Nape asema CCM ilimsimamisha Matata kugombea umeya Ilemela

DR. MWAKABANJE

JF-Expert Member
Nov 7, 2012
1,976
3,122
Ni kwa muda mrefu sasa chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimekuwa kikilalamikia tabia ya CCM kuingilia chaguzi mbalimbali nchini kama vile chaguzi za mameya wa majiji na manispaa kama ilivyotokea Arusha na Mwanza.

Hivi karibuni kuliibuka mgogoro mkubwa kati ya CHADEMA na CCM, juuu ya uchaguzi wa meya wa manispaa ya ilemela ukiachiliambali mgogoro mwingine wa mipaka ya halmashauri ya manispaa ya ilemela, mgogoro huo pia ulipelekea baadhi ya madiwani wa CHADEMA kuwekwa rumande kwa sababu eti walikiuka maagizo halali ya mahakama ya kuwataka kusitisha uchaguzi wao wa ndani ya kumteua mgombea wa umeya wa ilemela bila ya kuwepo diwani mwingine Henry Matata ambaye alikuwa alisimamishwa uanachama na kamati kuu ya Chadema hivyo kukimbilia mahakamani hivyo kuendelea na wadhifa wake wa udiwani, nadhani hakuna haja ya kuyaongelea mengi juu ya matata kwani mengi yamekwisha semwa kwenye jukwaa hili.

Sasa basi juzi tu Katiku wa itikadi na uenezi wa ccm Nape, alikuwa akihojiwa na kituo kimoja cha redio cha METRO FM cha jijini Mwanza kinachosemekana kumilikiwa na kada maarufu na tajiri mkubwa Gachuma, pamoja na mambo mengine nape aliulizwa kuwa kama ni kweli CCM ilishiriki kuhujumu uchaguzi huo kama inavyolalamikiwa na wengi hasa CHADEMA, alisema "ndiyo CCM tulimteua matata agombee umeya wa ilemela na naibu meya atoke ccm ili kuondoa hali ya kisiasa iliyokuwepo ili kulete maendeleo".

kwa maneno machache haya ya nape, inaonyesha bila shaka yoyoyte jinsi CCM wanavyokiuka misingi ya Demokrasia na utawala bora kwa kujiuliza maswali yafuatayyo:-

1. inaonyesha ni jinsi gani wamekuwa wakivuruga chaguzi hizi na kutuletea maafa kama yale ya Arusha kwani hata sheria za uchaguzi zilikiukwa wakati wa kumchagua meya huyu (idadi ya wajumbe).

2. Inaonyesha jinsi ambavyo wamekuwa wakiingilia mihimili ya dola kama mahakama kwani Nape anatuonyesha jinsi gani ambavyo inaonyesha wallingilia hata maamuzi ya mahakama ya kuwakamata madiwani wa CHADEMA kwa maslahi yao.
3. Mwisho, bila shaka yoyote ametueleza wazi kuwa diwani matata ni wa CCM na wala si wa mahakama kama yeye anavyojiita, na pia kwa kiasi kikubwa hawakilishi wananchi waliomchagua kwani hakuchaguliwa na idadi ya wajumbe inayotambulika kisheria.
 
Hili la Matata ni mfano hai wa Kuwataka wana Chadema kuwa Macho na Mamluki. Hapa kosa si Nape Bali Chadema kwa kumpokea Na kumruhusu Matata agombee ilihali alitapikwa na Ccm.
 
Hakuna mtu awaye yote anayeweza kuzuia wimbi la mabadiliko. Wakati umefika na Tanzania ni lazima ikombolewe kwa heri ama kwa shari. Kwa heri kama CCM wataongoka na kuacha demokrasia ichukue mkondo wake, kwa shari kama watajaribu kuzuia wimbi hili la mabadiliko. Ningewashauri CCM ili kuzuia shari waache demokrasia ichukue mkondo wake.
 
wasaliti wote tunawahesabu mmoja mmoja,tunarekodi idadi yao na majina,watatusaidia katika somo la historia topic ya"uhuru wa kweli wa tanganyika kutoka wakoloni weusi"
 
We have forced them to opt for short term strategy. Ni wazi kuwa huyo Matata hatakuwa Meya kwa miaka mia moja. Ngoma inogile, poor NEPI has lost the focus.
 
tatizo ni kwamba chadema hawana wanasiasa makini ndio maana wanategemea watoke ccm na kwenda chadema,nao wanaenda chadema huku mioyo yao na mapenzi yao yapo ccm,itawagharimu sana hii kitu wapendwa,niliwahi sema kuwa chadema wengi ni ccm ila wengine hawajijui,inajidhihirisha sasa.:target:
 
Acha kuweweseka,nape amesema lengo lilikuwa ni kuondoa ukakasi wa hali ya kisiasa uliokuwepo ndio mana wakakubaliana kuwe na meya kutoka chadema na naibu atoke ccm ili kuwaletea wananchi maendeleo
 
Watu hujifunza kwa makosa hilo ni fundisho kwa cdm nadhani somo limeeleweka hakuna magamba kupewa nafasi hata kama ni muadilifu cdm tengenezeni wanasiasa wa kwenu wapyaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa bila chenga
 
Inasemekana kwamba tofauti ya msingi sana kati ya binadamu na wanyama au viumbe wengine ni AIBU , sasa ukiona mtu anakosa aibu iwe kwa ajili ya cheo chake ( NAPE ) au kwa ajili ya tamaa ya madaraka ( MATATA ) basi ni lazima tuamini kwamba ana matatizo ya akili , TAFAKARI !
 
