Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,883
- 6,884
Kuna dalili za wazi Nape jitihada zake za kusafisha na kukijenga chama cha kisiasa kilichoshika dola nchini CCM kugonga mwamba kwa miaka kadhaa, huku jitihada zake zikionekana kugtoungwa mkono kila kukicha na baadhi ya vijana wenzake waliotegemewa kuwa pamoja katika vita hivyo kuamua kutangaza hadharani kuunga mkono mmoja wa wale vinara watatu waliotakiwa kujiondoa la sivyo wapewe barua wa kuwajibishwa ndani ya CCM jitihada ambazo ziliungwa mkono na aliyekuwa Katibu Mkuu kipindi kilichopita Mukama.
Nape anaonekana dhahiri kubaki peke yake katika safu ya juu kupigania anachokiamini kwani Katibu Mkuu wa sasa kuwa mwanasiasa zaidi ya ukweli wa maisha yake, historia yake pamoja na mazira ya nafasi aliyokirimiwa.
Mahojiano kwenye moja ya chombo cha habari karibuni Nape anaonekana kushangazwa na vyombo vya usalama kutofanya jitihada za uvunjaji wa amani na mauaji yenye utata katika mikutano ya hadhara kwenye mikutano ya vyama vya siasa na nyumba za kuabudia, serikali ikiunda kamati za uchunguzi bila kuja na majibu kitu ambacho amekitafsiri kama ni vyombo vinavyoundwa kuficha uozo wa kile kinachoendelea.
Hali halisi ya jitihada za Nape zinaonekana kugonga mwamba na pengine kubaki peke yake kati ya viongozi wa juu chamani wanaohangaikia kuondoa ufisadi kwa kukisafisha chama, na wale walio pamoja naye pengine ni kundi kubwa ambalo halina sauti ya juu ndani ya chama, matoke ni viti vya peke yake.
Anachokipigania Nape ndani ya CCM kifalsafa hakitofautiani na kile kilichomo ndani ya sera zinazoimbwa na kuhubiriwa na Chadema katika mikutano yao na katika jopo lao kwa jukwaa la chama cha upinzani bungeni.
Nape alionekana kuwa na sauti ya kusikika mbali siku za nyuma kuisimanga Chadema na viongozi wake, siku za karibuni ameonekana kuwa mpole, si dalili wazi kwamba yuko likizoni ingawa anaendelea na mikutano kuzunguka sehemu mbalimbali nchini, kuna dalili ya kuafiki jitihada za wahasimu wa CCM ambao ni Chadema, jambo ambalo hawezi kuliweka wazi kwa vile atakuwa amefanya makosa makubwa kwa vile yeye ndiye msemaji mkuu wa chama cha CCM kwa sasa ingawa damuni mwake kuna dalili za wazi za kuwa na chembechembe nyekundu na nyeupe za Chadema.
Siku Nape atakapotangaza kuchoshwa na CCM na kuamua kujiunga na makamanda wa M4C dhoruba yake ndani ya CCM italeta mafuriko makubwa ambayo CCM itashindwa kuhimili kishindo hicho kuliko wale ambao CCM inawatumia kudhofisha upinzani toka ndani ya ngome ya upinzani.
Nape anaonekana dhahiri kubaki peke yake katika safu ya juu kupigania anachokiamini kwani Katibu Mkuu wa sasa kuwa mwanasiasa zaidi ya ukweli wa maisha yake, historia yake pamoja na mazira ya nafasi aliyokirimiwa.
Mahojiano kwenye moja ya chombo cha habari karibuni Nape anaonekana kushangazwa na vyombo vya usalama kutofanya jitihada za uvunjaji wa amani na mauaji yenye utata katika mikutano ya hadhara kwenye mikutano ya vyama vya siasa na nyumba za kuabudia, serikali ikiunda kamati za uchunguzi bila kuja na majibu kitu ambacho amekitafsiri kama ni vyombo vinavyoundwa kuficha uozo wa kile kinachoendelea.
Hali halisi ya jitihada za Nape zinaonekana kugonga mwamba na pengine kubaki peke yake kati ya viongozi wa juu chamani wanaohangaikia kuondoa ufisadi kwa kukisafisha chama, na wale walio pamoja naye pengine ni kundi kubwa ambalo halina sauti ya juu ndani ya chama, matoke ni viti vya peke yake.
Anachokipigania Nape ndani ya CCM kifalsafa hakitofautiani na kile kilichomo ndani ya sera zinazoimbwa na kuhubiriwa na Chadema katika mikutano yao na katika jopo lao kwa jukwaa la chama cha upinzani bungeni.
Nape alionekana kuwa na sauti ya kusikika mbali siku za nyuma kuisimanga Chadema na viongozi wake, siku za karibuni ameonekana kuwa mpole, si dalili wazi kwamba yuko likizoni ingawa anaendelea na mikutano kuzunguka sehemu mbalimbali nchini, kuna dalili ya kuafiki jitihada za wahasimu wa CCM ambao ni Chadema, jambo ambalo hawezi kuliweka wazi kwa vile atakuwa amefanya makosa makubwa kwa vile yeye ndiye msemaji mkuu wa chama cha CCM kwa sasa ingawa damuni mwake kuna dalili za wazi za kuwa na chembechembe nyekundu na nyeupe za Chadema.
Siku Nape atakapotangaza kuchoshwa na CCM na kuamua kujiunga na makamanda wa M4C dhoruba yake ndani ya CCM italeta mafuriko makubwa ambayo CCM itashindwa kuhimili kishindo hicho kuliko wale ambao CCM inawatumia kudhofisha upinzani toka ndani ya ngome ya upinzani.