TandaleOne
JF-Expert Member
- Sep 4, 2010
- 1,644
- 709
Ameandika katika Wall yake asubuhi hii kuwa;
https://www.facebook.com/nape.mosesnnauye
"...UMOJA NI USHINDI..."
Pamoja tunaweza kufikia lengo., lakini kuhusu dhamira ya kweli hili lisibaki kwa viongozi pekee bali na kwa wanachama pia. Yapo mambo(nayo ni mengi) viongozi hawawezi kuyafanya bila msaada wa wanachama, kama wanachama nao watakuwa na dhamira ya kweli ya kukiona Chama chao kinasimama katika Asili ya kuundwa kwake basi mengi tunaweza kufanikiwa.
Katika wanachama wapo wanachama viongozi na wapo wanachama wasio viongozi, katika ngazi za uongozi wapo viongozi wakuu na viongozi wa kawaida, CCM inayo safu ya uongozi kuanzia mashina na hawa kwa pamoja kama wanachama na kama viongozi lazima nao wawajibike na wawe na dhamira thabiti.
Likija suala la utendaji unaolenga kukisaidia Chama kuondokana na changamoto zake za sasa na kupiga hatua zaidi za kimaendeleo, watu tumekuwa na tabia ya kurudi nyuma na kuona kuwa jambo hili ni la fulani ama anaweza kulifanya fulani na kusahau kuwa fulani ni nafsi ambayo nayo inatamani jambo hilo lifanywe na fulani, mwisho wa siku mambo tunayoyataka yafanyike hayafanyiki. Ndipo tunaporudi kwenye falsafa ya umoja katika upangaji na ufanikishaji wa mipango yetu kama Chama.
"..UMOJA NI USHINDI.."
https://www.facebook.com/nape.mosesnnauye
"...UMOJA NI USHINDI..."
Pamoja tunaweza kufikia lengo., lakini kuhusu dhamira ya kweli hili lisibaki kwa viongozi pekee bali na kwa wanachama pia. Yapo mambo(nayo ni mengi) viongozi hawawezi kuyafanya bila msaada wa wanachama, kama wanachama nao watakuwa na dhamira ya kweli ya kukiona Chama chao kinasimama katika Asili ya kuundwa kwake basi mengi tunaweza kufanikiwa.
Katika wanachama wapo wanachama viongozi na wapo wanachama wasio viongozi, katika ngazi za uongozi wapo viongozi wakuu na viongozi wa kawaida, CCM inayo safu ya uongozi kuanzia mashina na hawa kwa pamoja kama wanachama na kama viongozi lazima nao wawajibike na wawe na dhamira thabiti.
Likija suala la utendaji unaolenga kukisaidia Chama kuondokana na changamoto zake za sasa na kupiga hatua zaidi za kimaendeleo, watu tumekuwa na tabia ya kurudi nyuma na kuona kuwa jambo hili ni la fulani ama anaweza kulifanya fulani na kusahau kuwa fulani ni nafsi ambayo nayo inatamani jambo hilo lifanywe na fulani, mwisho wa siku mambo tunayoyataka yafanyike hayafanyiki. Ndipo tunaporudi kwenye falsafa ya umoja katika upangaji na ufanikishaji wa mipango yetu kama Chama.
"..UMOJA NI USHINDI.."