Hizi fogery za CCM tena bila AIBU zinazidi kuonesha umhimu wa KATIBA mpya. Ndiyo kwenye katiba mpya tupendekeze Mameya wa majiji na manispaa wawe wanapigiwa kura na wananchi, badala ya kupigiwa kura na madiwani tu ili kuondoa hizi RAFU za CCM kwa kusaidiwa na wakurugenzi kama huyu Willison Kabwe.

Wenzetu waliotutangulia kwenye demokrasia ndivyo wanavyofanya. Meya wa London, Paris, New York to mention the few wanapigiwa kura na wananchi.

Ona Sasa Municipaa ya ILemela ina Meya Ex-Jambawazi Mhe (SIC!) Matata aka Magnum.
 
Ni kwa muda mrefu sasa chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimekuwa kikilalamikia tabia ya CCM kuingilia chaguzi mbalimbali nchini kama vile chaguzi za mameya wa majiji na manispaa kama ilivyotokea Arusha na Mwanza.

Hivi karibuni kuliibuka mgogoro mkubwa kati ya CHADEMA na CCM, juuu ya uchaguzi wa meya wa manispaa ya ilemela ukiachiliambali mgogoro mwingine wa mipaka ya halmashauri ya manispaa ya ilemela, mgogoro huo pia ulipelekea baadhi ya madiwani wa CHADEMA kuwekwa rumande kwa sababu eti walikiuka maagizo halali ya mahakama ya kuwataka kusitisha uchaguzi wao wa ndani ya kumteua mgombea wa umeya wa ilemela bila ya kuwepo diwani mwingine Henry Matata ambaye alikuwa alisimamishwa uanachama na kamati kuu ya Chadema hivyo kukimbilia mahakamani hivyo kuendelea na wadhifa wake wa udiwani, nadhani hakuna haja ya kuyaongelea mengi juu ya matata kwani mengi yamekwisha semwa kwenye jukwaa hili.

Sasa basi juzi tu Katiku wa itikadi na uenezi wa ccm Nape, alikuwa akihojiwa na kituo kimoja cha redio cha METRO FM cha jijini Mwanza kinachosemekana kumilikiwa na kada maarufu na tajiri mkubwa Gachuma, pamoja na mambo mengine nape aliulizwa kuwa kama ni kweli CCM ilishiriki kuhujumu uchaguzi huo kama inavyolalamikiwa na wengi hasa CHADEMA, alisema "ndiyo CCM tulimteua matata agombee umeya wa ilemela na naibu meya atoke ccm ili kuondoa hali ya kisiasa iliyokuwepo ili kulete maendeleo".

kwa maneno machache haya ya nape, inaonyesha bila shaka yoyoyte jinsi CCM wanavyokiuka misingi ya Demokrasia na utawala bora kwa kujiuliza maswali yafuatayyo:-

1. inaonyesha ni jinsi gani wamekuwa wakivuruga chaguzi hizi na kutuletea maafa kama yale ya Arusha kwani hata sheria za uchaguzi zilikiukwa wakati wa kumchagua meya huyu (idadi ya wajumbe).

2. Inaonyesha jinsi ambavyo wamekuwa wakiingilia mihimili ya dola kama mahakama kwani Nape anatuonyesha jinsi gani ambavyo inaonyesha wallingilia hata maamuzi ya mahakama ya kuwakamata madiwani wa CHADEMA kwa maslahi yao.
3. Mwisho, bila shaka yoyote ametueleza wazi kuwa diwani matata ni wa CCM na wala si wa mahakama kama yeye anavyojiita, na pia kwa kiasi kikubwa hawakilishi wananchi waliomchagua kwani hakuchaguliwa na idadi ya wajumbe inayotambulika kisheria.

FULL name ya MATATA please!!!
 
Hakuna mtu awaye yote anayeweza kuzuia wimbi la mabadiliko. Wakati umefika na Tanzania ni lazima ikombolewe kwa heri ama kwa shari. Kwa heri kama CCM wataongoka na kuacha demokrasia ichukue mkondo wake, kwa shari kama watajaribu kuzuia wimbi hili la mabadiliko. Ningewashauri CCM ili kuzuia shari waache demokrasia ichukue mkondo wake.

utabakia na ngonjela zako hizi
 
Acha kuweweseka,nape amesema lengo lilikuwa ni kuondoa ukakasi wa hali ya kisiasa uliokuwepo ndio mana wakakubaliana kuwe na meya kutoka chadema na naibu atoke ccm ili kuwaletea wananchi maendeleo

Nape na CCM yake walikubaliana na nani Meya(Matata) atoke CHADEMA?
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom