Vijana wengi mlioko magamba na wale tunaoambiwa wamejiunga ni wale wanaotegemea kutumia uongozi kutafuta mali. Bali wenye wenye nia njema na taifa hili; wale wenye dhamira ya dhati ya kuondoa nchi katika lindi la umaskini na ufisadi wako kwenye vyama makini kama CHADEMA...Dah inaonekana ilikuwa ya mafanikio sana. Keep it up comrade Nnape.
Mimi nilikuwepo pale stendi,kwa kweli kama ndiyo hivi basi CCM 2015 Kazi wanayo.Kwanza nilisikiliza hoja zilizotolewa na Nape kuhusu kujivua gamba kwa kweli sikutegemea kama katibu huyu anaweza kuongea pumba kiasi hiki!eti anasema wameshajivua gamba sasa hivi ni wapya kabisa mara afananishe nyoka na nyoka wa shaba aliyenyanyuliwa na Musa,mimi nikadhani labda alivuta bangi kabla hajapanda jukwaani,sababu nyoka wa shaba hana gamba sasa unawezaje kumfananisha na magamba?alipoharibu zaidi ni pale alipoanza kuzungumzia mwafaka wa madiwani huko Arusha!hapo watu wakaanza kumzomea wakimshinika kuzungumzia tatizo la umeme lilioathiri uchumi wa nchi,lakini Nape hakusikiliza hayo malalamiko aliendelea na kuzungumzia siasa za kivuvuzela alizozoea..ndipo nikaona ni namna gani huyu bwana alivyo bogas!Stendi watu walikuwa wachache mno, hakunaanachama wapya waliopokelewa
Tehe tehe tehe tehe imenikuna hiyo post yako mkuu wametoka bila,saaafiiiiiii.Ni ukweli kuwa Nape amepokea wanachama wapya kutoka katika chuo cha SMMUCO. Lakini wanachama hawa ni mchanganyiko wa wanachama wa zamani wasiopungua 50 hamsini na wapya takriban 20. Wanachama hawa baada ya zoezi la kuapa walienda kwenye chakula cha mchana na Nape pale mjini Himo na kukodishiwa mabasi mawili aina ya Hino ya kampuni ya mabasi ya Ibra Line ya mjini Moshi. Lengo la kuwaleta wanafunzi hao mjini Moshi lilikuwa kuwapandisha tena jukwaani kupokea kadi za CCM na kwamba waliandaliwa kadi za CHADEMA watakazorudisha. Lakini hali ya mkutano ilivyokuwa ngumu kwao walilazimika kuachana na mpango huo. Awali wanyetishaji wetu kutoka katika vikao rasmi vya CCM walituhabarisha kuwa kuna mpango wa kupokea wanachama wapya 240 hapa hapa mjini Moshi. Vijana wa CDM walitanda uwanja mzima wakisubiri kuona ni akina nani hao walio amua kuwa wasaliti na kwa kweli tunamshukuru Mungu kwamba hakuna aliyejitokeza kwani kungewaka moto leo.