nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
NA MWANDISHI WETU
24th July 2012
Katibu Mwenezi wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Nape Nnauye
Katibu Mwenezi wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Nape Nnauye, amepiga marufuku wafanyabiashara ndogo ndogo kutozwa ushuru katika Manispaa ya Kigoma/Ujiji.
Nnauye alitoa agizo hilo jana katika uwanja wa Senta, manispaa ya Kigoma/Ujiji.
"Lengo la kuja Kigoma na timu yangu ni kutatua matatiza ya wananchi na siyo marumbano na matusi, bali nikuhakikisha serikali ya CCM inawalinda wananchi wote wanaofanya biashara ya mchicha, nyanya, maandazi, vitumbua na vitunguu, ni marufuku kutozwa ushuru na atakayekiuka agizo hilo atachukuliwa hatua kali za kisheria" alisema.
Aliyataja matatizo ambayo ni kero kwa wanachi wa Kigoma kuwa ni kuwatoza wakinamama wajawazito fedha wakati wa kujifungua, watoto chini ya miaka 5 kulipa fedha kwa ajili ya matibabu, wazee kulipa fedha za matibabu, akisema hayo ni makosa kwani serikali ya CCM ilishakataza siku nyingi makundi hayo kulipa fedha za matibabu.
Alisema kero nyingi ni watendaji wa kata kuchukua kitu kidodo kwa ajili ya kuandika barua za dhamana, wanafunzi kurudishwa nyumbani kwa ajili ya michango mbalimbali pamoja na ada kuonya kuwa watakaobainika wanafanya hivyo watafukuzwa kazi.
Alisema kero kubwa kwa wananchi wa Kigoma ni maji ambayo hayatoki lakini wanatozwa fedha za bili na kueleza kwamba serikali ya CCM imeagiza mita 4,000 ili kila mwananchi afungiwe mita kuondoa malalamiko ya kutoa fedha bila ya maji kutoka.
Aidha alisema serikali ya CCM imeazimia kuimarisha reli, bandari pamoja na miundombinu ya barabara za lami ili kukuza kilimo katika mikoa ya Kigoma, Rukwa na Kagera.
CHANZO: NIPASHE