Nape: CCM kuwarejesha kwenye ukweli vijana waliopotoshwa na wapinzani

Nape acha Masihara na Vijana wa Tanzania

Mr Nape uwe unachagua nn cha kuzungumza na wapi pa kuzungumzia?
hasa kipindi hiki cha mapambano ya kuibadilisha hii nchi yetu....,
je unategemea kauli kama hizo tena unazitoa radio Clouds kwa hao vijana wanaopigika kila corner hapa nchini Tanzania..?
Labda ulikuwa unawazungumzia Vijana toka society ya Wanasiasa Mafisadi!

Je Radio Clouds ina kipindi ambacho mtu unaweza kusema kinaleta msukumo wa mtazamo wa kifikra kwa vijana wa tanzania ya leo zaidi kupiga musics 345 dayz non stop?

Vijana wa leo hapa Tanzania ni waelewa kuliko wanasiasa wanavyofikiri, mambo ya DOtCom siyo mchezo ktk upashanaji wa habari ktk dunia ya leo. Vijana wamebadikika kama sehemu ya jamii duniani.

Nape Vijana wanahitaji Opportunities ktk nchi yao sio propaganda! na wao wanastahili kupata nafasi ktk nchi yao.
tumia nafasi yako kutoa maoni na mapendekezo mbadala ktk vikao vyenu vya CC na ndani ya CCM, CCM ndiyo baba+mama wa MATATIZO

Nape kama unaweza kuuza mvuto mtaani ni nafasi pekee utumie mvuto wako ndani CC ili uweze sikilizwa na wajumbe wenzako, kama utafikiri umeshindwa kuwasilisha hoja mbadala CC, basi wache wanasiasa vijana wenzio ktk CCM waifanye kazi hiyo.

Nape kama uijuavyo CC ya CCM haipo kwa maslahi ya Taifa zaidi ya Makundi na Ubinafsi,
wakati mmekaa dodoma juzi dar UDA iliuzwa kiaina!
Watoto wa Mjini waliiba UDA yetu ambayo kwa njia moja au nyingine inawasaidia vijana ktk usafiri wa jijini Dar,
Je ww km mjumbe Kijana wa CC mbona haujatoa Taarifa ya kuulaani au kumwomba M/kiti wako kuwatetea wanafunzi - vijana kwa kuingilia kati sakata hilo kwa kutoa maagizo watu wakamatwe....?
Mtoto wa mkulima yy alitoa maagizo yale kisera coz ya kipindi hiki cha mjengoni.., but na wewe ulikuwa unayo nafasi yako ya kichama! but ndiyo hivyo ufisadi!

Kama ungeweza kusimamia mambo kama hayo yanayowahusu vijana nadhani ungekuwa ktk nafasi nzuri ya kuwazungumzia vijana matatizo yao!

Nape toa kauli nzuri zenye tija ya kutoa nafasi kwa vijana kupata nafasi ya kuijenga nchi yao kwa maendeleo yao pamoja na Taifa kwa jumla.

Tuwape opportunities!
 
hakuna kijana anayeipenda ccm kwa sasa na hata hao waliopo ccm ni kwa sababu ya njaa.chama hakina muelekeo kabisa na hakina uwajibikaji
 
<br />
<br />
hivi umekosa kazi ya kufanya tukupe mpunga uuze.. Tunajua kwamba wanaowapa kura ni akina mama sababu wana shida na kanga. Yan ccm inanuka,hakuna mwenye akili timamu anaethubutu kuitaja. Wewe unafikiri nyerere angekuwepo wewe na aliyekuweka hapo mngekuwa kama mlivyo.? C mngekuwa mnauza vinyago mwenge ss hv. Huna cha kutuambia ss hv,wkt hujui kama kuna watu wanakula mlo 1/day,


Nape we unaongea hivo maana unafikiri kwa tumbo badala ya ubongo , oky!

Take this "Mungu ana akili sana kumuua Nyerere mapema maana kama angekuwepo sasa na kuyashuhudia haya tuyaonayo angejiua mwenyewe kwa kujitundika" na wala asingesubiri kusheherekea hiyo miaka yenu 50 ya kusheherekea utajiri wa mafisadi. pumbafuuuuuu!!!

peoplezzzzzzzzz powerrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrr
 
I can not Imagine kama Nape ni average thinker this way. Nadhani hili ni tatizo la kudumu kwa baadhi ya viongozi wa CCM hasa ngazi ya Taifa.
 
[h=3][/h]
NA MWANDISHI WETU


CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kitahakikisha katika mabadiliko yake ya sasa kinawarejesha katika kuujua ukweli vijana waliopotoshwa na wapinzani hadi kufikia hatua ya kudhani hakuna mazuri yaliyofanywa tangu uhuru.

Mikakati hiyo ilisemwa jana na Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi CCM, Nape Nnauye wakati akizungumza na baadhi ya viongozi na watangazaji wa Clouds Media Group, Mikocheni Dar es Salaam, alipofanya ziara ya kujitambulisha katika wadhifa wake huo na kueleza mabadiliko yaliyofanywa na Chama, mapema Aprili mwaka huu.
Alisema, wakati wapo vijana ambao hawakuipigia kura CCM katika uchaguzi mkuu uliopita kwa sababu zinazoonekana kuwa za msingi, lakini ipo idadi kubwa ya vijana ambao walifanya hivyo kutokana na chuki tu kutokana na kushibishwa na uongo na baadhi ya vyama vya upinzani.
Nape alisema katika miaka ya karibuni hasa baada ya kupevuka kwa kiwango kikubwa mawasiliano kwa njia ya mitandao kwenye kompyuta, baadhi ya vyama hivyo vimetumia na vinaendelea kutumia mawasiliano hayo kueneza uongo kwa njia hiyo na kufanikiwa kuwanasa vijana wengi kwa kuwa ndio wanaopendelea zaidi kutumia mawasiliano hayo ya mtandao.
"Baada ya vyama vya upinzani kujua kwamba vijana wengi wanapenda zaidi upashanaji habari kwa njia ya mitandao kwenye kompyuta, kuliko mikutano ya hadhara na njia nyingine za kawaida, baadhi ya vyama hivi vimetumia sana njia hii kuwajaza uongo vijana", alisema Nape.
"Na kwa sababu uongo ukizidi kuenezwa bila kupingwa huweza kuonekana ndiyo ukweli, baadhi ya vijana wameamini uongo huo, na matokeo yake wamejenga chuki kiasi cha kutoyaamini hata mambo ya maana na ya msingi wanayoambiwa na CCM na serikali yake jambo ambalo ni hatari kwa hatma ya taifa", alisema Nape.
Alisema katika mikakati yake ya sasa CCM itahakikisha inawapa ukweli kupitia njia hiyo ya mawasiliano ya mitandao ya kwenye kompyuta kama 'face book' na kueleza matumaini yake kwamba hatua hiyo itazaa mafanikio kwa kuwa yameanza kuonekana katika hatua za awali ambazo CCM imeanza kufanya.
Nape alisema, CCM inafanya hivyo kwa kuwa bado kina uwezo wa kuongoza huku kukiwa hakuna chama cha upinzani ambacho kinaweza kujitapa kuwa kinaweza kuongoza nchi kwa uhakika ikilinganishwa na hali inayojionyesha katika vyama hivyo hadi sasa.
Alisema, mbali ya kuyaendea makundi ya vijana, CCM pia imejipanga kuyafikia kwa ufanisi zaidi makundi yote, kwa kutumia njia mbadala, ikiwemo kufuatilia kwa karibu maoni ya vyombo vya habari hasa vile vinavyoonekana kuwa makini zaidi katika kutoa habari zake.
Nape aliahidi CCM kutoa ushirikiano mkubwa kwa vyombo vya habari katika kuhakikisha vinapata habari za ukweli, sahihi na kwa wakati kuhusu chama na hata za ndani ya serikali.
"Tunaamini sisi CCM tukifungua masikio yetu vilivyo kwa vyombo vya habari tuyaweza kuongoza nchi kwa usahihi zaidi, kwa sababu ninyi vyombo vya habari ndiyo mliopo mitaani wakati mwingi, hivyo mnaweza kuwa mnayajua mengi kuliko sisi, ni vizuri tukawa tunawasikiliza na kufanyia kazi mnayosema", alisema Nape.
Katika ziara hiyo, Nape alizungumzia kwa kina dhana ya mabadiliko ndani ya Chama na utekelezwaji wake unavyoendelea na baadaye waandishi wa Clouds Media Group walipata fursa ya kuzungumza na kumuuliza maswali yaliyoona yanafaa.
Baadaye Nape akiongozwa na Mkurugenzi Mwendeshaji wa kampuni hiyo ambayo ni walimiki wa vituo vya Clouds FM, Choice FM na Clouds TV, Ruge Mutahaba alipata fursa ya kutembelea baadhi ya vituo hivyo kuona kazi zinavyofanyika.

Source: fullshangwe.blogspot.com

Ukweli pekee ambao CCM inaoweza kuwarejeshea vijana ni kuwahakikishia kuwa wanakuwa na ajira bora na za uhakika katika kuendeshea maisha yao. Serikali yoyote iliyopo madarakani haiwezi kuaminika kwa maneno matupu bali ni matendo. Kama ambavyo akina Nape wameujua ukweli na kuiamini CCM baada ya kupatiwa ajira basi wafanye hivyo kwa vijana wote. Huo ndiyo ukweli pekee utakaoweza kuwarejesha vijana

Vinginevyo wataendeleo kuamini wapinzani kwani wanawaambia ukweli kuhusu hali zao mbaya kiuchumi.
 
Kaka nape 'habari chowani'
hapo nape andika ameumia sisi siyo mazuzu kufuata upepo,
nasema tena , kwanza hatukuwahi kuwa ccm na kuwa na kadi za ccm. Acha dharau. Uturejeshe kwani sisi tumekuwa mizigo? Tatizo lenu ccm mnakuwa kama bi kirembwe katika nchi ya giningi. .....nyeusi mansema nyeupe na nyekundu mnasema njano, basi na sisi mnataka tuamini hivyo. Hizo zama zimepitwa na wakati, sasa hivi vijana tunajua nyekundu ni nyekundu na nyeusi ni nyeusi. Rudi masasi nape ukainue wakulima wa korosho. Kwa taarifa yako nape ujue kuwa vijana wengi siku hizi hawasikilizi hyo redio, imekosa mvuto kupitia mtangazaji wake yule mc wa ccm, ephraim kibonde.
Naichukia clouds fm
 
Habari chowani, kaka kwa taarifa hatujawahi kuwa wanachama wa ccm hivyo hatuwezi kurejea au kurejeshwa sehemu ambayao hatjawahi kuwepo hapo awali. Tataueni kero za wananchi. Nafurahi wewe ni wa nyumbani kabisa... Hivi kaka unajisikiaje kwa serikari inayoongozwa na chama chako kutokuwa na msimamo na maamuzi magumu? Pia elewa kuwa radio clouds fm vijana wengi hasa wanaopiga kura huwa hawasikilizi...... Wamwchoshwa na yule mc wenu mnayempa tenda, ephrahim kibonde, kwa hiyo andika hautafanikiwa kwa hili. Toeni vibanzi machoni penu kwanza ndipo ujaribu hilo unalodhamiria.
 
Kaka nape 'habari chowani'
hapo nape andika ameumia sisi siyo mazuzu kufuata upepo,
nasema tena , kwanza hatukuwahi kuwa ccm na kuwa na kadi za ccm. Acha dharau. Uturejeshe kwani sisi tumekuwa mizigo? Tatizo lenu ccm mnakuwa kama bi kirembwe katika nchi ya giningi. .....nyeusi mansema nyeupe na nyekundu mnasema njano, basi na sisi mnataka tuamini hivyo. Hizo zama zimepitwa na wakati, sasa hivi vijana tunajua nyekundu ni nyekundu na nyeusi ni nyeusi. Rudi masasi nape ukainue wakulima wa korosho. Kwa taarifa yako nape ujue kuwa vijana wengi siku hizi hawasikilizi hyo redio, imekosa mvuto kupitia mtangazaji wake yule mc wa ccm, ephraim kibonde.
Naichukia clouds fm
 
Habari chowani, kaka kwa taarifa hatujawahi kuwa wanachama wa ccm hivyo hatuwezi kurejea au kurejeshwa sehemu ambayao hatjawahi kuwepo hapo awali. Tataueni kero za wananchi. Nafurahi wewe ni wa nyumbani kabisa... Hivi kaka unajisikiaje kwa serikari inayoongozwa na chama chako kutokuwa na msimamo na maamuzi magumu? Pia elewa kuwa radio clouds fm vijana wengi hasa wanaopiga kura huwa hawasikilizi...... Wamwchoshwa na yule mc wenu mnayempa tenda, ephrahim kibonde, kwa hiyo andika hautafanikiwa kwa hili. Toeni vibanzi machoni penu kwanza ndipo ujaribu hilo unalodhamiria.
 
Nape,labda unatarget mtu kama mimi ambaye nimewahi kuwa ccm. Kwa upande wangu so far sioni hoja yoyote ambayo umewahi kuongea ikanifanya niregret kuhama chama chako.
Pia sikusubiria kuelezwa na mtu either huo unaouita uongo au ukweli kama ndio chama chako kinao na kinakutuma kuja kwangu kunipa huo ukweli! I'm a grown woman I can see 4 myself! Chadema walichofanya ni kunidhihirishia tu yale ambayo nilikua nayaona tayari na nina deal nayo kila siku.
Labda kukusaidia nikwambie jaribu kutengeneza sera zako mwenyewe kwani lazima ukumbatie failed policies za chama chako? Yani mimi nakufa njaa wewe unaniletea porojo za ccm?
Sijui elimu yako ikoje lkn naona majibu yako hayajaenda shule kabisa! Anyway at this point ccm ni sikio la kufa halisikii dawa! Pole sana!
 
Kijana kama mimi watafanyaje niwe na imani nao? Ccm sikio la kufa, waendelee na wanawake na wazee wao!
 
Huyu naye kalewa hangover kuwa watu(vijana) hufuata mkumbo, haamini kuwa kila binadamu ana utashi wake, hivyo akiona watu wanafurika jamiiforum anafikiri watu wameshawishiwa au kurubuniwa na chama fulani. Walieneza uondo kuwa jamiiforum ni mali ya CDM kumbe inamilikiwa na wanachama wa vyama vyote hususan CCM, Swali ni kwanini wasahabiki na wapenzi wengi wa CDM ndio wanaonekana kuitumia forum hii vizuri zaidi? Ni kutokana kukereketwa na mambo yanavyoendeshwa na ccm. Tunakuomba Nape badala ya kuanzisha topic na kuingia mitini uwe unadumu ili utupatie majibu muafaka wa maswali waliyonayo watu hususna vijana kuhusu mambo mbali mbali hususan ufisadi ndani ya CCM na Serikali yek. Likini ukiendelea na tabia hii ya kuingia mitina utabakia kulaamika kuwa vijana wanalishwa uongo!!
 
HIVI NI kweli tukisema kwa ujumla KUWA hakuna kilichofanyika nchini toka tupate uhuru toka kwa wakoloni Mwaka 1961?

Ni ukweli kabisa. Miaka ya sitini Tanzania ilikuwa katika level moja na nchi kama Malaysia n.k.
Leo Tanzania ipo wapi na Malaysia ipo wapi. Na mifano kama hii ipo mingi t.

Nani mwenye akili timamu anayeweza kusfia Chama na Serikali zilizoua mtandao wa reli ambayo life span yake ni muda mrefu na kujenga mtandao wa barabara ambazo life span yake ni muda mfupi tena kwa gharama kubwa ili viongozi wa CCM, Serikali yake na watoto wao(akina Rizwan) waingize maelfu ya magari makubwa ya mizigo kubeba shehena ambazo kimsingi zilitsahili kusafirishwa kwa kutumia reli kwa haraka zaidi na gharama nafuu?

Kutoakana na maelfu ya magari makubwa ya mizigo kutumia barabara hizi kwa muda mrefu. baada ya miaka 10 hizo barabara zitakuwa hazipo wakati huo huo viongozi wa CCM, Serikali yake na wototo wao watakuwa wametajirika kutokana na biashara ya usafirishaji wa mizigo. Maamuzi kama haya yanayua pia bandari zetu na kuikosesha nchi mapato.
 
Nazipokea kwa unyenyekevu MKUBWA kejeli na kasha zote...LAKINI naheshimu sana pia wale waliojaribu kujadili HOJA ...
Wametaja hapa idadi ya wanafunzi walio vyuoni KUWA NI zaidi ya 70000.... Hivi wakati tunapata uhuru wanafunzi WA Elimu ya juu kwa takwimu ZENU walikuwa zaidi ya ho NADHANI NDO MAANA Leo twasema inashuka idadi BADALA ya kuongezeka.....
Nani kawatukana vijana.? Nilichosema vijana wengi Mwaka jana walionekana mutiny ga mkono CCM, na hii NI kwa MUJIBU WA matokeo ya utafiti SI NAPE.... SABABU NYINGI ZINAZOTOLEWA KWAKWELI NYINGI SI ZA KWELI JUU YA SABABU ZA UAMUZI HUO WA VIJANA.... SASA HAPA TUSI LIKO WAPI?

KITU KIMOJA AMBACHO HUFAHAMU NI KUWA WEWE NDIO UNZIDI KUWABOA NA KUWAUDHI VIJAN HAPA NCHINI. KAMA CCM INGETAKA KUJIADDRESS NA VIJANA INGEFANYA INTERVIEW ILI KUPATA CANDIDATE MWENYE MAWAZO KAMA VIJANA WA SASA WANAVYOFIKIRI. KWA BAHATI MABAYA NAPE UNAFIKIRI KIZEE SANA, NA HII SIO MAKOSA YAKO NI MATOKEO YA MALEZI YA KIKADA ULIYOYAPATA. MFANO HAI NI PALE ULIPOVAMIA VYUO VIKUU HUSUSAN UDOM KWA KASI KUBWA NA KUFIKIA HATUA YA KUJIFANYA WEWE NDIO MHANDISI WA CHUO HICHO KWANI ULIONEKANA UKIKAGUA MIUNDO MBINU YA MAJI/MAJI TAKA. WANACHUO WALIPOPATA MATATIZO NA SERIKALI YAKO NA KULAZIMIKA NGUVU KUTUMIKA DHIDI YA WALIPOKUWA WAKIDAI HAKI ZAO ZA MSINGI ZA KUHUDHURIA INTERNSHIP UKAINGIA MITINI NA HUKUONEKANA TENA. hIZI NDIOZ AINA YA GHILIBA VIJANA WASIZOWEZA KUVUMILIA
 
Nape huo uongo uliosambazwa na wapinzani ni vema ukauweka hapa, kama unazungumzia idadi ya wanafunzi vyuoni pia usisahau na population ya wakati huo na ya sasa, ukizungumzia ukusanyaji wa kodi usisahau na viwango vya ubadilishaji pesa yetu na za kigeni kwa wakati husika, ukijadili faida tuipatayo kwenye migodi ya dhahabu usisahau kuzungumzia dhahabu iliyopatikana/kuuzwa bot na wachimbaji wa dogo vs wachimbaji wakubwa huku ukikumbuka kwamba wachimbaji wadogo fedha yao haitoki ndani ya nchi, ukijadili uadilifu serikalini usisahau kuweka takwimu za mafisadi kwenye utawala wa mwal. vs tawala zingine na hasa huu, njoo na takwimu sahihi halafu useme kwa takwimu hizo wapinzani wamedanganya hapa uone kama hatuta kupigia debe na chama chako vinginevyo wewe usijisumbue
 
kama anashindwa kufahamu kwanini vijana wanaichukia ccm hafai kuwa na cheo alichonancho ndani ya ccm
 
Hapa namtetea Nape naona mnamuonea kijana mwezenu. sikiliza kauli hii" Mzee Nyerere akuyamaliza akaja Mzee Mwinyi Miaka 10 akuyamaliza akaja Mzee Mkapa miaka 10 hakuyamaliza na mie nitamaliza miaka 10 sitoyamaliza". mwe!

Hapa sioni tatizo la Nape liko wapi! kama Rais wa nchi hajui kwa nini Tanzania ni maskini mnategemea nini hapo? katika zile ajila millioni moja alizoahidi Rais Kikwete mojawapo ni hiyo aliyopata Nape Nnauye. sasa tumuacheni kijana mwenzetu nae atengeze maisha yake kumbukeni ana familia inahitaji matunzo yake, Nape hawezi kuiga uadilifu wa Baba yake kwa sababu anajuwa matunda ya uadilifu ndani ya ccm = kufa maskini, wafananishe Timoth Apiyo na Philemon Luhanjo je maisha yao ni sawa? wote hawa wametumikia cheo kimoja pale ikulu.

Nape nakuomba ongeza ziara za kichama kwa kadili ya uwezo wako ili uvune posho za nguvu kwa haraka, mwakani ni uchaguzi mkuu ndani ya ccm huenda ukatupwa nje ya uongozi huu, ndio wakati wako sasa, kumbuka mwenyekiti wako ni kinyonga huwa hajulikani langi yake kamwe. na ningeshauri kama haujawahi kufika Marekani huu ndio wakati wako, ongea na William Malecela pangeni dili umwambie Wilson Mukama kwamba Vijana wamekualika Marekani ukafunguwe matawi kwenye majimbo 20 ili litakuongezea posho zaidi na siku za kukaa Marekani. ukipuuza ushauri huu utakuja kunikumbuka na utajuta.

ahhh aahh wewe kweli matola.umesababisha nicheke sana thats why i like jf.
 
Ww nauye acha kufuata nyayo za tambwe, unayoyatoa ni yale ambayo umealishwa na babako ccm uje kutoa porojo tu. Miaka 50 inatosha. Fuata ushauri wa matola.
 
hatua zinazochukuliwa na CCM hazitoshi......! labda yatokee maajabu toka kwa Hayati Mwalimu...

kwa kweli Jamaa wamelala totally.... mtu dhabiti na mwerevu huwa anatafakari mambo ya msingi ktk maisha pale atafutapo usingizi wake kitandani,
but hawa jamaa yaani maisha ya bata na ulinzi wa masaa 24 taifa linalowapa bado wapi?
hawajitambui wapi walipo!
 
Back
Top Bottom