Nape atoa angalizo hali ya Uchumi; awaponda CHADEMA

Wadau kama kuna mtu ana nakala ya kale kawimbo kanaitwa MKE WANGU NI VUVUZELAAAA akaatacha hapa tukaskilizieee

Ushauri kwa Nape ugumu wa maisha hauko kwenye ripoti, apite tu kitaa aone tulivyopigika. Hata huo mlo mmoja ni mgogoro halafu yeye anaongelea namba za kwenye ripoti. Ccm hawajui nini wananchi wanataka na ndio safari yao ya kuzimu inakaribia
 
Lakini kwa mtazamo wangu Nape yuko sahihi kwani alichojaribu kufanya ni kutoa comparison analysis kati ya Tanzania na nchi nyingine Duniani. Kwa kuwa suala la uchumi ni la kidunia na linategemeana na nchi nyingine duniani, ni sawa kwake akifananisha.

Kuhusu hawa jamaa vibaraka wa wazungu ni kweli wanajaribu kupotosha kwa kadri wawezavyo kwani ni hao hao ndio ambao waliweka ahadi ya kuuza mfuko wa cement kwa shilingi 5
 
ndugu yangu nape na mwana ccm mwenzangu, ukuaji wa uchumi wa asia au ulaya kwa asilimia moja tu ni tofauti kubwa mno na sisi walalahoi wa afrika
 
the horse. Nachangia hapo kny cement tu. Kwa hapa kwetu inawezekana kabisa mfuko wa cement wa 50kg kuuzwa kwa sh elf 5 au chini ya hapo, lkn sio sh5 ulizo sema wewe.

Kuna mdau mmoja alitoa mchanganuo mzuri sana na wakueleweka wa jinsi uwezekano wa kuzalisha cement ambapo nchi kama india inatumia.

Nchi yetu ni tajiri sana kwa rasilimali kuliko hata uk, lakini viongozi wajinga kama nepi ndio wametufikisha hapa na kuwa matonya.
 
Pole sana kijana mzee Nape, inaonyesha dhahiri kwamba hujui kulinganisha masuala ya sayari Dunia.Hao wanaochangisha wananchi hawajawalazimisha.

Hizo nchi ulizozitaja hazipo ulimwengu wa tatu kama TZ. Huwezi kuwaaminisha watanzania kwa mipango ya CCM ya sasa ambayo imewashusha mgongoni wakulima na wafanyakazi na kuwabeba matajiri na wafanyabiashara.

Sasa ondoeni ktk bendera ya CCM alama ya jembe na nyundo na wekeni alama ya gari na mzani maana ninyi si wajamaa tena.
 
  1. Ukuaji shughuli za utoaji huduma ya elimu ulikuwa kwa 7.4%(2011-12)ukilinganisha na 7.3%(2010-11).hapa japo nafuu..
  2. Ukuaji wa sekta ya afya uliporomoka toka 6.9%(2010-11)mpaka 5.4%mwaka (2011/12)...
  3. Maeneo ambayo ni ndoto kufikia malengo ya milenia ni pamoja na vifo vya watoto wachanga na walio chini ya 5 years!..
  4. Kwa mujibu wa Wassira lengo lingine la mkukuta mbalo ni ndoto kutimia ni kupunguza umasikini wa wananchi wanaoishi kwa chini ya $1kwa siku.
  5. Kiwango cha uchumi kwa mwaka 2011-12 kilikuwa kwa 6.4% ikilinganishwa na 7.0%(201-11).ukuaji huu ni chini ya shabaha ya mkukuta 11.
  6. Shabaha ya Mkukuta 11ilikuwa ukuaji wa wastani wa 8%-10%
  7. ukuaji wa Sekta ndogo ya ujenzi uliporomoka toka 10.2%(2010-11) mpaka 9.0%(2011-12).
  8. ukuaji wa Sekta ya umeme na gas uliporomoka toka 10.2%(2010-11)mpaka 1.5%(2011-12)
  9. ukuaji wa shughuli za Uzalishaji viwandani uliporomoka toka 7.9%(2010-11) mpaka 7.8% (2011-12).

Sijui kama Katibu Mwenezi alifuatilia Bunge au alisimuliwa!

Nape ana matatizo sana ya upembuzi wa masuala yote ya kiulimwengu.itoshe tu kusema kwamba ajifunze umakini wa JJM pale CDM.
 
One of the very best reason why I admire CCM is that, her members always compare themselves with failures, they never ever compare one another with successors. For example economy growth success is compared with economy crisis countries, declining of level of education they compare with worst countries, until the day when our country will be on top down to the list in every thing, thereby the song shall be comparing test of time (Oooooh bwana, wapinzani mavuvuzela tu, mwaka juzi tulikuwa juu sana!!!!!). Poor Chama cha Mapinduzi

Right meeeen! But the way nape is there's no need of using English b'se the guy is lowly to the language.
 
Lakini kwa mtazamo wangu Nape yuko sahihi kwani alichojaribu kufanya ni kutoa comparison analysis kati ya Tanzania na nchi nyingine Duniani. Kwa kuwa suala la uchumi ni la kidunia na linategemeana na nchi nyingine duniani, ni sawa kwake akifananisha.

Kuhusu hawa jamaa vibaraka wa wazungu ni kweli wanajaribu kupotosha kwa kadri wawezavyo kwani ni hao hao ndio ambao waliweka ahadi ya kuuza mfuko wa cement kwa shilingi 5

Kwa hiyo na wewe unajiingìza kichwa*2? Kwa nn ajilinganishe na nchi zilizo endelea?kwa nini asijilinganishe na hata na somalia au botswana?nyie nyote wenye mawazo kama ya Hiyo nepi tutawatafutia pumpers mpunguze harufu chafu ya akili zenu.
 
Nape kachagua nchi zenye matatizo ya kiuchumi kwa mwaka huu.. Tanganyika yetu ina matatizo ya kiuchumi muda wote Magamb watakapokuwa madarakani
 
Kama kweli hali ndiyo ilivvyo kulikuwa na haja gani kwa rais JK kuwaita wenyeviti wa kamati za kudumu za bunge kuwaelezea hali ya uchumi nchini ilivyo mbaya kiasi cha kushindwa kuongeza bajeti ya wizara ya uchukuzi kama kamati zilivyoshauri?

Watanzania wa leo bwana Nape si wadanganyika wa miaka ile,pia ni kwanini kila bajeti inapotaka kusomwa lazima mhangaike kulainisha wqabunge wenu kupitia caucus ya chama.Tuwe wakweli na wazalendo kwa nchi na watu wake
 
Ndugu wana JF,

For the past few months nimekuwa nikisikiliza viiongozi wetu wakisema kuwa ukilinganisha tanzania na mataifa mengine mengi economically we are better off....lakini hiyo dhana mimi siikubali...we should not be comparing ourselves with other countries...we should look at ourselves and compare ourselves....kama jirani yako anaishi kwenye nyumba ya manyasi na yako ni ya mabati it does not mean umefika kileleni...you should strive to build a better house for yourself sio kubweteka because you are better off than your neighbour....

Nawasilisha
 
Back
Top Bottom