofanyika ktk halmashauri. Ni afadhali hata wangelimshauri Rais awaagize hao wezi wamrejeshee fedha walizoiba kama alivyofanya kwa wale wezi wa EPA aliowaagiza wakamrejeshea mabilioni ya fedha za umma walizokuwa wamezikwapua! Ijapokuwa njia hii nayo sio nzuri sana lakini ni nafuu kuliko 'kuwakemea' tu wezi na kuwaachia waendelee kutumbua pesa za umma.
 
Moja ya tatizo ambalo limepelekea Wizara ya TAMISEMI ya Hawa Ghasia kuonekana mzigo, ni mtandao wa wizi katika halmashauri nyingi nchini. Lakini inasikitisha kwamba kamati kuu ya ccm IMEKEMEA tu wizi huo badala ya kupendekeza/kushauri wezi hao wafungwe jela. Hii kwa mujibu wa maelezo ya Nape Nnauye alipokuwa akihojiwa na waandishi wa habari.

Kwa kweli kamati kuu haijawatendea haki wananchi wanaokosa huduma za jamii kufuatia ufisadi mkubwa unaofanyika ktk halmashauri. Ni afadhali hata wangelimshauri Rais awaagize hao wezi wamrejeshee fedha walizoiba kama alivyofanya kwa wale wezi wa EPA aliowaagiza wakamrejeshea mabilioni ya fedha za umma walizokuwa wamezikwapua! Ijapokuwa njia hii nayo sio nzuri sana lakini ni nafuu kuliko 'kuwakemea' tu wezi na kuwaachia waendelee kutumbua pesa za umma.
Ccm hawezi kuwafanya chochote. Refer, majigambo ya Kapuya, chama ni chao na serikali ni yao, hakuna wa kuwagusa,
Ccm wanacheza na maisha ya Watanzania, Waziri ateuliwe na mtu mmoja ila akifanya makosa ahojiwe na kamati kuu????? Hii iko Tz peke yake,
Ccm nashauri acheni kuoneana aibu chukueni mfano kwa wapinzani wenu Chadema,
 
Moja ya tatizo ambalo limepelekea Wizara ya TAMISEMI ya Hawa Ghasia kuonekana mzigo, ni mtandao wa wizi katika halmashauri nyingi nchini. Lakini inasikitisha kwamba kamati kuu ya ccm IMEKEMEA tu wizi huo badala ya kupendekeza/kushauri wezi hao wafungwe jela. Hii kwa mujibu wa maelezo ya Nape Nnauye alipokuwa akihojiwa na waandishi wa habari.

Kwa kweli kamati kuu haijawatendea haki wananchi wanaokosa huduma za jamii kufuatia ufisadi mkubwa unaofanyika ktk halmashauri. Ni afadhali hata wangelimshauri Rais awaagize hao wezi wamrejeshee fedha walizoiba kama alivyofanya kwa wale wezi wa EPA aliowaagiza wakamrejeshea mabilioni ya fedha za umma walizokuwa wamezikwapua! Ijapokuwa njia hii nayo sio nzuri sana lakini ni nafuu kuliko 'kuwakemea' tu wezi na kuwaachia waendelee kutumbua pesa za umma.

I afraid ni ktu hamstuki tu! Hata hizo za EPA hazikuwahi kurudi. Kwani zilienda wapi vile?
 
nape please okoa jahazi. Muenzi mandela hata kama wana ccm watakuchukia



kwani mandela alifanyaje zaidi ya kukalia kiti cha urais na kuwasamehe mafisadi wa kizungu waliomwaga damu za waafrika maelfu kwa maelfu. Zaidi alizunguka nchi mbalimbali za afrika akiwashauri wawapokee makaburu kama wawekezaji kwani ni watu wazuri. Kwa mandela tunajifunza uungwana na upendo na kuachana na visasi, kwn visasi ndio chanzo cha vita.
 
Bamiza mawe huyo maza mashavu ka bundi, piga mawe ka kule Mwanza, si mmezidisha siasa sasa subirini mawe
 
Japo maneno ya kinafiki lkn yanafurahisha masikio.......muda mwingine unaweza kusema Nape ndio anaona uchafu ndani ya CCM peke yake.
 
Ccm hawezi kuwafanya chochote. Refer, majigambo ya Kapuya, chama ni chao na serikali ni yao, hakuna wa kuwagusa,
Ccm wanacheza na maisha ya Watanzania, Waziri ateuliwe na mtu mmoja ila akifanya makosa ahojiwe na kamati kuu????? Hii iko Tz peke yake,
Ccm nashauri acheni kuoneana aibu chukueni mfano kwa wapinzani wenu Chadema,


Ni kweli kabisa mkuu. Tatizo la CCM ni hii tabia ya kulindana. Kwa mfano, Shukuru Kawambwa amekuwa akiharibu katika kila wizara anayoisimamia lakini, badala ya kufutwa kazi, Rais kikwete (binamu yake na Kawambwa) amekuwa akimhamisha kutoka wizara moja hadi nyingine. Hii sio vizuri hata kidogo.
 
kwani mandela alifanyaje zaidi ya kukalia kiti cha urais na kuwasamehe mafisadi wa kizungu waliomwaga damu za waafrika maelfu kwa maelfu. Zaidi alizunguka nchi mbalimbali za afrika akiwashauri wawapokee makaburu kama wawekezaji kwani ni watu wazuri. Kwa mandela tunajifunza uungwana na upendo na kuachana na visasi, kwn visasi ndio chanzo cha vita.

Mkuu, wizi wa mali za umma ni tofauti sana na issue ya makaburu--hazifanani hata kidogo.
 
Ilishasemwa CCM ni ukoo wa panya

Ni kweli kabisa---babu mwizi, baba mwizi, watoto wezi, wajukuu wezi, vitukuu wezi na vilembwe wezi!!!!!!! Na bado maisha yanaendelea kama kawaida kana kwamba hakuna tatizo lolote.
 
mkuu, wizi wa mali za umma ni tofauti sana na issue ya makaburu--hazifanani hata kidogo.



nafikari sehemu yoyote isiyo na demokrasia ya kweli mfumo wake ni kama ule wa makaburu. Kundi la wachache ndilo linalopora na kuneemeka na mali za umma. Na ndicho kilichokua kule a.kusini ,makaburu walineemeka kwa kubaka demokrasia na haki za weusi,wazungu wachache ndio walokua wamefaidi utajiri wa mali asili za south africa.
Nadhani ukifikiri kwa mbali zaidi utaona hata ndani ya tanzania kuna mfumo wa kikaburu unaohitaji maridhia kama ni suala la kumuenzi mandele kinyume chake ni kuwa tu kama kagame. Mfano tu unaonekana kwny uchaguzi wa nafasi ya urais,mpaka karne hii ambapo makaburu yameruhusu demokrasia lakini kwetu bado kuna makabila na kanda hazitakiwi kushika nafasi ya urais. Je,hapo tusemeje kama sio ukaburu wa kubaguana? Je,nikumuenzi mandela?
 
Kaka
Nape talatibu kaka c unajua ukisema wizi wote CCM yetu itakwisha maana
Hata mwenyekiti wetu yumo kwenye first eleven ya mafisadi nchini au
umesahau.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom